Home » » WENYE ULEMEVU WAHIMIZWA KUJITOKEZA KUHESABIWA

WENYE ULEMEVU WAHIMIZWA KUJITOKEZA KUHESABIWA


Festus Pangani, Njombe
Mkuu wa Mkoa wa Njombe Kaptein Mstaafu Aseri Msangi ameitaka jamii kutoa taarifa sahihi za watu katika Kaya husika ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa za watu wenye ulemavu wakati wa zoezi la sense ya watu na makazi.

Katain Msangi aliyasema hayo jana wakati akifungua semina na wawakilishi wa watu wenye ulemavu kutoka Wilaya zote za Mkoa wa Njombe juu ya Umuhimu wa sensa ya watu na makazi.

Aliwataka wakuu wa kaya wakuu wa Kaya kutoa ushirikiano kwa makarani wa sensa wakati wa zoezi hiilo linalolenga kupata takwimu sahihi kwa maendeleo ya nchi.
Alisema kuwa ni vyema kuandaa taarifa kamilia za kaya zao endapo hawatakuwa nyumbani siku ya zoezi hilo ili kuondoa usumbufu na upotoshaji wa habari ambao unaweza kujitokeza kutokana na kukosekana kwao katika kaya zao wakati wa zoezi.
Awali akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mkuu wa Wilaya ya Njombe Sarah Dumba amewataka watu wenye ulemavu kuelewa kuwa sensa ya watu na makazi ni haki ya kila mtu hivyo wawe tayari kwa kuhesabiwa.

Sensa ya watu na makazi hufanyika kila baada ya miaka kumi ambapo kwa mwaka huu inatarajiwa kufanyika kwa siku saba kunzia Agosti 26 Mwaka Huu.
Blogzamikoa

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa