NEWS ALERT TUKIO KATIKA PICHA: WATU WANNE WAMEFARIKI PAPO HAPO BAADA YA KUDONDOKEWA NA KUFUNIKWA NA LORI LA MIZIGO , MTONI ILEMBULA USIKU WA KUAMKIA LEO..

 Watu wanne wamefariki papo hapo Saa kumi usiku leo baada ya kudondokewa na Lori la mizigo , Lililopindukia katika mto njia panda ya kuelekea Ilembula, kutokana na kufunikwa na Lori hilo watu hao wameendelea kuwa chini ya Lori hilo na Kazi ya kuwatoa inaendelea kufanyika sasa.
 Lori hilo la mizigo likiwa limedondoka Chini ya Mto njia panda ya Ilembula huku  watu wanne wakiwa wamefunikwa.
 Baadhi ya watu wakiwa wanashuhudia tukio la ajali huku wengine wakijipanga jinsi ya kuwaokoa walifunikwa na kifusi.
 Baadhi ya mizigo ikiwa imedondoka katika mto
 Hivi ndivyo Lori linavyo onekana likiwa limedondoka chini ya mto eneo la njiapanda Ilembula
 Mashuhuda wakiwa wanaongezeka kufika katika eneo la Tukio

 Kazi ya uokoaji ikiwa imeanza
 Lori la mizigo likiwa limedondoka
 Picha zote na Njombe yetu Blog

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

CHADEMA MAKETE WAFANYA UCHAGUZI MKUU KWA MARA YA KWANZA‏

 Jiunge na Huduma ya Tone Mobile News Bure kabisa kupitia Whatsapp yako na uwe wa kwanza kupata kile kinachotokea ni Rahisi sana Ingia katika uwanja wa kuandika ujumbe mfupi wa maneno katika Whatsapp yako kisha andika TONE MOBILE NEWS tuma kwenye namba 0756364660 utapokea ujumbe kuwa umeunganishwa.



 Msimamizi wa Uchaguzi Bw. Alfred Kayombo (kulia) akimtangaza mshindi wa nafasi ya mwenyekiti Bw. Ibrahim Ngogo.
Kwa mara ya kwanza katika historia, chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) wilaya ya Makete mkoani Njombe kimefanya uchaguzi wa uongozi mbalimbali ambapo Bw. Ibrahim Ngogo amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa chama hicho wilaya.

Akitangaza matokeo msimamizi wa uchaguzi huo Bw. Alfred Kayombo amesema Bw. Ibrahim Ngogo amepata kura 25 akifuatiwa na Isaac Sanga aliyepata kura 6 na Shaaban Mkakanze aliyepata kura 1

Bw. Kayombo amesema kutokana na umuhimu wa demokrasia ndani ya chama hicho, wameamua kufanya uchaguzi huo kwa mara ya kwanza toka chadema iingie wilayani hapa, hivyo kuonesha kuwajali wanachama wake

Mbali na viongozi hao wa juu wa chama pia Bw. Lazaro Chaula amechaguliwa kuwa katibu mwenezi wa Chadema wilaya ya Makete kwa kupata kura 30, Bi. Rose Mbilinyi amechaguliwa kuwa Mtunza hazina wa wilaya kwa kupata kura 26

Aidha Bw. Atukuzwe Mahenge amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa baraza la vijana (BAVICHA) wilaya na Bw. Shadraack Mwachota akichaguliwa kuwa katibu wake na wote wamepita bila kupingwa

Bi. Beatrice Kyando amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa baraza la wanawake wa chadema wilaya (BAWACHA), Bi Christina Timoth akichaguliwa kuwa katibu wa BAWACHA, na Bi. Mariam Asheli akichaguliwa kuwa Katibu wa uhamasishaji wa BAWACHA na wote wamepita bila kupingwa

katika uchaguzi huo pia Bw. Abiud Elia amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa baraza la wazee kwa kura 3, Abeli Juma Sanga akipata kura 1 na kuchaguliwa kuwa Makamu mwenyekiti, pamoja na Simon Nyasanga kuwa katibu wa baraza la wazee wilaya

Katika hatua nyingine wamechaguliwa wajumbe 4 waliochaguliwa kuingia kwenye kamati tendaji ambao ni John Sanga, Patison Pela,Orignal Sanga na Alafat Msigwa, huku Bw.Illomo Werner Naftal akichaguliwa kuwa mwakilishi wa wilaya kwenye mkutano mkuu taifa.

Akiahirisha mkutano huo mwenyekiti wa Chadema wilaya Bw. Ibrahim Ngogo amewasihi wajumbe kuondoa makundi na kutokubali kutumia kwa ajili ya kukibomoa chama na badala yake washikamane wawe kitu kimoja kukijenga chama

"Makamanda uchaguuzi umeisha haitakiwi tuwe na makundi, tushikamane kukijenga chama chetu, hilo ndilo la msingi kwa sasa, sisi viongozi mtupe ushirikiano" amesema Ngogo
Na Edwin Moshi, Makete
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

SHULE YA SEKONDARI IWAWA WILAYANI MAKETE YATOA SIRI YA KUFANYA VIZURI MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2014‏


Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 



Makamu mkuu wa shule ya sekondari Iwawa Fadhili Dononda akizungumza na mwandishi wetu ofisini kwake hii leo.Ikiwa zimepita siku chache tangu kutangazwa matokeo ya kidato cha sita mwaka huu, shule ya sekondari Iwawa iliyoko wilayani Makete mkoani Njombe imetoa siri ya mafanikio ya wanafunzi wake kufaulu na kushika nafasi ya nne kitaifa. 
 
Akizungumza na mwandishi wetu ofisini kwake Makamu mkuu wa shule hiyo Mwl. Fadhili Dononda amesema miongoni mwa sababu hizo ni pamoja na wanafunzi hao kuwa na utayari wa kusoma hivyo wanafunzi hao hawakuwa walevi wala watoro bali walikuwa wakizingatia masomo. 
 
Amesema kutokana na wanafunzi hao kutopenda utoro wala ulevi na kuwasikiliza walimu wao na kufuata taratibu za shule kumepelekea wao kutumia muda mwingi katika masomo. 
 
Mwalimu Dononda amesema pia nidhamu baina ya wanafunzi wenyewe kwa wenyewe pamoja na kwa walimu wao kumesababisha walimu kuwa na ari ya kuwafundisha na kutumia jitihada za hali ya juu kwa wanafunzi hao ili waweze kufaulu vizuri jambo ambalo limefanikiwa. 
 
"Unajua kila mzazi anamleta mtoto wake shule ili afaulu, sasa ukiwakuta wanafunzi wana ari kwa kweli hata mwalimu unapata moyo wa kufundisha kwa bidii, wanafunzi hawa waliofaulu walikuwa wamechujwa ipasavyo toka wakiwa o'level (kidato cha i-iv) kutoka kwenye shule walizosoma, hivyo kila mmoja alikuwa na moyo wa kuhakikisha anafaulu, na pia wenyewe walikuwa na mshikamano pia" amesema mwalimu huyo. 
 
Ameongeza kuwa katika mtihani wa utamirifu (mock) ambao ulifanywa na wanafunzi 39 pia ulionesha dalili njema za matokeo ya mwisho kuwa mazuri kwa sababu wanafunzi 29 walipata daraja la I, 9 wakapata daraja la II, na mmoja alipata daraja la III.
 
Kwa upande wake mwalimu Jitahidi Sanga ambaye alikuwa akifundisha masomo ya Jiografia na General Studies kwa wanafunzi hao na pia mwalimu wa darasa, amesema siri ya wanafunzi hao kufaulu vizuri ni pamoja na walimu kufundisha kwa muda wa ziada na wikiendi bila malipo yeyote. 
 
Amesema utayari waliokuwa nao wanafunzi hao ulipelekea kufundishwa muda wa ziada bila kusukumwa. 
 
"Kwa mfano likizo ya mwezi Juni mwaka jana wanafunzi hao wengi wao hawakwenda likizo, na mimi mwenyewe nilikuwa nikiwafundisha kwa muda wa ziada bila kudai malipo yeyote, na pia kwa kuwa nilikuwa mwalimu wa darasa nilikuwa nikiwasihi wazingatie masomo pamoja na yale waliyoaswa na wazazi wao" amesema mwalimu Sanga.
 
Bi Anita Sanga ni mzazi ambaye amezungumza na mwandishi wetu na kusema kuwa matokeo hayo wameyapokea kwa furaha na hawakutegemea kama shule hiyo ingefanya vizuri kwa kiasi hicho. 
 
Amesema wanafunzi wote wazingatie masomo kama walivyofanya hao waliomaliza kidato cha sita ili shule hiyo iendelee kufanya vizuri na hatimaye iwe ya kwanza kitaifa kwa kidato cha nne na cha sita. 
 
Shule ya sekondari Iwawa ni miongoni mwa shule tatu za serikali zenye kidato cha tano na sita wilayani hapo.

Na Edwin Moshi

TANZANIA INAVYOSHINDWA KATIKA KISWAHILI KIMATAIFA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
 
Wako waandishi na watafiti ambao ni wageni na hupenda zaidi kujifunza Kiswahili. Ukiwauliza kwa nini wanapenda Kiswahili, wanajibu kuwa ni lugha ya pekee isiyobanwa na dhana za kikabila na kieneo, inavuka mipaka ya nchi na kuwa ni ya kimataifa.
Mgeni mmojawapo ni Pete Muhunzi (jina la kupanga) ambaye ni Mmarekani mwenye asili ya Afrika. Ni Profesa mstaafu wa historia na anafanya utafiti wa masuala ya lugha katika jamii na hasa Kiswahili.
Alifafanua kuwa sababu ya kutambuliwa kwa Kiswahili kuwa ni lugha ya kazi katika vikao vya Umoja wa Nchi za Afrika (AU) ni hatua muhimu katika historia ya lugha hiyo. Uamuzi uliotolewa wa kukifanya Kiswahili kuwa ni lugha ya kazi, uliotokana na kukosekana kwa lugha nyingine za Kiafrika zinazokidhi viwango vya kimataifa.
Kwa mfano, lugha kama Kiigbo, Kiyoruba na Kihausa zote zikiwa ni za Afrika Magharibi na zinavuka mipaka ya nchi. Umoja wa Nchi huru za Afrika (OAU) uliamua kuteua moja ya lugha za Kiafrika na kupendelea kukiteua Kiswahili.
Hatua ya kukiteua Kiswahili ilitokana na uamuzi uliofanyika katika kikao cha Mawaziri wa Utamaduni wa Umoja wa Nchi Huru za Afrka nchini Mauritius mwaka 1988. Mawaziri wa Utamaduni waliibua wazo la kupata lugha moja ya Kiafrika itakayotumika pamoja na lugha za kazi, ambazo ni za kikoloni yaani Kiingereza, Kifaransa, Kireno na Kiarabu. Pendekezo la mawaziri wa utamaduni la kutumia Kiswahili kuwa ni lugha ya Kiafrika na ya tano katika vikao vya OAU ni uamuzi wa kipekee.
Pendekezo hilo liliwasilishwa katika kikao cha Wakuu wa Nchi na Serikali za Afrika huko Addis Ababa na lilikubaliwa.
Kwa kuwa Tanzania ni kitovu cha lugha ya Kiswahili na kina vyombo kadhaa vya kukikuza na kukiendeleza katika ngazi mbalimbali za jamii ikiwamo katika shughuli za Serikali, shuleni na vyuoni, iliteuliwa kusimamia na kutekeleza suala hili.
Hatua ya kwanza ni kuwatambua wafanyakazi waliohitimu chuo kikuu wenye digrii ya kwanza na waliosomea lugha ya Kifaransa.
Kwa maana hiyo, waliochaguliwa walikuwa wakifahamu Kifaransa, Kiingereza na Kiswahili, lugha zilizokuwa zikitumika katika vikao vya OAU. Ilibidi kuwaandaa wataalamu katika fani za wakalimali na wafasiri ili waende kupata taaluma ya juu ya ukalimani na tafsri, ili watakaporejea kutoka masomoni wapelekwe Addis Ababa kutekeleza majukumu yao kwenye shughuli za kazi.
Je, hali ilikuwaje baadaye. Hapo awali ilibidi waandaliwe vijana waliosomea lugha katika ngazi ya shahada ya kwanza ili kupelekwa kujiendeleza katika taaluma hizi. Serikali ya Ufaransa ilikubali kugharimia mafunzo ya vijana hawa kwa safari na mafunzo. Kwa bahati nzuri waliteuliwa vijana wanne kwenda kusoma Ufaransa kwa mwaka mmoja. Baada ya kurejea nchini waliripoti Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Jambo la kushangaza ni kuwa wizara husika haikuwajali, hivyo wakaanza kujitafutia kazi wao wenyewe katika nchi za nje. Mmoja alikwenda Burundi katika Umoja wa Nchi za Maziwa Makuu, mwingine alikwenda Ivory Coast katika Shirika la Uchumi la ECOWAS, Afrika Magharibi.
Tanzania imekosa nafasi ya kuwapatia vijana wake ajira ya uhakika. Hivi sasa huduma za ukalimani na tafsiri zinafanyika kwa mtindo wa kazi za muda (part time), badala ya kuwapo kwa wafanyakazi wa kudumu
Sasa, ipo haja kwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa pamoja na Wizara ya Utamaduni, Vijana na Michezo kuwa na makubaliano ya kulikabili suala hili kwa pamoja na kurejesha nchi katika hadhi iliyopewa huko awali.
Kutokana na Tanzania kushindwa kutekeleza mapendekezo ya OAU, tutajilaumu wenyewe. Hii siyo mara ya kwanza kwa Tanzania kushindwa kutekeleza majukumu yake ya kimataifa kuhusu lugha ya Kiswahili. Soma makala yajayo..
 Chanzo:Mwananchi

CHADEMA WAMBWAGA MBUNGE CCM

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Mbunge wa Njombe Kaskazini, Deo SangaMAHAKAMA ya Wilaya ya Njombe imetupia mbali kesi iliyokuwa ikiwakabili viongozi wa CHADEMA mkoani hapa, ya kutishia kummwagia tindikali Mbunge wa Njombe Kaskazini, Deo Sanga (CCM) maarufu kama Jah People.
Sanga ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Njombe, alidai kukumbana na tishio hilo wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Njombe mjini.
Akizungumza na waandishi wa habari juzi, mwanasheria wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), John Malya, alisema kesi hiyo iliyokuwa chini ya Hakimu Augustino Rwizele, ilitupiliwa mbali kwa kutumia kifungu cha 91 cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai.
Alisema kuwa shitaka la kwanza lililokuwa likiwakabili viongozi hao ni lile lililotokea Februari 3, mwaka huu, ambapo washitakiwa Ali Mhagama, Robert Shejamabu na Award Kalonga walidaiwa kuvamia kikao cha CCM na kutishia kummwagia tindikali mbunge huyo.
Shitaka la pili lilimhusu Emmanuel Mwasongwe ambaye ni msaidizi wa Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, la kutoa lugha ya matusi dhidi ya Jeshi la Polisi mkoani Njombe.
Baada ya hukumu hiyo kutolewa, viongozi wa CHADEMA waliviomba vyombo vya dola pamoja na mahakama kuendelea kufanya kazi kwa kufuata maadili ya kazi zao ili kila mwananchi apate haki yake.
Katibu wa CHADEMA Kata ya Njombe Mjini, Ali Mhagama aliwataka wananchi kuwa makini katika chaguzi mbalimbali zijazo kwa kuchagua viongozi ambao watajali maslahi ya umma.
“Tunamshukuru Mungu kwa kushinda kesi hii, na endapo tungepatikana na hatia leo hii, bila shaka kungekuwa na pengo kubwa katika utendaji wa kazi za chama,” alisema Mhagama.
Kalonga, alisema pamoja na kupigwa katika tukio hilo kiasi cha kuvunjwa taya, alishangaa kupelekwa polisi na kufunguliwa mashitaka huku akiwa ana maumivu makali.
“Siku hiyo nilivunjwa taya, baada ya hapo tulikimbia na kujifungia, lakini jambo la kushangaza ni kwamba tulipelekwa polisi na wakatufungulia mashitaka,” alisema Kalonga.
Akizungumza mara baada ya hukumu hiyo, Katibu wa CCM Wilaya ya Njombe, Clemence Mponzi, alikiri kuwa chama chake kilishindwa kwenda kutoa ushahidi na hivyo kuifanya mahakama itoe uamuzi wake.
Katika uchaguzi huo mdogo uliofanyika Februari 9, mwaka huu, CHADEMA ilishinda kupitia mgombea wake Joseph Mtambo, akichukua nafasi iliyoachwa wazi na marehemu Lupyana Fute
Chanzo:Tanzania Daima 

RC AHIMIZA UWEKEZAJI CHUMBA CHA MAITI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
MKUU wa Mkoa (RC) wa Njombe, Kapteni Mstaafu, Assery Msangi, amekaribisha watu binafsi, mashirika na taasisi yoyote kujitokeza kusaidia ujenzi wa chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Mkoa ya Kibena kutokana na kilichopo kuwa katika hali mbaya hivi sasa.
Kapteni Msangi, aliyasema hayo wakati akikabidhiwa msaada wa taa maalumu mbili za kufanyia upasuaji kwenye chumba cha upasuaji cha hospitali hiyo iliyopo mjini hapa, uliotolewa na Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF), wenye thamani sh milioni 9.
Msangi, alitoa rai kwa yeyote ambaye atakuwa tayari kufanya kazi ya kuwekeza kwenye chumba cha maiti, hatakuwa na kipangamizi.
Aliipongeza NSSF kwa msaada huo, lakini akatoa rai kwa shirika hilo, taasisi na watu binafsi, kufikiria namna ya kuweza kusaidia kujenga chumba cha maiti kwenye hospitali hiyo ya Kibena.
“Kwa niaba ya wananchi wangu na viongozi wa Mkoa wa Njombe, napenda kuwashukuru NSSF kwa msaada huo, lakini tunalo tatizo kubwa hivi sasa la mochwari, na mochwari hivi sasa hazijengwi na serikali, bali zinajengwa na mtu binafsi, taasisi na shirika lolote,” alisema Msangi.
Alisema endapo watajitokeza kuwekeza kwa kujenga chumba cha kuhifadhia maiti, kutasaidia kupata faida ya haraka na yenye manufaa.
“Mochwari na mila zetu ni mahali nyeti sana, lakini nataka niseme kwamba hili Katibu Tawala mliangalie, kwani zinajengwa na watu binafsi au taasisi, kwa sababu ukiweka maiti nane au kumi, maana yake utakuwa unamdai maiti hela kwa kila siku, ni biashara nzuri tu,” alisema Msangi.
Alitoa mfano kwa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Yusuph Makamba, aliporuhusu biashara ya majeneza wengi waliona kama ni biashara ya ajabu, lakini hivi sasa imekuwa ni muhimu na isiyokuwa na shaka kwa jamii.
“Wapo walimfuata Makamba na kumwambia sasa mkuu hii si balaa, majeneza yanauzwa barabarani kama mashati, akawaambia muda wake ukifika mtaona umuhimu wake, ukienda hospitali ya KCMC pale, ile wamejenga wenyewe, lakini ile wameibinafsisha, kuna mtu anafanya shughuli pale, ukilaza maiti unalipia sh 5,000 au 10,000 kwa ‘night’, hivyo nataka nitoe wito kwa mashirika na watu binafsi wajitokeze kujenga.
“Ni biashara ambayo haina ubishi wala mapatano, kwa kawaida mfiwa hana mapatano au nipunguzie, huwa hamna mapatano ya kupunguziana bei, ni eneo ambalo ni zuri la biashara, hivyo watu wajitokeze kujenga, Watanzania wenye moyo na kuguswa na tatizo hili, wajitokeze kujenga hospitali yetu.”
Meneja wa NSSF Mkoa wa Njombe, Godwin Mwakalukwa, alisema shirika lao limetoa msaada huo, baada ya kuguswa na tatizo la ukosefu wa taa maalumu ya kufanyia upasuaji kwenye chumba hicho
 Chanzo:Tanzania Daima

WAKULI MAMBOGA ZA MAJANI WAHIMIZWA KUTUMIA MBOLEA ASILI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Christopher Chiza,
 
Wakulima wa mboga za majani wamehimizwa kutumia mbolea za asili, ambazo mbali na kutumika kama kitoweo, pia hutibu na kukinga maradhi mbalimbali.
Mtakwimu wa Masuala ya Kilimo wa Taasisi ya Wanawake Wajasiriamali (Resewo), Joyce Urassa, alisema miongoni mwa changamoto kubwa kwa wakulima wa mboga na matunda ni jinsi ya kukabiliana na wadudu waharibifu.

Alisema hayo katika semina ya uchambuzi wa ripoti juu ya sera za kilimo barani Afrika na madhara yake kwa wanawake vijijini hivi karibuni na kuongeza kuwa mmea wa alovera, majivu na majani ya mwarobaini vikichanganywa pamoja ni dawa pekee yenye uwezo wa kuua wadudu wa aina yoyote katika mimea.

Afisa Biashara Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Ernest Elias, alishauri wakulima kufuata kanuni za ukulima bora kwa kutumia mbolea asili na kuongeza mbali na kuzipatia bidhaa za Tanzania masoko ndani na nje ya nchi, pia watajikwamua kimaisha.

Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake Viongozi katika Kilimo na Mazingira (Tawlae), Dk. Sophia Mlote, alisema: “Serikali itilie mkazo katika kukuza na kuendeleza maarifa ya kilimo cha jadi, hasa katika kumuwezesha mwanawake kuzalisha na kusindika chakula.”
SOURCE: NIPASHE

WAZIRI WA MAZINGIRA DKT. BINILITH MAHENGE AKANUSHA KUTUMIA FACEBOOK YENYE JINA LAKE



Waziri wa nchi ofisi ya Makamu wa rais Mazingira Dkt Binilith Mahenge amewataka wananchi kupuuza taarifa zozote zinazotolewa kwa jina lake kupitia mtandao wa facebook kwa kuwa yeye hatumii mtandao huo. 

Waziri Mahenge ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Makete mkoani Njombe ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na mwandishi wetu wilayani hapo na kusema kumekuwa na baadhi ya watu wanaoitumia mitandao hiyo vibaya kwa kufungua akaunti yenye jina lake ilihali yeye hajawahi kujiunga na facebook na hana mpango huo. 

Amesema kwa kuwa yeye ni kiongozi mkubwa wa serikali wapo watu wanaoziamini taarifa mbalimbali zinazotolewa kupitia mtandao huo wakidhani zimetolewa na yeye lakini imekuwa tofauti na kuwataka wananchi kuzipuuza taarifa hizo kwa kuwa zinatolewa na mtu ama watu fulani na si yeye.

 "Ukiangalia pale pana picha yangu kweli, lakini taarifa zingine ni uongo mtupu, kwa mfano tarehe yangu ya kuzaliwa iliyoandikwa hapo sia ya kweli, hii inaashiria wanavyoviweka ni vya uongo" amesema Waziri Mahenge.

 Aidha ametoa rai watu kuitumia vizuri mitandao hiyo kwa kuisaidia jamii huku akiwataka waliofungua akaunti hiyo kuifunga na kuacha kuwapotosha watu kwa kutumia jina lake kwani ni kinyume cha sheria na atakayebainika sheria iko wazi dhidi yake. 

Hivi karibuni kumekuwa na watu fulani kufungua akaunti kwnye mitandao ya kijamii kwa kutumia majina ya viongozi mbalimbali kwa lengo la kuwahadaa watu na kuwapa taarigfa ambazo si sahihi

Habari/Picha Na Edwin Moshi, Makete

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

MTOTO AFARIKI BAADA YA NYUMBA KUTEKETEA KWA MOTO,POLISI AMRAGHAI MWANAFUNZI ALIYE ACHIWA NYUMBA NA KULALANAE KWAKE.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Wananchi wa Mlangali  Ludewa  wakiwa  wamekizingira  kituo cha polisi Mlangali  mara baada ya  kuipeleka maiti ya mtoto aliyeteketea kwa  moto katika  kituo hicho
Wananchi  Mlangali  Ludewa  wakiwa  wamekizingira kituoa  cha polisi cha Mlangali jana
Kitanda ambacho mtoto  huyo alikuwa amelala
Dirisha  likiwa limevunjwa ili  kuutoa mwili wamtoto aliyeungua kwa moto
Wananchi  wakitazama chumba  alichokuwa amelala mtoto  huyo aliyeteketea kwa  moto
 Nyumba  ya askari  iliyodaiwa  kutumika  kufanya mapenzi na mwanafunzi huyo kabla ya mtoto kutetekea kwa  moto
.................................................................................................................
KIONGOZI  wa  mbio  za mwenge  Kitaifa awatuliza wananchi wa Mlangali wilaya ya Ludewa ambao baadhi yao  waliandamana kituo cha polisi kushinikiza kutolewa kwa askari polisi aliyedaiwa kusababisha kifo cha mtoto ili auwawe .
 kiongozi  huyo aliwaomba  wananchi wa Mlangali kutokubali  kujihusisha na vitendo  vya uvunjifu wa amani ikiwa ni pamoja na kuepuka  kujichukulia  sheria mkononi  kutokana na  wananchi  zaidi ya 200 jana kuvamia kituo cha polisi Mlangali na kuacha  kushiriki mbio za mwenge kutokana na mmoja kati ya askari kudaiwa kusababisha mauwaji ya mtoto wa miaka 2.
Mbali ya kiongozi  huyo kuwaomba wananchi  kutofanya  vurugu hizo na kutaka  kuacha  vyombo vya usalama kulifanyia kazi bado wananchi hao  waliendelea  kukizunguka kituo  hicho cha polisi hadi majira ya mchana huku mwili  wa  mtoto  huyo ukiwa  umepelekwa kituoni  hapo baada ya  kuungua vibaya kwa  moto.
Wananchi  hao  walifikia  hatua  hiyo ya kuzingira kituo  cha  polisi kutokana na kifo cha mtoto Angela Mtitu kufariki dunia  kwa moto wakati  askari polisi aliyetambuliika kwa jina moja la  kabasa  kudaiwa  kumrubuni mwanafunzi  wa kidato cha tatu katika shule  moja ya  sekondari wilayani Ludewa ambae  ndie  alikuwa akimlea mtoto huyo na kwenda  kufanya nae mapenzi nyumba ya pili ambako ni nyumbani kwa askari  huyo na kupelekea  mtoto huyo kuungua moto.
Hivyo  wananchi hao  wenye hasira kali  walilazimika  kukizingira  kituo  hicho kwa  zaidi ya masaa matano kabla ya askari wa FFU kutoka mkoani Njombe  kufika eneo hilo na kuwatawanya kwa  mabomu ya machozi huku mwili wa mtoto huyo ukiwa ndani ya kituo cha polisi pamoja na askari  huyo na binti huyo mwanafunzi ambao walikuwa  wakishikiliwa na jeshi la polisi.
Kamanda  wa  polisi  wa mkoa wa Njombe hakuweza kupatikana kuzungumzia undani wa  tukio hilo japo baadhi ya askari  waliokuwepo  eneo la tukio  walidai kuwa  tukio hilo lilitokea usiku  wa  kuamkia.

Mtandao huu www.jamvilahabari.com ulifanya mawasiliano na baadhi ya wananchi hao walidai kuwa baba wa mtoto huyo alikamatwa na polisi kwa kesi ambayo ambayo haipo wazi lakini wanadai mzazi huyo kuwekwa kizuizini ni mbinu ya askari huyu ili aendelee kujivinjari na mwanafunzi huyu wa Ulayasi sekondari.

Pia katika vurugu hizo inadaiwa askari wa kutuliza ghasia walitumia mwanya wa vurugu hizo kupora mali katika baadhi ya sehemu za biashara. 

Wananchi hao wamesema walikwenda polisi kuripoti kupotelewa kwa mali zao wanadai mkuu wa kituo anasema hawezi kupokea malalamiko yao kwakuwa jambo hili lipo ngazi za juu, kituhicho kimewafanya wanachi hao washindwa kuelewa wapi ni sehemu sahihi yakupeleka malalamiko yao
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa