Home » » ASKARI MBARONI KWA KUTOROKA LINDO NA KUSABABISHA WIZI NYUMBANI KWA RC

ASKARI MBARONI KWA KUTOROKA LINDO NA KUSABABISHA WIZI NYUMBANI KWA RC


Mwandishi wetu, Njombe Yetu

Jeshi la polisi Mkoani Njombe linawashikilia askari wawili waliokuwa lindo nyumbani kwa mkuu wa mkoa baada ya kutokea wizi usiku wa kuamkia siku ya sensa ambapo watu wasiofahamika waliingia nyumbani hapo na kuiba kompyuta mpakato moja,simu 3 mbili zikiwa nia aina ya Nokia ambazo ni mali ya watoto wa mkuu huyo wa mkoa.

Kamanda wa polisi kamishna msaidizi wa polisi Bw.Fulgence Ngonyani amesema, tukio hilo lilitokea wakati nyumbani hapo wakiwepo walinzi ambao ni askari polisi na kwamba kutokana na tukio hilo askari aliowataja kuwa ni mwenye namba G15414 PC Ombeni na wengine ni mwenye namba G 5455 PC Mohamed wanahojiwa kuhusiana na tukio hilo.

kutokana na tukio hilo mkuu wa mkoa alisema kumekuwepo uzembe kwa askari polis wanaokuwepo Lindoni hapo kwani mara nyingi wamekuwa wakiacha lindo na kwenda kusikojulikana na kurudi wakiwa wamelewa, na kwamba kuna wakati wamekuwa wakitumia uda mwingi kulala na kuacha lindo.

Akizungumzia suala hilo Mkuu wa Mkoa wa Njombe Kapteni mstaafu Aseri Msangi ametoa duku duku lake ama kero kuhusu askari hao kwamba tabia ya askari hiyo, ameiona si mara moja huondoka na kuacha lindo.

Amesema kuwa kuna siku alimkuta askari akiwa amelala ndani ya moja ya magari kati ya yaliyopo nyumbani hapo na kumwamsha akiwa fofo.

Blogzamikoa

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa