Home » » RC NJOMBE AAGIZA KUFUKUZWA KAZI WATENDAJI WAZEMBE LUDEWA

RC NJOMBE AAGIZA KUFUKUZWA KAZI WATENDAJI WAZEMBE LUDEWA

Mkuu wa mkoa wa Njombe Kapten Aseri Msangi, akiapa mbele ya Raisi Kikwete.
Nickson Mahundi, Ludewa
Mkuu wa mkoa wa Njombe Kapten Aseri Msangi aliuagiza uongozi Halmashauri ya wilaya ya Ludewa kuwachukulia hatua za kisheria wafanyakazi wazembe ndani ya wilaya hiyo kutokana na kusababisha hati chafu ya hesabu za Serikali.
Kauli hiyo ilitilewa jana katika ziara yake wilayani Ludewa kutokana na ripoti chafu iliyotolewa  Mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za Serikali(CAG) kwa wilaya hiyo kutokana na uzembe wa baadhi ya wafanyakazi uliopelekea upatikanaji wa hati hiyo.

Kapten Msangi alisema asingependa wilaya za mkoa wake kupata hati chafu kwa uzembe wa baadhi ya wafanyakazi.
“Sijapenda na sitopenda ndani ya Mkoa wa Njombe kuwepo kwa uzembe wa namna hiyo kwani nitaonekana sifanyi kazi hivyo ninachohitaji ni kuanza na hawa wazembe waliopelekea upatikanaji wa hati chafu kuchukuliwa hatua za kisheria ili iwe fundisho kwa wilaya nyingine” alisema Kapten Msangi.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauli hiyo Mathei Kongo alikiri kuwepo kwa uzembe huo miongoni mwa wafanyakazi na kuahidi kulifanyia kazi suala hilo ili lisijirudie katika wilaya ya Ludewa.
Kongo alisema kumekuwepo kwa ukiukwaji wa malipo na ukusanyaji wa fedha za Halmashauri katika miradi na vyanzo nya mapato katika maeneo mbalimbali hiyo ni sababu kubwa ya upatikanaji wa hati chafu.
Hivi karibuni ofisi ya mkaguzi mkuu na mdhibiti wa hesabu za Serikali (CAG) ilitoa hati chafu kwa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa kwa kushindwa kufikia malengo katika manunuzi na ukusanyaji wa fedha mbalimbali.
Katika hatua nyingine Kapten Msangi aliwataka Madiwani na viongozi mbalimbali kuhimiza kilimo cha Kahawa, Mahindi na ufugaji Kuku na Nyuki kwaajili ya asali ambapo itakuwa ni ukombozi kwa wananchi wa wilaya ya Ludewa.
Alisema watanzania wamekuwa wakiilalamikia Serikali kuwa maisha yamekuwa magumu bila kujua kuna fursa nyingi zikiwemo za ufugaji wa nyuki na kilimo ambazo zinaweza kumfanya kila mwananchi kuishi maisha bora.
Alisema vijana wamekuwa wakikaa bila kufanya kazi wakisubiri maisha bora na kuhamahama vyama ili kupata maisha bora hilo sio suruhisho la maisha bora bali maisha bora yanamtaka kila mmoja kufanya kazi kwa bidii.
Kuhusu pembejeo za kilimo Kept Msangi alisema kumekuwa na wizi mkubwa kwa wazabuni wasio waaminifu hivyo Serikali inaandaa utaratibu wa kuzipitisha Pembejeo hizo katika vyama vya msingi, Saccos na Vikoba ili kuondoa uchakachuaji.
Nae Mkuu wa wilaya ya Ludewa Juma Madaha alikili kuwepo kwa uchakachuaji wa pembejeo za kilimo kwa baadhi ya wazabuni na watendaji wa kata na vijiji wasio waadirifu hivyo hatua za kisheria zinafuata dhidi yao.
Kapten.Msangi aliwataka viongozi wa wilaya hiyo kuhimiza kilimo kwa haitakubarika kuwaruhusu wawekezaji wa kichina kufanya shuguri za kilimo katika wilaya hiyo ili kuwawezesha wakulima kujiinua kiuchumi.
Blogzamikoa

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa