Home » » WANANCHI NJOMBE WAITAKA CCM KUTEKELEZA AHADI ZAKE.

WANANCHI NJOMBE WAITAKA CCM KUTEKELEZA AHADI ZAKE.


Mwandishi wetu, Njombe

WANANCHI wa Kata ya Kitandililo halmashauri ya Mji wa
Makambako Mkoani Njombe, Wameutaka uongozi wa Chama cha
Mapinduzi kutekeleza ahadi ambazo waliahidi ili kuondoa kero 
ambazo wanakabiriwa nazo.

Wakizungumza katika mkutano uliofanyika katika kata hiyo,
wananchi hao wamlalamikia huduma ambazo hazikidhi mahitaji yao 
ambapo wazee, watoto na wanawake wajawazito wamekuwa akilipia 
huduma za afya, pamoja na kukosekana kwa pembejeo kwa wakati 
katika msimu wa kilimo.

Upande wake m/kiti CCM wa Wilaya hiyo, Adamu Msigwa 
amewataka viongozi wa vijiji na kata kuhakikisha wanashiriki 
katika kusimamia shughuli za maendeleo.

Viongozi wa ccm Wilaya ya Njombe walifanya ziara ya kukagua 
miradi ya maendeleo katika Vijiji na kata za Kitandililo na Mahongole kama kutekeleza ilani ya ccm kuhakiki na kutathimini 
fedha za wananchi na halmashauri ikiwa zinatumika ipasavyo.

Blogzamikoa

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa