HII NAYO NOMA: KIJANA AFARIKI DUNIA BAADA YA KUFANYA MAPENZI NA NGURUWE WILAYANI LUDEWA, SOMA HAPA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Kijana mmoja aitwaye Simon Dustan Mwanjavala maarufu kama Mwachakala (15) mkazi wa kijiji cha Mbwila kata ya Luana wilaya ya Ludewa mkoani Njombe amefariki dunia muda mchache baada ya kukutwa akifanya mapenzi na Nguruwe.

Tukio hilo la kustaajabisha limetokea leo wilayani Ludewa baada ya kijana huyo "kufumaniwa" akifanya mapenzi na mnyama huyo, ndipo walipomkamata na kumfunga kamba mikono yake na miguu ili asikimbie.

Baada ya majirani kumuona kijana huyo akimbaka nguruwe huyo kwenye banda la mnyama huyo walikwenda kumwambia baba yake mdogo ambao kwa pamoja walimkamata kijana huyo, ambaye alikiri kufanya kosa hilo.
Alipoulizwa sababu zilizomfanya kufanya mapenzi na nguruwe, alisema alikuwa na hamu ya kufanya tendo hilo.

Kutokana na kitendo hicho waliamua kumvua nguo zote na kumfunga kamba na kumpa kichapo  kisha wakamuacha kwa muda kwenye eneo la tukio, na walipokuja kumfungua kamba na mwenyekiti wa kijiji hicho, alidondoka na kufariki dunia papo hapo.
Chanzo Kijukuu cha Bibi K blog

PHILIP FILIKUNJOMBE AOMBEWA USHINDI KURA ZA MAONI UBUNGE LUDEWA‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 
Na Matukiodaima Blog , Ludewa
WAKATI wanachama wa  chama  cha mapinduzi (CCM)  jimbo la  Ludewa mkoani  Njombe  kesho jumanne wanapiga kura za maoni  ili  kumpata mgombea wa  ubunge atakayezipa pengo  lililoachwa  wazi na aliyekuwa mbunge wa  jimbo  hilo kwa  kipindi  cha miaka  mitano iliyopita na na mgombea  ubunge marehemu Deo Filikunjombe  ,wananchi wa  jimbo  hilo wameomba wajumbe wa CCM kurudisha  jina la mdogo wa marehemu Bw Philip Filikunjombe ili akawatumikie bungeni.

Wakati  mchungaji  wa kanisa la kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKT) usharika  wa  Ludewa mjini mchungaji Tafuteni Mwasonya akidai  kuwa tayari Mungu amekwisha wapatia  wananchi  wa Ludewa mbunge hivyo wagonje taratibu  za  kidunia  zifanyike.

Kwani  alisema anaetoa   uongozi ni  Mungu na  kikubwa kwa  wananchi wa Ludewa wanapaswa kuomba kwa Mungu badala  ya kusikiliza  wanadamu na  kuongeza  kuwa wanaemtaka ni yule ambae anaijua  Ludewa  vizuri na mwenye  kuwaletea maendeleo .

Wakizungumza na mtandao  wa  www.matukiodaima.co.tz  kwa  nyakati  tofauti    wananchi hao   walisema  kuwa imani na matumaini  yao ni  kuona  wajumbe wa mkutano wa CCM wanamchagua  Philip Filikunjombe kuendeleza  mipango  mbali mbali ya kimaendeleo iliyoachwa na marehemu Filikunjombe.

Kwani  wamesema  kuwa Philip ambae  alikuwa ni msaidizi  na mratibu  wa mipango  ya  jimbo  hilo wakati  wa uhai  wa kakake Filikunjombe  wanaimani  kuwa ataweza kuwatumikia  vema kama  ilivyokuwa kwa kaka  yake hivyo ili  kuweza kuwafuta machozi  yao  juu ya maendeleo ya jimbo  hilo wanaomba  jina la Philip  kuweza kuchaguliwa .

John Haule  mkazi  wa Mavanga akiungumza kwa niaba ya wananchi wenzake  alisema  kuwa ni  wagombea   zaidi ya  watano  wamejitokeza  ila kwa wote  hao  bado  wao kama  wananchi  wa jimbo  hilo ambae wanaona anaweza  kuwatumikia ni Filikunjombe .

" Tunaomba  sana kama  ingekuwa ni  wananchi  tunaamua  ni nani awe mbunge  wetu  basi tusingehitaji kupiga kura   za maoni kwa  kauli  moja tungempa Philip Filikunjombe .....ila kwa  kuwa ni taratibu  ndani ya  CCM na sehemu ya  Demkrasia basi tunalazimika  kuzama  katika maombi  kuona azma yetu  inatimia kwa  kumpata  yule  tulie mtegemea  baada ya kifo  cha  kipenzi  chetu Deo"
Jumla ya  makada  10 wa CCM waliochukua na kurejesha fomu na wanataraji  kuchujwa  katika mchakato   huo  wa ndani ya CCM ili  kumpata  mmoja atakapambana na  mgombea wa Chadema mbali ya Philip Filikunjombe wengione ni   Edgar Lugome.Johnson Mgimba,Emmauel Mgaya, James Mgaya,  Jackob Mpangala, Saimon Ngatunga, Evaristo Mtitu, , Deo Ngalawa na Zephania Chaula,

Kwa upande  wake Bw  Philip  akielezea vipaumbele  vyake  iwapo  atachaguliwa katika  mchakato  huo wa  kura za maoni ndani ya chama  na wananchi  kumchagua  kuwa mbunge wao  kwanza ni  kuendelea mipango yote  iliyoachwa na marehemu ambayo mipango  mingi anaitambua  na  kuwa suala la nidhamu na uwajibikaji  katika kazi kwake  litakuwa ni msingi  wa  kweli  wa kuwaletea wana Ludewa maendeleo .

Alisema Ludewa mbali ya kumpoteza mbunge  wao bado wanayonafasi ya kuamua  na  kumchagua  ili  kuendeleza yote mazuri  kwa ajili ya maendeleo yao  na  kuona kasi ya maendeleo katika wilaya   hiyo inaendelea  kukua kwa kasi na kuwaomba  wana CCM kumwamini kwani hata waangusha na kuwa anachoomba wana CCM kumkopesha  kura  zao za ndio ili  ndani ya  miaka mitano awe  kuwalipa maendeleo .
ELIMU
wakili wa mahakama kuu, mtafiti shahada uzamivu, katika sharia (PHD) Chuo Kikuu huria cha Tanzania , Shahada ya uzamili katika sharia (LLM), Chuo kikuu cha Stratchclyde, Uingereza,  Diploma ya juu ya Mafunzo ya sheria kwa vitendo, Chuo cha Mafunzo ya Uwakili Tanzania, Dar es Salaam 2012, Stashada ya sheria (LLB), 2007 Chcha Tumaini Iringa, Cheti cha Lugha ya Kifaransa. Chuo kikuu cha Blida, Algeria 2004, Cheti cha Uandishi wa Habari, Dar es Salaam School of Journalism 2003.

Elimu ya kidato cha sita, shule ya sekondari Mzumbe 2002, Elimu ya Sekondari, Njombe Sekondari 1999, Elimu ya Msingi, Shule ya msingi Ludewa mjini 1995.

UZOEFU WA KAZI.
mwanasheria mwandamizi, Mamlaka ya ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) 2012 mpaka sasa, Mkufunzi wa sheriaKikuu Huria cha Tanzania, 2010-2012, Mkufunzi wa Sheria, Chuo kikuu cha Matakatifu Augustino 2010-2912, Mkufunzi wa Sheria Chuo kikuu  Tumaini Iringa 2007-2010.

UJASILIAMALI NA BIASHARA BINAFSI.
Mkurugenzi na mmiliki wa Kampuni ya uwakili wa Reliance Legal Consultants, Dar es Salaam, Mkurugeni mmiliki wa kampuni ya usafiri ya Matatu Logistics, Dar es Salaam na Mkurugenzi na mdau wa Kampuni ya Jumbo Camera House, Dar es Salaam.


  Deo  Filikunjombe pamoja na watu  wengine watatu alifariki kwa ajali  ya  Chopa katika  hifadhi  ya Selou akitokea  jijini Dar es Salaam  kuelekea jimboni Ludewa mnamo Octoba 15  mwaka 2015
 

ERIC SHIGONGO: NENDA KAMANDA WANGU DEO‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

chopa
Aliyekuwa Mbunge wa Ludewa kwa tiketi ya CCM, Deogratias Filikunjombe, enzi za uhai wake akipanda chopa yake.
Nakupenda Deo
Nimesikitishwa sana na kifo chako. Kweli kifo kipo na kila mmoja wetu atakipitia lakini cha aina hii, cha kijana aliyekuwa akipigania watu wake kiasi hiki? Kinaumiza sana, hata hivyo, hatuna budi zaidi ya kukubali kuwa Deo Filikunjombe, jembe la mkono limeondoka.
chopa 2
Chopa iliyosababsha kifo cha Filikunjombe, Capt. William Silaa na watu wengine wawili.
Nasema kutoka ndani ya moyo wangu, taifa limepoteza mtu muhimu sana, hakusita kupigania alichokiamini bila uoga wala hofu! Wakati mwingine alitofautiana na msimamo wa chama chake kwa maslahi ya Watanzania maskini, kwako ukweli ulikuwa nguzo. Nenda Deo, nenda kapumzike muda si mrefu tutaungana nawe, kila mwanadamu atafariki dunia maana ndivyo ilivyoandikwa.
Lakini cha muhimu ni mtu atakuwa anafanya nini wakati anakufa! Je, atakuwa akiiba au akifanya uzinzi? Deo umekufa ukitumikia watu wako, umekufa kifo chema na Wanaludewa watakuombea. Nenda Deo, pumzika Deo, mema yako yamekutangulia.
Hayo ndyo yatakutetea mbele ya Maulana! Mwisho nasema kwa uchungu na ninakuahidi, pale ulipoishia, sisi tutaendelea bila kujali tupata nini mpaka siku moja wananchi wa taifa hili wafaidi mema ya nchi yao.
Nenda Deo, kapumzike kwa amani, umekufa katika mapambano. Natoa pole kwa familia yako, mkeo, watoto, wazazi na wananchi wote wa Jimbo la Ludewa, msiumie sana, Mungu anajua ni kwa nini ameamua jambo hili litokee. Naamini Deo yuko mahali sahihi, kutokana na kile alichokuwa akikifanya wakati anakutwa na mauti, kwetu sisi, kibinadamu ni maumivu lakini kiimani, Deo yuko mahali salama. Nenda kaka Deo. Pumzika kwa amani kaka!
Eric James Shigongo,
Mkurugenzi, Global Publishers Ltd.
Nenda kamanda wangu Deo

MCHUNGAJI MTIKILA AZIKWA ,FILIKUNJOMBE JAJI MUTUNGI WATOA YA MOYONI HELKOPTA YA FILIKUNJOMBE YAWA KIVUTIO‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Mwenyekiti  wa CCM wilaya ya  Ludewa Bw Stanley Kolimba  akiweka shada la maua katika kaburi ya mwenyekiti wa DP mchungaji Mtikila leo
 Viongozi  wa kitaifa wa DP na  mkoa wa Iringa na Njombe wakiwa katika kaburi la Mtikila
 Mmiliki wa mtandao huu wa matukiodaima Bw Francis Godwin  wa pili kushoto akimhoji Live kupitia radio Country Fm naibu katibu mkuu wa DP Taifa Bw Abduli Mluya juu ya kifo cha Mtikila 
Wananchi  wa kijiji cha Milo Ludewa wakitazama Chopa aliyotumia Deo Filikunjombe kufika msibani hapo leo
ACT Wazalendo na DP  waungana katika msiba wa Mtikila
Mwenyekiti wa DP mkoa wa Iringa na mgombea ubunge jimbola Iringa mjini Robart Kisinini kushoto akiungana  kubeba jeneza lenye mwili wa Mtikila
 mkuu  wa mkoa wa Njombe Dr Rehema Nchimbi kulia akiwa na Deo Filikunjombe mgombea  ubunge jimbo la Ludewa na mbunge aliyemaliza muda  wake katikati kushoto ni msajili wa vyama vya siasa nchini Jaji Francis Mutungi leo  wakati wa mazishi ya Mchungaji Mtikila
 Mchungaji Patrick Mgaya aliyekuwa  safari moja na marehemu Mtikila wa pili kulia akiwa katika mazishi hayo
 Waombolezaji wakiwa msibani

 Filikunjombe akitoa salamu zake wakati wa mazishi ya Mtikila
 Wananchi wakimsikiliza Filikunjombe



 Filikunjombea akitoa mkono wa pole  kwa wafiwa  katikaati ni mjane Bi Jojina Mtikila

 Filikunjombe akiwasili msibani kwa chopa

 Jaji Francis Mutungi kushoto Bw MGaya na Askofu Mtetemela na Filikunjombe wakiwa msibani
 Filikunjombe akijiandaa kubeba jeneza

 Mjane  wa Mtikila  akiweka shada la maua

 Na MatukiodaimaBlog
MWENYEKITI wa chama cha DP mchungaji Christopher Mtikila azikwa kijijini kwake Milo Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe vilio vyatawala aliyekuwa mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe na Msajili wa vyama vya siasa nchini Jaji Francis Mutungi  watao ya Moyoni wasema alikuwa kiungo mhimu katika Taifa .

Wakati Msajili wa vyama vya siasa nchini Jaji  Mutungi  akiwataka watanzania hasa viongozi wa vyama vya siasa kumuenzi Mchungaji Mtikila kwa kuenzi Amani wakati huu wa kuelekea katika uchaguzi mkuu octoba 25 mwaka huu ,Filikunjombe asema mbali ya ukorofi wa Mtikila kwa kile alichokiamini ila kwake alikuwa ni mshauri mkubwa wa Ubunge wake katika jimbo la Ludewa.

Wakitoa salamu za rambi rambi wakati wa mazishi hayo yaliyofanyika leo  kijijini kwake Milo Wilaya ya Ludewa ,Jaji Ntungi alisema kuwa katika Enzi zake marehemu Mtikila alikuwa akisimamia kile anachokiamini.

Alisema kuwa mbali ya misimamo yake ya kusimamia alichokiamini bado alikuwa ni mtu wa kujenga hoja na ambae hakupenda kuhatarisha Amani ya nchi hakuwa anapenda njia za mkato katika kupata majibu ya kile asichokiamini.

" Njia za mkato marehemu hakupenda kabisa kwani hata Kama jambo la kutisha ambalo wengine huogopa yeye alikuwa tayari kwenda mahakamani kusaka Haki yake bila kuhatarisha Amani ya nchi Mimi nafikiri kila mmoja akafuata misingi yake katika kudai Haki bila kuvuruga amani naamini tutafanikiwa

" Alisema kuwa kuna mapungufu yanaweza kujitokeza ila Jambo la msingi kila mmoja kutanguliza kwanza amani ya nchi badala kuipa kisogo Amani na kupenda machafuko katika nchi"

Hivyo aliwataka watanzania bila kujali itikadi zao za vyama kuendelea na siasa huku wakitanguliza Amani ya nchi.

Mbunge aliyemaliza muda wake wa jimbo la Ludewa ambae ni mgombea Ubunge wa jimbo hilo Bw Filikunjombe alisema kuwa pamoja na Mchungaji Mtikila enzi za uhai wake alisimamia jambo ambalo
alikuwa akiamini ila kwake amekuwa msaada mkubwa katika ushauri wa kuwatumikia wananchi wa Ludewa .
Alisema Mchungaji Mtikila hakuwa tayari kumuunga mkono mbunge wa Ludewa ambae hakuwa msaada wa kimaendeleo kwa wananchi ila kwa upande wake alikuwa akimuunga mkono na hata kutosimamisha mgombea katika jimbo la Ludewa.

" Mchungaji Mtikila hakuwa tayari kuungana na mbunge asiyefanya Kazi za maendeleo jimboni Ludewa ila kwangu alikuwa akiniunga mkono na hata kunipingeza kwa Kazi nzuri ..... Kicho chake ni pigo kubwa kwa Taifa hasa kwa wana Ludewa ambao tulijivunia sana uwepo wake"

Hata hivyo alisema njia pekee kwake ya kumuenzi Mchungaji Mtikila ni kuendelea kuwatumikia vema wananchi wa Ludewa kwa kuleta maendeleo zaidi Kama alivyohitaji katika uhai wake.

Filikunjombe alisema katika kuamini kwake na kusimamia anachokiamini hadi mauti inamkuta alikuwa akitetea kuwepo kwa nchi ya Tanganyika na ndio maana kazikwa na bendera ya Tanganyika na kudai kuwa hakuna na kosa kupigania Tanganyika kwani Tanganyika inahitajika.

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dr Rerema Nchimbi alisema kuwa Mkoa wa Njombe umepoteza kiongozi makini na kuwa katika kumuenzi ni vema kwa vyama vya siasa kuendesha kampeni za amani na utulivu zaidi na kuwa wakati taifa linaelekea katika uchaguzi mkuu ni vema kila chama kumuenzi Mtikila kwa kulinda Amani .

Naibu Katibu mkuu wa DP Taifa Abdul Mluya alisema kuwa suala la kifo cha mwenyekiti wake ni utata mtupu na bado wanaendelea kuchunguza.

Wakati huo huo Chopa ya Filikunjombe aliyotumia kufaria kwenda katika mazishi hayo iliwafanya wananchi kuacha kusikiliza Salam mbali mbali za viongozi na kukimbilia kutazama na kumlaki Mgombea huyo Ubunge jimbo la Ludewa.

DK MAGUFULI ATOA MPYA TENA AFANYA MAZOEZI YA NGUVU JUKWAANI MAKAMBAKO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli akifanya mazoezi jukwaani akijiandaa kujinadi kwa wananchi katika Mji wa  Makambako, mkoani Njombe leo,  jambo ambalo lilizua vifijo, nderemo na vigelegele kutoka kwa wananchi waliofurika kwenye mkutano huo wa kampeni.PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG


 Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli akijinadi kwa wananchi  kwa kuwaomba ifikapo Oktoba 25, mwaka huu wakati wa Uchaguzi Mkuu, waende wote kumpigia kura za ndiyo ili ashinde kwa kishindo urais.
 Wakazi wa Mwanjelwa, jijini Mbeya, wakimsikiliza Dk Magufuli akijinadi kwao baada ya msafara wake kuzuiwa eneo hilo ukitokea Uwanja wa Ndege wa Songwe ukienda Mbarali kuendelea na kampeni.
 Dk Magufuli akiomba kupigiwa kura na wananchi wa Nswisi wilayani Mbarali huku akirekodiwa na Shaban Kwaka wa TBC.

 Mama mkazi wa Igurusi wilayani Mbarali Mbeya, akifurahi baada ya kumuona Dk Magufuli.PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Dk Magufuli akizungumza na wananchi wa Igurusi waliouzuia msafara wake

 Wananchi wakimshangilia Dk Magufuli alipokuwa akihutubia na kuomba kura kwao katika Mji wa Chimala, Mbarali mkoani Mbeya leo.
 Mfuasi wa CCM, akishangilia huku akiwa na picha ya Dk Magufuli  wakati wa mkutano wa kampeni Rujewa wilayani Mbarali, Mbeya leo.
 Waziri Mkuu mstaafu,  Samuel Malecela akitangaza wasifu wa Dk Magufuli na kwamba niye anayefaa kuchaguliwa kuwa rais tofauti na mgombea wa Ukawa, Edward Lowassa.
 Sehemu ya wananchi wakiwa katika mkutano wa kampeni Rujewa leo
 Wananchi wakimshangilia Dk Magufuli wakati wa mkutano huo na kukubali kumpigia kura za ndiyo
 Dk Magufuli akimnadi mgombea ubunge Jimbo la Mbarali,
 Ni furaha iliyoje kwa wananchi wa Mbarali baada ya kufurahishwa na ahadi mbalimbali za maendeleo alizokuwa akizitoa kwaoPICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Dk Magufuli akimpokea mmoja wa wanachama wa chama cha ACT -Wazalendo aliyeamua kujiunga na CCM wilayani Mbarali
 Dk Magufuli akimnadi Mgombea ubunge jimbo la Wanging'ombe, Gerson Lwenge katika Mji wa Ilembula, mkoani Njombe. Lwenge alikuwa Naibu waziri wa ujenzi wilazara iliyokuwa akiiongoza yeye
 Wananchi wa Ilembula wakimsikiliza Dk Magufuli akijinadi
 Moja ya mabango yalyokuwepo katika mkutano wa kampeni za CCM, mjini Makambako,
 Mgombea ubunge Jimbo la Makambako, Jah People akijinadi kwa wananchi katika mkutano wa kampeni mjini Makambako ambapo pia alimuombea kura Dk Magufuli
 Huree Dk Magufuli
 Jah People akiibusu picha ya Dk Magufuli ikiwa ni ishara ya kumkubali kuwa rais
 Mjumbe wa Kamati ya Kampeni za CCM, Abdallah Bulembo akitangaza wasifu wa Dk Magufuli na kwamba anafaa kuchaguliwa kwa kura nyingi kuwa Rais wa Tanzania mjini Makambako, mkoani Njombe.
 Wananchi wakifurahia hotuba ya Dk Magufuli
 Dk Magufuli akiwa na baadhi ya waliovihama vyao vya upinzani na kuamua kujiunga na CCM wakati wa mkutano mjini Makambako

Dk Magufuli akihutubia katika mkutano wa kampeni mjini Mafinga, wilayani Mufindi
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa