Home » » RC NJOMBE: TUMIENI VYEMA BENKI ZA WANANCHI

RC NJOMBE: TUMIENI VYEMA BENKI ZA WANANCHI




Mwandishi wetu, Njombe


WANANCHI mkoani Njombe, wametakiwa kutumia vema benki ya wananchi (NJOCOBA) ili kujipatia mikopo na kukuza uchumi wao badala ya kutumia taasisi nyingine za kifedha ambazo riba ya mikopo yao ni kubwa na haziwasaidii kujikwamua kiuchumi.

Akiwahatubia wananchi waliohidhuria mkutano huo wa mwaka, mkuu wa mkoa wa Njombe, Aseli Msangi amewataka kuweka akiba na kununua hisa pamoja na kulipa mikopo kwa wakati.


Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi Twilumba Ulaya amesema, ili kuboresha huduma kwa wananchi benki hiyo imelenga kuwafikia wakazi wa wilaya za makete, Ludewa na kuhudumia mkoa mzima badala ya wilaya pekee.

Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo Michael Ngwira ameeleza mafanikio na changamoto zinazoikabili benki hiyo na jinsi ambavyo amejipanga kukabiriana nazo.

Hadi kufikia Desemba mwaka jana benki hiyo imetoa mikopo ilikuwa imetoa mikopo yenye thamani ya sh. bilioni 3.6

urejeshaji wake umekuwa mbaya ambapo hadi wakati huo mikopo yenye thamani ya sh. milioni 267 sawa na silimia 18,
haijarejeshwa. 


Blogzamikoa

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa