Wananchi waomba eneo lao Kupimwa ana kugawiwa viwanja Njombe

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


 Mkuu wa wilaya ya Njombe Ruth Msafuri akizungumza na wananchi wa Mjini Njombe katika mkutano wake wa Hadhara
Baadhi ya wakazi mjini njombe wakisikiliza mkutano wa mkuu wa wilaya ambapo walipata nafasi ya kutoa maoni yao

WANANCHI halmashauri ya Mji wa Njombe wamemuomba mkuu wa wilaya hiyo Ruth Msafiri kuiamuru halmashauri hiyo kuwagawia wananchi viwanja vilivyopimwa ambapo katika halmashauri hiyo tangu mwaka 2012 hakujapimwa tena viwanja.

Wananchi wanatoa kero zao wakati wa mkutano wa kwanza wa mkuu wa wilaya na wananchi ambapo ni kitu cha kwanza kufanyika wilayani hapo.

Nestori Kigae akitoa kero yake kwa mkuu wa Wilaya ya Njombe alisema kuwa halmashauri hiyo haigawi viwanja kwa vijana na kuwa sasa ni muda mrefu viwanja havijagawiwa na kusasabisha wananchi kukosa maeneo ya kujenga.

Alisema kuwa vijana wapo tayari kujenga makazi yao lakini halmashauri hiyo haipimi viwanja na kuvigawa kwa wananchi.
Mkuu wa wilaya alitoa nafasi kwa afisa wa Ardhi kujibu masuala yanayo husu ardhi yaliyo ulizwa na wananchi.

Afisa ardhi Taday Kabonge alisema kuwa halmashauri yake ilipima viwanja mwaka 2012 lakini mpaka sasa haijawahi kupima na kuwa kuna viwanja ambavyo mpaka leo bado vipo havijachukuliwa.

Alisema kuwa viwanja vinavyo gawiwa na halmashauri vinauzwa na havigawiwi bure kwa wananchi na kuwa vinatolewa kwa wananchi wote wa halmashauri hiyo.
Katika hotuba ya mkuu wa wilaya ya Njombe ya lisaa limoja kwa wananchi anasema kuwa serikali itahakikisha kero kwa wananchi zinaondoka na kuishi kwa amani bila bughuza.

Hata hivyo aliitaka halmashauri hiyo kuhakikisha kuwa inapima viwanja mara kwa mara ili wananchi wake kuendelea kupata maeneo ya kujenga na kuachana na kujenga maeneo ambayo hayahusiki.

Alisema kuwa haiwezekani halmashauri ikapima viwanja kila mara na sio baada ya miaka minne, na kuwa wananchi wanajenga kila wakati.

Hata hivyo diwani wa kata ya Njombe Mjini, Agrey Mtambo alilalamika viwanja vinavyo pimwa na halamshauri kuuzwa bei ghari na kusababisha wananchi kushindwa kuvimiliki.

Na Furaha Eliabu wa Habari Online na Elimtaa

WAFANYABIASHARA WA VIUMBE PORI HAI WAOMBA HURUMA YA RAIS MAGUFULI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Na Ally Daud-MAELEZO
WAFANYABIASHARA wa viumbe pori hai wamemuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kufungulia biashara ya viumbe hao kutokana na kusitishwa Machi mwaka huu na Waziri wa Maliasili na Utalii Jumanne Magembe.
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa wafanyabiashara wa Viumbe pori hai Bw. Salim Mussa amesema kuwa wanamuomba Mh. Rais Magufuli aingilie kati swala hilo na kupata ufumbuzi wa kudumu wa kuendelea na biashara hiyo ya viumbe kwa maendeleo yao na uchumi wa taifa.
“Tunakuomba Mh. Rais Magufuli uingilie kati swala hili na kutupatia ufumbuzi wa kudumu ili kuendlea na biashara ya viumbe pori hai bila ya usumbufu wa mara kwa mara kwani biashara hii ipo kwa mujibu wa sheria , taratibu na kanuni za nchi” alisema Bw. Salim.
Aidha Bw. Salim amesema kuwa maamuzi hayo yanaweza kusababisha hasara kubwa kwa jumuiya ya wafanyabiashara wa viumbe hivyo na uchumi wa nchi kwa ujumla kwani  muongozo haujatolewa tangu kusitishwa kwa biashara hiyo mwezi machi mwaka huu.
Kwa upande wake Msemaji wa wafanyabiashara wa viumbe pori hai Bw. Enock Balilemwa amesema kuwa kusitishwa kwa biashara hiyo imepunguza kiwango cha ajira kwa kiasi cha watanzania milioni moja ambao asilimia 95 wanaishi vijijini.
“kusitishwa kwa biashara hii ya viumbe pori hai imefanya watanzania takribani milioni moja hasa wakazi wa vijini asilimia 95 kukosa ajira jambo ambalo linapelekea wananchi hao kukosa uwezo wa kujikimu kwa maisha ya kila siku” alisema Bw. Balilemwa.
Biashara hiyo ya viumbe pori hai inayojumuisha Vyura, wadudu, ndege,mijusi na tumbili, zoo na mashamba ya wanyapori ilianza kabla ya uhuru sambamba na leseni zingine za uwindaji wa kitalii ambayo mpaka sasa inatambulika kwa sheria namba 5 ya mwaka 2009.

Serikali kukipandisha kituo cha afya cha Laela kuwa hospitali ya Wilaya

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO, Dodoma

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaendelea kukarabati kituo cha afya cha Laela kilichopo mkoani Rukwa ili kikidhi vigezo vya kuwa Hospitali ya Wilaya ikiwa ni moja ya jitihada za kupunguza adha ya wananchi kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya zilipo.

Hayo yamesemwa leo mjini Dodoma na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mhe. Suleimani Jafo alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Kwela Mhe. Ignas Malocha aliyehitaji kujua ni lini kituo hicho cha afya kitapewa hadhi ya kuwa Hospitali ya Wilaya.

Mhe. Jafo amesema kuwa ni uamuzi wa muda mrefu wa Serikali kuiweka Hospitali hiyo kuwa ya Wilaya na ndiyo sababu ya kufanya jitihada za kukiongezea uwezo kituo hicho kwa kujenga wodi nyingi pamoja na kutoa kibali cha kuajiri watumishi wapya kwani kwa sasa kituo hicho kina upungufu wa watumishi .

Amefafanua kuwa hadi sasa kuna baadhi ya majengo ambayo tayari yameshakamilika ambayo ni jengo la upasuaji wa dharura, wodi ya wagonjwa waliofanyiwa upasuaji pamoja na wodi ya mama wajawazito.

“Kwa sasa kituo cha afya cha Laela hakina miundombinu inayokidhi sifa za kuwa Hospitali ya Wilaya ila kutokana na kupanuka kwa Mji huo na kuongezeka kwa watu wanaohitaji huduma katika kituo hicho tumeamua kukiboresha ili kifikie hadhi ya kuwa Hospitali ya Wilaya”, amesema Jafo.

Ameongeza kuwa kwa sasa huduma za rufaa kwa wagonjwa wanaohudumiwa katika kituo hicho zinatolewa kupitia magari ya kawaida ya Halmashauri kutokana na ukosefu wa gari la kubebea wagonjwa lakini Wizara ina matarajio ya kutenga fedha ya kununulia gari hilo katika Bajeti ya mwaka 2017/2018.

Aidha, Mhe. Jafo amethibitisha kuwa kituo hicho kimetengewa jumla ya shilingi 9,358,100 katika Bajeti ya fedha ya mwaka huu ambayo itagharamia kununua dawa na vifaa tiba vitakavyorahisisha upatikanaji wa matibabu kwa wananchi wa eneo hilo.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Dkt Hamisi Kigwangalla amesema kuwa Wizara hiyo inaendelea kuipitia mikataba ya makampuni binafsi ili kuangalia namna ya kushirikiana nao katika kusaidia upatikanaji wa vifaa tiba katika Hospitali na vituo vya afya nchini.


KAMPUNI YA TANWAT YATOZWA FAINI YA MILIONI HAMSINI KWA UHARIBIFU WA MAZINGIRA

Na Lulu Mussa
Njombe

Wadau wa Mazingira wametakiwa kufuata Sera, Kanuni na Tararibu katika kuendesha shughuli zao.  Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. January Makamba ameyasema hayo leo Mkoani Njombe alipokuwa katika mwendelezo wa ziara ya kutembelea Mikoa mbalimbali hapa nchini kwa lengo la kujionea hali ya mazingira na kutoa maelekezo stahiki.
Waziri Makamba ametoza faini Kampuni ya TANMAT kwa kuikuka Sheria ya Mazingira inayokataza upandaji wa miti ndani mita sitini kutoka katika chanzo cha maji. "Kampuni hii imevunja sheria hivyo hamna budi kuchukuliwa hatua stahiki ili iwe mfano na kwa wengine" alisisitiza Waziri Makamba.
Kampuni hiyo imeagizwa kulipa faini hiyo ndani siku saba na endapo watakiuka hatua kali zaidi za kisheria zitachukuliwa dhidi yao. Waziri Makamba pia ameiagiza Kampuni hiyo kuondoa miti hiyo ambayo si rafiki kwa mazingira mapema iwezekanavyo na kuagiza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kuwapa 'Restoration Order"  kurudisha mazingira katika hali yake ya kawaida.
Katika hatua nyingine, Meneja wa Kampuni hiyo inayojishughulisha na upandaji wa miti Bw. Joseph Shirima amekiri kupokea barua zizoelekeza kusitisha uharibifu huo wa Mazingira katika chanzo cha Mto Mbukwa ambacho kinasambaza maji kwa wakazi wengi wa Wilaya ya Wanging'ombe.
Aidha, Waziri Makamba ameupongeza Uongozi wa Mkoa wa Njombe kupitia Mkuu wa Mkoa huo Dkt. Rehema Nchimbi kwa kuwa mstari wa mbele kuhamasisha wanachi kuacha kulima bustani za mbogamboga pembezoni mwa mito.
Dkt. Nchimbi alimfahamisha kuwa kwa sasa kuna kikundi kijulikanacho kwa jina la "Jerusalemu" kinachotoa mafunzo kwa wananchi juu ya matumizi bora ya ardhi na kuhamasisha uhifadhi wa mazingira ambapo lengo ni kuanzisha vituo kama hivyo vya mafunzo kwa Halmashauri zote za Mkoa huo.
Waziri Makamba alitembelea na kuona "vinyungu" ambavyo awali vilikua vikilimwa kando ya mito na kwasasa vimehamishiwa majumbani, katika kuunga mkono jitihada hizo njema Waziri Makamba amechangia mifuko Hamsini ya Saruji kwa ajili ya ujenzi wa darasa litakalotumika kutoa mafunzo zaidi ya kilimo.
Waziri Makamba Waziri Makamba anaendelea na ziara yake ya kikazi ya kukagua hali ya mazingira nchini, hii leo amewasili katika Mkoa wa Mbeya.

SHULE YA SEKONDARI YA MALANGALI YAPATA NEEMA KUTOKA KWA MALANGALI ALUMNI ASSOCIATION (MAAS)


Hawa ndio baadhi ya wanafunzi waliowahi kusoma katika shule ya sekondari ya Malangali wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya  kuwasili katika shule hiyo na kukaangalia mazingira ya shule hiyo na kutafuta njia za kutatua baadhi ya changamoto kwa kushirikiana na serikali ya Jamhuri ya muungano ya Tanzania
mkurugenzi wa kampuni ya Yono action mart Yono Kevela ambaye ni mlezi wa kundi la Malangali Alumni association (MAAS) akizungumza mbele ya wanafunzi wa shule ya sekondari Malangali na kuwaeleza jinsi gani shule hiyo ilivyowapa mafanikio hadi sasa walipofikia.



 na fredy mgunda,Iringa

Wanafunzi waliowahi kusoma shule ya sekondari ya Malangali iliyopo wilaya ya Mufindi mkoani Iringa wamewataka vingozi,wafanyabiashara,wakulima na wajasiliamali mbalimbali walinufaika na elimu kutoka shule ya malangali kurudisha fadhila katika shule hiyo.

Hayo yamesemwa na mkurugenzi wa kampuni ya Yono action mart Yono Kevela ambaye ni mlezi wa kundi la Malangali Alumni association (MAAS) alisema kuwa maendeleo aliyoyapata sasa ni kutoka na shule ya mangali hivyo ameamua kurudi na kuisadia shule hiyo. 

“Wafanyakazi na viongozi mblimbali tunatakiwa kuboresha mazingira na miundombinu ya shule tulizosoma ili kuendeleza na kukuza elimu ya hapa nchini tanzania.” Alisema Kevela

Kevela amesema kuwa shule nyingi walizosoma viongozi,wafanyabiasha na wajasiliamali mbalimbli zinahitajika kukarabatiwa hivyo amewataka wadau wote kuzikumbuka shule walizosoma.

Naye Padre wa kanisa la kikatoriki mkoani mbeya Telesipholi Tweve aliwakata wanafunzi mbalimbali waliosoma katika shule kongwe kurudisha upendo katika shule hizo kwa kuwa ndio chanzo cha mafanikio yao ya leo.

“Leo nimerudi katika shule hii ya malangali kuja kusaidia kutatua changamoto ambazo zipo katika shule hii ukizingatia kuwa shule hii inauchakavu wa majengo na miundombinu hivyo sisi kama MAAS tumeanza kwa kukarabati ukumbi ambao utakuwa na faida kwao kwa kutumia kwenye sherehe na kukodishwa pia”.alisema Tweve

Kwa upande wake mwenyekiti wa Malangali Alumni association (MAAS) Paul Mng’ong’o alisema kuwa wameanza kuisaidia shule ya Malangali muda mrefu kwa kuwa tayari wameshakarabati ukumbi wa shule,wamewanunulia tv na king’amuzi kwa ajili ya habari na wanaendelea kutatua matatizo ya shule hiyo.

“Hebu angalia sisi tuliosoma hapa tumepata mafanikio lakini shule yetu bado ipo pale pale na inazidi kuchakaa hivyo inatulazimu kuchangishana ili kurudisha fadhila kwa kuwa wengi wetu tumepata mafanikio makubwa kutoka shule hii,tunaviongozi wengi,matajili wengi ,wakulima wakubwa sana hapa nchini wote wamesoma katika shule hii”.Alisema Mng’ong’o

Lakini pia Mng’ong’o alisema kuwa lengo la kundi la Malangali Alumni Association kuunganisha wanafunzi wote waliowahi kusoma shule ya secondary ya Malangali na kuweza kupeana malengo na kusaidiana pale wanapokwama kimalengo.

Shule ya Malangali ni kati ya shule kongwe ambazo viongozi mbalimbali katika serikali,taasisiza Umma na sekta walijengewa msingi wa kwanza wa maisha.

kaika mwaka wa bajeti huu serikali imetenga bajeti ya kukarabati shule kongwe zipatazo thelethini na saba (37) jambo ambalo wananfunzi hao wameomba serikali kuharakisha utekelezaji wake.  
K

Sera ya Ajira kupitiwa upya



SERIKALI inapitia upya Sera ya Taifa ya Ajira ya mwaka 2008 ili kuangalia changamoto zilizomo. Mapitio hayo yatakamilika kabla ya Desemba, mwaka huu, lengo likiwa kutoa fursa kwa wadau kushirikiana na serikali katika suala zima la ajira nchini.
Mkurugenzi wa Ajira kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Ally Msaki alisema hayo jijini Dar es Salaam hivi karibuni na kuongeza kuwa hatua ya kuipitia sera hiyo, inatokana na kuwapo kwa mabadiliko mbalimbali.
Alisema, serikali itafanya kila linalowezekana, kuhakikisha kunakuwepo sera, sheria pamoja na kanuni rafiki, kwa maendeleo ya programu zinazokuza ujuzi na ajira kwa vijana.
“Sera hiyo imekuwa ikipitiwa na Taasisi ya Utafiti ya Kuondoa Umaskini (Repoa) na tayari ripoti inayoelezea hali halisi, imeshajadiliwa na wadau na sasa hivi wanaandika sera yenyewe,” alisema Msaki.
Alisema wadau, wameshiriki katika kuipitia sera hiyo, kazi kubwa imefanyika na imeangalia changamoto na matatizo mbalimbali yanayoikabili sera hiyo ili itakapokamilika itatoa mwanga wa wadau wengine kushirikiana na serikali katika suala la ajira.
Msaki alisema serikali itaendelea kusimamia sera hiyo ya elimu na mafunzo ya ufundi stadi, kwa lengo la kuweka msisitizo katika kuandaa mazingira na kutoa elimu ya ufundi stadi katika ngazi mbalimbali kuendana na mahitaji ya soko la ajira na hatimaye kuongeza ajira nchini.
Kuhusu mipango ya serikali katika juhudi za kukuza ajira, ni pamoja na kuimarisha utekelezaji wa mfuko wa maendeleo ya vijana ambao unalenga kuwasaidia vijana kujiajiri na kuwapa mikopo ya masharti nafuu na mafunzo ya ujasiriamali.
Alisema serikali itajikita katika kuhamasisha na kuwezesha uwekezaji kwenye viwanda vidogo, vya kati na vikubwa ili kufikia lengo la asilimia 40 ya nguvukazi nchini kuwa katika sekta ya viwanda ifikapo mwaka 2020, kulingana na mpango wa pili wa maendeleo wa miaka mitano kuanzia 2016/17 hadi 2020/21.

SERIKALI YAWAOMBA WANANCHI KUTOA USHIRIKIANO VITA DHIDI YA WAHUJUMU MIUNDOMBINU YA MAJI, YAAHIDI KUONGEZA HUDUMA YA UPATIKANAJI WA MAJI MIJINI NA VIJIJINI.



Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson LwengeAkizungumza katika kipindi cha TUNATEKELEZA kinachoratibiwa na Idara ya Habari (MAELEZO) na kurushwa na Televisheni ya Taifa (TBC)

Na. Aron Msigwa -Dar es salaam.
 
Serikali imesema kuwa itaendelea kuchukua hatua kali za kinidhamu na kisheria kwa watendaji wa sekta ya maji watakabainika kujihusisha na vitendo vinavyohujumu miundombinu ya maji kutokana na maslahi binafsi na kusababisha wananchi kukosa huduma maji katika maeneo mbalimbali nchini. 

Akizungumza katika kipindi cha TUNATEKELEZA kinachoratibiwa na Idara ya Habari (MAELEZO) na kurushwa na Televisheni ya Taifa (TBC) leo jijini Dar es salaam, Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge amesema baadhi ya watumishi wasio waaminifu wamekuwa wakijihusisha na vitendo vya kuhujumu miundombinu na miradi mipya ya maji inayoanzishwa na Serikali ili waweze kunufaika na biashara ya kuuza maji. 

Amesema Wizara yake imekwisha kuwasimamisha kazi Mameneja 9 waliokuwa wakihushishwa na wizi wa kimtandao wa maji katika maeneo mbalimbali hususani katika jiji la Dar es salaam.

‘’ Nimewasimamisha Mameneja karibu 9 waliokuwa wakihusika na wizi wa kimtandao wa maji na kuwafanya wananchi wakose huduma hii kwa muda mrefu, ninaomba wananchi watoe ushirikiano ili tuwakomeshe wahujumu hawa, tunahitaji kuondoa hali hii kwa kuwa maji ni uhai wa Taifa’’ Amesisitiza 

Amewaomba wananchi waendelee kutoa taarifa  kwa mamlaka zinazohusika pale watakapobaini vitendo vinavyoihujumu sekta hiyo ili ili hatua stahiki kwa wahusika zichukuliwe ikiwemo kuwafikisha mahakamani wale wote wanaojihusisha na vitendo vya wizi wa maji na kuwafanya wananchi wawe na malalamiko ya kukosa maji.

Akizungumza kuhusu vipaumbele vya Serikali ya awamu ya tano katika kuboresha sekta ya maji nchini amesema kuwa kiasi cha shilingi Trilioni moja kimetengwa kwa ajili ya kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji mijini na vijijini.

Amesema lengo la Sera ya Maji ni kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma ya maji safi ndani ya umbali wa mita 400 jambo ambalo linaendelea kutekelezwa na kuongeza kuwa tayari miradi ya maji 1200 kati ya 1800 mijini na vijini imekamilika na kuwezesha asilimia 72 ya wananchi vijijini kupata maji na asilimia 80 ya wananchi walio mijini kupata huduma hiyo.

Amesema Serikali imejitahidi kuwekeza kwenye miundombinu mikubwa ya maji katika maeneo ya mijini hasa katika mikoa yenye idadi kubwa ya watu ikiwemo jiji la Dar es salaam, Mbeya, Mwanza na miji mingine na kuongeza kuwa awamu inayofuata ni ujenzi wa miundombinu ya kusambazia maji katika maeneo mbalimbali.

‘’Katika awamu ya kwanza tumefanikiwa sana kuwekeza katika miundombinu mikubwa ya maji hasa kutoa maji kwenye vyanzo vya maji ikiwemo chanzo cha maji cha Ruvu Chini na Ruvu juu na mradi wa kuyatoa maji kutoka ziwa Victoria, sasa tunakwenda awamu ya pili ya ujenzi wa miundombinu ya kusambazia maji hayo’ Amebainisha Mhandisi Lwenge.

Ameongeza kuwa awamu hiyo ya pili pia itahusisha uondoaji wa miundombinu chakavu katika maeneo mbalimbali ambayo imekua ikisababisha upotevu wa maji kwa asilimia 47 pamoja na kuimarisha mifumo hiyo ili kutimiza lengo la Serikali la kufikia asilimia 95  ya kuwaunganishia maji wananchi ifikapo mwaka 2020.   

Akifafanua kuhusu utekelezaji wa miradi ya maji maeneo yanayozunguka ziwa Victoria amesema kuwa katika mwaka wa fedha wa 2016/2017 mradi wa maji katika vijiji 100 vilivyo pembezoni mwa bomba kuu la maji linalotoka ziwa Victoria hadi Kahama na Shinyanga itatekelezwa ili kuwawezesha wananchi wanaoishi katika vijiji hivyo kupata huduma ya maji safi.

Amesema mradi wa kuvipatia maji vijiji hivyo utakwenda sambamba na uboreshaji wa huduma ya maji kwenye vijiji 40 vilivyotambulika katika Halmashauri za Misungwi, Kwimba, Shinyanga na Msalala, Nansio, Geita na  Buselesele pamoja na uboreshaji wa miundombinu ya maji katika jiji la Arusha na mkoa wa Morogoro, Rukwa na Sumbawanga chini ya ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Ufaransa.

Aidha, kuhusu kilimo cha Umwagiliaji Mhe. Lwenge amesema kuwa Serikali imeanzisha Tume ya Umwagiliaji itakayokuwa na jukumu la kujenga mifumo na miundombinu ya maji pamoja na kusimamia na kutoa ushauri wa kitaalam kwa wananchi katika maeneo ya kilimo.

Ameeleza kuwa katika mwaka wa fedha 2016/2017 ,Serikali imetenga kiasi cha shilingi Bilioni 39 ili kuiwezesha sekta  hiyo kufanya vizuri na kuwaondoa wakulima kwenye kilimo kinachotegemea mvua pekee kwa kuwa na kilimo endelevu cha umwagiliaji na kutoa wito kwa wananchi kuanza kuvuna maji ya mvua katika maeneo yao.

Kuhusu ujenzi wa mfumo wa kusafisha maji taka katika jiji la Dar es salaam amesema kuwa katika mwaka wa fedha 2016/2017 Serikali itatekeleza mradi huo kwa kuweka mfumo mpya wa uondoaji na usafishaji wa majitaka yanayozalishwa katika jiji la Dar es salaam ili kuliweka jiji hilo katika hali ya usafi

Amesema mradi huo utahusisha upanuzi wa miundombinu ya maji taka kwenye maeneo ya katikati ya jiji, ujenzi wa miundombinu mipya ya kupitishia maji hayo katika maeneo ya Ilala, Kinondoni na Temeke.

"Serikali tumeanza kutekeleza mpango wa kupanua mfumo wa uondoaji na usafishaji wa majitaka yanayozalishwa na watumiaji maji , usanifu wa awali wa miradi mipya ya majitaka umekamilika,kazi inayoendelea ni usanifu wa kina ili kuweza kupata vitabu vya zabuni na michoro itakayotumika kumpata mkandarasi wa ujenzi" Amesisitiza Mhandisi Lwenge.

Amesema kuwa kupitia mpango huo bomba linalomwaga majitaka baharini litaacha kutumika na badala yake maji hayo yatapelekwa katika mtambo mpya wa kisasa wa kusafisha majitaka ambapo maji hayo ambayo yatakua yamesafishwa yatauzwa na kutumiwa katika shughuli mbalimbali za upozaji wa mitambo na umwagiliaji.

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa