Home » » FILIKUNJOMBE AKATAZA WANANCHI KUUZA MAHINDI BEI ‘CHEE’ YA SH.350

FILIKUNJOMBE AKATAZA WANANCHI KUUZA MAHINDI BEI ‘CHEE’ YA SH.350

Festus Pangani, Nombe Yetu
Mbunge wa jimbo la Ludewa mh Deo Haule Filikunjombe amewataka wananchi jimboni humo kutouza mahindi katika msimu huu wa kilimo kwa bei ya shilingi 350 kwa madai kuwa hiyo inawakandamiza na kuwanyonya wakulima.

Akizungumza kwa njia ya simu Filikunjombe amesema serikali imekuwa ikiwanyonya wananchi wilayani Ludewa kwa kununua mahindi yao kwa bei kandamizi wakati katika mikoa mingine mahindi hayo yamekuwa yakinunuliwa kwa bei ya shilingi 380.

Amehoji kuwa kama mbolea ya ruzuku inayotolewa kwa wakulima katika msimu wa kilimo haitofautiani nchini,ni kwa nini kwa jimbo la Ludewa pekee mahindi kutoka kwa wakulima yanunuliwe kwa bei ya shilingi 350 tofauti na mikoa mingine, na kuhoji kuwa shilingi 30 ambayo ni ongezeko kwa mikoa mingine inapelekwa wapi.

Amesema katika taarifa yake  wakala wa ununuzi mahindi katika ghala la chakula  lililoko katika mji wa Makambako mkoani Njombe imebainisha kuwa wamelazimika kununua mahindi kwa bei hiyo kutoka kwa wakulima wilaya ya ludewa kufuatia miundo mbinu ya barabara kuwa mbovu hali inayopelekea gharama kubwa katika suala la usafirishaji.
Blogzamikoa

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa