HASSAN MAAJAR TRUST YAKABIDHI MADAWATI 680 KWA RC WA NJOMBE.



 Mkuu wa mkoa wa NjombeKaptain Mstaafu Asseri Msangi katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi.

 Mkuu wa mkoa wa Njombe Kaptain Mstaafu Asseri Msangi (aliyekaa wa pili kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi Hassan Majaar Trust Bi. Zena Maajar Tenga (waliosimama wa pili kushoto) na Mwakilishi kutoka Kampuni ya Tigo pamoja na baadhi ya Walimu na Wanafunzi wakiwa katika picha ya ukumbusho.

Wanafunzi wakionyesha furaha baada ya kuboreshewa mazingira ya kusoma na Taasisi ya Hassan Maajar Trust ambayo lengo lake ni kutatua tatizo la Madawati nchini na kuhakikisha kauli mbiu yao ya “Dawati kwa kila mwanafunzi” inatimia.

MAFUTA YA PETROLI YAADIMIKA MKOANI NJOMBE

Festus Pangani, Njombe Yetu
Kwa siku ya tatu sasa mji wa Njombe umekumbwa na adha ya kukosekana kwa nishati ya mafuta ya petroli kwenye vituo vya mafuta hali inayopelekea kukwama kwa usafiri na kushuka kwa uchumi miongoni mwa jamii.
Hali hiyo imetokea kuanzia septemba 30 mwezi uliopita hadi sasa ambapo hadi hii leo ni kituo kimoja tu cha mafuta cha Ndime PetrolSstation kinauza mafuta hayo.
Wakizungumza na Njombe Yetu kwa nyakati tofauti baadhi ya madereva wa magari na pikipiki mjini Njombe wamesema kuwa adha hiyo imepelekea baadhi ya magari na pikipiki kuzima njiani yakiwa na abiria kitu ambacho kimeleta usumbufu kwa abiria.
Kwa upande wao mameneja wa baadhi ya vituo vya mafuta mjini hapa Prosper Mtewelewa wa kituo cha Ndime Petrol Station na Kaimu Meneja wa kituo cha mafuta cha Total wamesema tatizo hilo limetokea sehema ya kusambazia mafuta kutokana na siku za jumamosi na jumapili kutokuwepo kikazi.
Hata hivyo pamoja na kutokuwepo kwa mafuta mjini Njombe hakuna ongezeko lolote la bei ya mafuta mkoani hapa.
Blogzamikoa

TANESCO NA MWEKEZAJI KUTOKA MAREKANI KUZALISHA UMEME MEGAWATI 400

Na Festus Pangani, Njombe Yetu
Serikali ya Tanzania kupitia shirika la umeme tanesco kwa kushirikiana na mwekezaji kutoka nchini marekani, inajiandaa kutekeleza mradi wa umeme wa maji katika mto ruhuji.
Akizungmza wakati wa baraza la madiwani Mpimaji ardhi   mwandamizi wa Tanesco makao makuu Hamis Boby amesema mradi huo unatarajiwa kukamilika hadi kufikia mwaka 2019 na kuzalisha umeme wa megawati takribani mia tatu hadi mia nne.
Boby amesema mradi huo utahusisha ujenzi wa mgodi kufua  umeme wa megawati 350 hadi 400, bwawa la kuhifadhi maji, bwawa la kuzalisha umeme, njia ya umeme, barabara, njia ya kusafirisha maji chini ya ardhi, ofisI na makazi.
Hata hivyo amesema hatua hiyo itazingatia haki za wananchi katika eneo husika kwa kulipwa fidia ya ardhi, kupata huduma za kijamii, elimu ya mahusiano, pamoja na huduma nyingine zitakazopendekezwa kwenye makubaliano yao na wadau.
Kwa upande wao madiwani wa halmashauri ya mji wa Njombe na wilaya ya Njombe wameupongeza mpango huo wa serikali na kuwataka wawekezaji hao kutoa fidia kwa wananchi watakaohamishwa ili kupisha utekelezaji wa mradi huo bila ubaguzi wala upendeleo.
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ludewa Venancy Kabelege amewataka madiwani kushirikiana na serikali katika kuwahamasisha wananchi ili kufanikisha zoezi hilo la mradi.
Blogzamikoa

KATIBU MWENEZI WA CHADEMA MAKETE HASOMEKI......


Mwenyekiti  wa Chadema Taifa Mhe. Freeman Mbowe

Katika hali ambayo haikutegemewa na wengi, katibu wa itikadi na uenezi wa CHADEMA wilayani Makete Bw. Sinene amekifagilia chama cha mapinduzi kwa kusema kuwa kimejitahidi katika mambo yake ikiwemo kuwa na wanachama wengi wilayani hapo kwa zaidi ya asilimia 90

Sinene ameyasema hayo alipokuwa akitoa nasaha zake alipoalikwa kuhudhuria mkutano wa uchaguzi wa CCM uliofanyika jana kwenye ukumbi wa shule ya sekondari Iwawa wilayani hapo

Katibu huyo alisema “nikilinganisha huko nyuma na hii leo kwa kweli chama chenu kimejitahidi kwa zaidi ya asilimia 90, mna wanachama wengi na mnaendelea kufanya mengi”

Awali wakati akianza kutoa salamu zake alisema unapokwenda sehemu inabidi utumie taratibu za eneo hilo, hivyo kulazimika kusema ‘CCM hoyeeeeeee’ hali iliyowafurahisha wajumbe wa mkutano huo wakiwemo viongozi wa CCM

Baada ya kumaliza salamu zake hizo kulipelekea utani wa hapa na pale ikiwemo kumvalisha kofia ya CCM ingawa alikataa kuivaa huku wengine wakitaka kumpa shati la kijani, na sauti za kumkaribisha CCM zikisikika

Akizungumza mara baada ya kiongozi huyo wa CHADEMA kumaliza kutoa salamu zake, katibu wa CCm wilaya ya Makete Miraji Mtaturu alisema ni kweli chama chake ni kikubwa na wapinzani watazidi kupata tabu kama alivyokiri mwenyewe

“Ndugu wajumbe kauli ya katibu mwenezi wa CHADEMA mmeisikia wenyewe, kwa kawaida katibu mwenezi ni msemaji wa chama, hivyo kauli yake ni kauli ya chama, nachopenda kumwambia hakuna haja ya kupoteza muda, njoo CCM ndugu yangu” alidai Mtaturu

Kauli hiyo ya katibu mwenezi wa CHADEMA ilizua gumzo miongoni mwa wanachama wake waliokuwa nje ya ukumbi huo huku wakisikika wakisema amejimaliza kisiasa na kuona hana haja ya kuendelea kuwepo ndani ya Chadema na badala yake ahamie CCM aliyoifagilia

Kauli hiyo pia ilitumiwa na wagombea wa CCM katika uchaguzi huo hasa wale waliokuwa wakitetea nafasi zao akiwemo Mzee Mwamwala kwa kusema kuwa “katika uongozi wangu nimefanya mengi mazuri hadi mmesikia mwenyewe CHADEMA wanaikubali CCM na wasingeikubali bila uongozi wangu mahiri, hivyo naomba kura zenu”

Pamoja na kutumia fursa hiyo Mzee Mwamwala alishindwa kutetea kiti chake na nafasi yake ilichukuliwa na Francis Chaula aliyepata kura 791 dhidi ya Mwamwala aliyepata kura 155
Francis Godwin Blog
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa