MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ASHIRIKI IBADA YA MAZISHI YA ASKOFU MSTAAFU, MHASHAM RAYMOND MWANYIKA ILIYOFANYIKA MKOANI NJOMBE LEO.


  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka shada la maua juu ya kaburi ya Askofu Mstaafu, Mhasham Raymond Mwanyika, wakati wa shughuli za maziko zilizofanyika leo katika Kanisa Katoliki Njombe.
 Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitia saini katika kitabu cha maombolezo ya Askofu Mstaafu, Mhasham Raymond Mwanyika, wakati wa shughuli za maziko zilizofanyika leo katika Kanisa Katoliki Njombe. 
  Makamu wa Rais, Dkt Bilal, akitoa heshima za mwisho.
Picha na OMR.

RAIS KIKWETE ATEMBELEA MGODI WA CHUMA WA LIGANGA,LUDEWA MKOANI NJOMBE


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo toka kwa Meneja mradi wa Maganga Matatitu Resource Development limited Bw. Lawrence Manyama kuhusu mlima huo uliosheheni mashapu ya chuma alipotembelea eneo lenye utajiri wa chuma la Liganga wilaya ya Ludewa mkoani Njombe leo Oktoba 22, 2013.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na wawekezaji wa kampuni ya Sichuan Hongda ya China ambao ni wawekezaji katika eneo lenye utajiri wa chuma la Liganga wilaya ya Ludewa mkoani Njombe leo Oktoba 22, 2013. Kampuni hiyo inatarajiwa kujenga kiwanda cha kufua chuma mapema mwakani kitachajiri watu 32,000 kitakapokamilika.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akionesha kilele cha Central Liganga hill ambacho ni mojawapo ya sehemu ambazo kampuni ya Sichuan Hongda ya China itachimba mashapu ya chuma na kuyafua katika kiwanda kikubwa cha kufua chuma kitachoajiri watu 32, 000 katika eneo hilo lenye utajiri wa chuma la Liganga wilaya ya Ludewa mkoani Njombe leo Oktoba 22, 2013. Kampuni hiyo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na wananchi alipoowasili katika uwanja wa mikutano wa Ludewa ambako alihutubia mkutano wa hadhara. PICHA NA IKULU


 Sikiliza Tone Radio Tz : http://www.toneradiotz.com/listenlive.php

ZIARA YA RAISI JAKAYA KIKWETE KATIKA MKOA MPYA WA NJOMBE

 Rais akitoka kuweka jiwe la msingi madarasa ya kidato cha tano shule ya sekondari lupalilo.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakiongea na Bi Sarah Mageni Sanga, mlemavu ambaye Rais alimpa pikipiki ya Bajaji pamoja na mtaji wa pesa taslimu wa shilingi milioni mbili October 28, 2009 baada ya kuguswa na mkasa wa maisha ya mkaazi huyo wa kijiji cha Lupalilo wilaya ya Makete mkoa wa Njombe alipomuona akohojiwa katika TV na kueleza kuwa maisha yake ni magumu mno baada ya ndugu na jamaa zake wote kuteketea kwa maradhi ikiwa ni pamoja na UKIMWI. Pichani Bi Sanga akimshukur Rais kwa msaada huo ambao amesema umebadili kabisa maisha yake kwani sasa anaishi kama mtu yeyote kijijini hapo
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongeana wananchi wa kijiji cha Ivalalila wilayani Makete baada ya kuweka jiwe la msingi la kituo cha afya cha kijiji hicho mwishonimwa juma.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kufungua rasmi  Chuo cha Ufundi Stadi cha VETA cha Wilaya ya Makete mwishoni mwa juma
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akishuhudia ubora wa shati lililotengenezwa na wanafunzio wa Chuo cha Ufundi Stadi cha VETA cha Wilaya ya Makete baada ya kukifungua rasmi chuo hicho mwishoni mwa juma

MFANYABIASHARA NA DIWANI WA KATA YA NJOMBE MJINI LUPYANA FUTE[Jacky's]AMEFARIKI DUNIA GHAFLA


Lupyana Fute enzi  za uhai wake akizungumza Kwenye Moja ya Vikao vya Baraza la Madiwani Enzi za Uhai Wake.
...................................................................................................................
Na Mwandishi Wetu.

Diwani wa Kata ya Njombe Mji Lupyana Fute  ambae  pia aliuwa mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa NEC Wilaya ya Njombe amefariki dunia Ghafla Jioni ya jana mjini Njombe .

Taarifa za awali toka kwa Mashuhuda wa tukio hilo Akiwemo Solanus Mhagama Amesema Kuwa Kwa Mara ya Mwisho Marehemu Lupyana Fute alimpigia Simu na Kumwambia amtafutia Gari la Kikosi cha Zima Moto na Uokoaji Baada ya Moto Kuzuka Kwenye Chumba cha jengo la Ofisi yake Iliyopo Karibu na Tumaini Dispensari.


Bwana Mhagama Amesema Kuwa Mara Baada ya Kufika Kwa Gari hilo na Kufanikiwa Kuzima Moto Kwa Kushirikiana na Wananchi moto uliokuwa Ukiwaka Kwenye Chumba Cha Kuhifadhia Vitu[STOO] ndipo Marehemu alipoingia Ofisini Kwake alikopotezea fahamu.

Aidha amesema Kuwa Walipoingia Ndani ya Chumba Ofisini Kwake Walimkuta Marehemu Fute akiwa amepoteza fahamu huku akiwa ameketi Kwenye Kiti Chake Ndipo walipomchukua na Kumwahisha Katika Hospitali ya Kibena.Mara Baada ya Kufika Katika Hospitali ya Mji Njombe Kibena Ndiko Waliko ambiwa ameshafariki.

Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Njombe Bw. Edwin Mwanzinga amesema ni Kweli diwani huyo amefariki dunia  na  kuwa taarifa zaidi zitaendelea Kutolewa.

Na Francis Godwin

RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE AZINDUA RASMI CHUO CHA VETA MAKETE‏


 Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na viongozi wa VETA wakati akiwasili chuo cha VETA Makete kwa ajili ya kukizindua, kushoto kwake ni mkurugenzi wa VETA Tanzania Zebedayo Moshi
 Rais kikwete akikata utepe kuashiria kukifungua chuo cha VETA Makete
 Rais Jakaya kikwete akielekea kujiones shughuli zinazofanywa na VETA Makete katika majengo ya chuo hicho, katikati ni mkurugenzi wa VETA nchini Zebedayo Moshi, kulia ni mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro
 Rais jakaya Kikwete akipata maelekezo kutoka kwa mwanafunzi wa veta makete kuhusu namna ya kutengeneza batiki
 Rais jakaya Kikwete akipata maelekezo kutoka kwa mwanafunzi wa veta makete kuhusu namna ya kuweka rangi kwenye batiki
 Mwalimu wa ujenzi chuo cha VETA Makete Mwl. Mathew Komba akitoa maelezo ya shughuli za ujenzi kwa rais Jakaya Kikwete
 Tofali za kisasa zinazotumia udongo na saruji katika kuzitengeneza zilioneksns kuwa kivutio kikubwa kwa rais Jakaya Kikwete.Kulia kwa rais ni mama Salma Kikwete na waziri wa elimu Dk Shukuru Kawambwa
 Rais jakaya Kikwete akipanda mti wa kumbukumbu katika chuo cha VETA Makete
 Mkurugenzi wa VETA nchini Zebedayo Moshi akitoa taarifa ya chuo kwa rais Kikwete
 Waziri wa Elimu Dk Shukuru Kawambwa akizungumzia kuhusu chuo cha VETA Makete
Rais jakaya Kikwete akizungumza na wananchi katika chuo cha VETA Makete
Picha ya pamoja na wanafunzi wa kozi fupi waliohitimu Chuoni hapo
(picha zote na EDDY BLOG)

RAIS KIKWETE ASIMIKWA UCHIFU WA KABILA LA WABENA MKOANI NJOMBE


Rais Jakaya Kikwete akipokea Mkuki wakati akisimikwa Uchifu wa Kabila la Wabena na mmoja wa wawakilishi wa Wazee wa Kabila hilo,kwenye wa Hafla ya Uzinduzi wa Mkoa wa Mpya wa Njombe.
Wazee wa Kabila la Wabena wakimsimika Uchifu Rais Jakaya Kikwete.
Chifu Mpya wa Kabila la Wabena,Rais Jakaya Kikwete akiwahutubia wakazi wa Mkoa Mpya wa Njombe.
Chifu Mpya wa Kabila la Wabena,Rais Jakaya Kikwete akiteremka Jukwaani baada ya kusimikwa Uchifu wa Kabila hilo na kuwahutubia wananchi wa Mkoa wa Njombe.
Rais Jakaya Kikwete akipongezwa na Mkewe Mama Salma Kikwete baada ya kusimikwa Uchifu wa Kabila la Wabena,wakati wa Hafla ya Uzinduzi wa Mkoa wa Mpya wa Njombe.
Pongezi zikiendelea.
Machifu wa Kabila la Wabena wakiwa kwenye picha ya Pamoja.

Picha na Ikulu

RAIS KIKWETE NAMNA ALIVYOFUNGUA KIWANDA CHA CHAI IKANGA WILAYANI NJOMBE.



Rais Jayaka Mrisho Kikwete akikagua sehemu mbalimbali za kiwanda cha chai cha Ikanga wilaya ya Njombe baada ya kukifungua Oktoba 18, 2013

Rais Jayaka Mrisho Kikwete aki furahi na mkurugenzi wa kampuni ya mufindi tea & coffee limited baada ya kufungua kiwanda cha chai cha Ikanga wilaya ya Njombe baada ya kukifungua Oktoba 18, 2013.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua sehemu mbalimbali za kiwanda cha chai cha Ikanga wilaya ya Njombe baada ya kukifungua Oktoba 18, 2013. Rais Jayaka Mrisho Kikwete akihutubia mkutano wa hadhara baada ya kufungua kiwanda cha chai cha Ikanga wilaya ya Njombe baada ya kukifungua Oktoba 18, 2013.

Picha na Ikulu 

RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE AZINDUA RASMI MKOA WA NJOMBE JANA.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akibofya kitufe huku wazee wa Njombe wakirusha njiwa kuashiria kuzinduliwa rasmi mkoa wa Njombe leo Oktoba 18, 2013 katika Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa Maisha Bora kwa Watanzania hajawezi kuja kwa watu kushinda wanacheza mchezo wa pool badala ya kujihangaisha kwa kufanya kazi na shughuli nyingine za kujiingizia mapato.
 
Aidha, Rais Kikwete ameahidi kuwa Serikali yake itakomesha haraka iwezekanavyo kero ya wananchi wa sehemu za Mkoa wa Njombe kulazimika kupanda mitini ili kupata mawasiliano ya simu za mkononi.
 
Rais Kikwete amayesema hayo leo, Ijumaa, Oktoba 18, 2013, wakati alipohutubia mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Wanginyi, Kata ya Lupembe, Wilaya ya Njombe katika Mkoa Mpya wa Njombe kwenye siku yake ya kwanza katika ziara yake ya siku saba kukagua na kuzindua miradi ya maendeleo katika Mkoa huo.
 
Akizungumza na wakazi wa Kijiji hicho na vijiji vya jirani, Rais Kikwete amezungumzia dhana nzima ya Maisha Bora kwa Watanzania akisisitiza kuwa maendeleo na Maisha Bora kwa Kila Mtanzania hajawezi kupatikana kwa watu kushinda wanacheza mchezo wa pool mchana kucha.
 
“Ndugu zangu, nimepata kusema huko nyuma na nataka kurudia tena kuwa Maisha Bora kwa Kila Mtanzania yanawezekana kwa watu kujituma na kuchapa kazi na siyo kwa watu kushinda kwenye meza za pool wakipiga kale kampira huko wakiilaumu Serikali na kuulizana ‘Maisha Bora yako wapi?’”
 
Ameongeza Rais Kikwete: “Inawezekana kweli Maisha Bora yakaja kwa mtu anayeshinda anagonga mpira wa pool kwenye meza? Ni kwa kufanya kazi kwa bidii na shughuli nyingine za kutuingizia kipato ndipo maisha yetu yatakapokuwa bora.”
 
Kuhusu hali ya mawasiliano ya simu Mkoani Njombe, Rais Kikwete, baada ya kuwa ameambiwa kuwa katika baadhi ya sehemu za Mkoa huo, watu wanalazimika kupanda juu ya miti ili kupata mawasiliano, alisema kuwa Serikali yake itakomesha haraka kero hiyo.
 
“Ni ajabu na aibu kabisa kwamba watu wanalazimika kupanda miti ili kupata mawasiliano….Hii ni hatari … kwa sababu mtu anaweza kuanguka na kuvunja viungo…mtu anaweza kuvunja kiuno,” alisema Rais Kikwete huko watu wakiangua kicheko.
 
“Tutahakikisha kuwa watu hawavunjiki viungo kwa sababu ya kupiga ama kupokea simu za ndugu zao,” Rais Kikwete amewahakikishia wana-Njombe.
 
Katika kufafanua azma hiyo ya Serikali kumaliza kero hiyo, Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Mheshimiwa Profesa Makame Mbarawa amesema kuwa Serikali italimaliza tatizo la mawasiliano katika Mkoa wa Njombe kwa awamu mbili.
 
Alisema kuwa katika awamu ya kwanza, kiasi cha sh milioni 260 zimetengwa kwa ajili ya kuboresha mawasiliano katika vijiji 25 vya Jimbo la Uchaguzi la Njombe Kaskazini na kuwa kazi hiyo itakuwa imekamilika ifikapo Machi, mwakani, 2014. “Tunataka watu waache kupanda miti kwa kutafuta mawasiliano ya simu tu.”
 
Amesema kuwa katika awamu ya pili, kiasi cha sh bilioni 1.552 zitatumika kutoka Mfuko wa Mawasiliano Vijijini kwa ajili ya kuboresha mawasiliano ya simu katika Mkoa mzima wa Njombe.
 
Amesema kuwa kazi ya kuboresha mawasiliano katika awamu hiyo ya pili, itakamilika ifikapo Agosti, mwakani, 2014.
 
Kuhusu matumizi ya simu zenyewe, Mheshimiwa Mbarawa amewataka Watanzania kuzitumia simu hizo za mkononi vizuri kwa mawasiliano ya maana na yasiyokuwa na ovyo ikiwa ni pamoja na kutukana watu. “Tuzitumie simu zetu vizuri kwa mawasiliano mazuri na ya maana na siyo kutumia simu kujenga na kusambaza fitina na majungu ama kushiriki matusi dhidi ya watu wengine.”
 
Baadaye jioni, Rais Kikwete alikuwa anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika sherehe za Uzinduzi Rasmi wa Mkoa wa Njombe kwenye Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe.
Picha na Ikulu

Wavurugaji wa Katiba ,walimtaka JK asaini mswada pasipo kuangalia bada ya kutokuwepo nchini.

WAZALENDO NET..
JK awatibulia Wassira, Chikawe • Filikunjombe asema wanapaswa kuwaomba radhi wananchi
na Waandishi wetu
HATUA ya Rais Jakaya Kikwete kukutana na viongozi wa vyama vya siasa vyenye wabunge na kuridhia muswada wa sheria ya marekebisho ya sheria ya mabadiliko ya katiba urejeshwe bungeni, imeungwa mkono na wengi, huku mawaziri wake wakisutwa.
Mawaziri hao ni Stephen Wassira (Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu), Mathias Chikawe (Katiba na Sheria) na William Lukuvi wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge).
Kwa nyakati tofauti baada ya vyama vya CHADEMA, CUF na NCCR-Mageuzi, kususia muswada huo bungeni waliwakejeli wakidai kuwa wanapoteza muda kwani safari hii hakuna nafasi ya kukutana na Rais Kikwete kama ilivyokuwa awali mwaka 2011.
Mawaziri hao waliongeza kuwa viongozi wa upinzani wanatamani kwenda Ikulu kunywa chai na juisi, huku wakisisitiza kuwa milango hiyo sasa imefungwa na rais lazima asaini muswada huo kama ulivyopitishwa na Bunge, kwamba kutofanya hivyo ni kutangaza mgogoro na wabunge.
Licha ya kejeli hizo, Rais Kikwete aliamua kukutana na viongozi wa vyama hivyo vitatu jana huku akiwashirikisha pia wale wa CCM, TLP na UDP ambao wabunge wao waliupitisha muswada huo.
Akizungumza jana na gazeti hili, Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe (CCM), alimpongeza rais kwa hatua hiyo na kumtahadharisha awe makini na wabunge wa chama hicho, akidai wamekuwa wakitumia wingi wao vibaya bungeni.
Filikunjombe alisema Kikwete ameonesha ukomavu na kwamba hiyo ndiyo demokrasia ya kuwasikiliza wachache pia.
“Kwenye katiba hakuna mshindi, muswada uliopitishwa si wa CCM, katiba si ya CCM, inapaswa kuwa ya wananchi wote hata wachache wasikilizwe.
“Katiba mpya haikuwa ajenda ya CCM, rais aliichukua labda kutoka chama kingine akaona inafaa. CCM wamepokea suala la mabadiliko ya katiba bila kukubali maumivu yake, ndiyo maana tunafikia hatua hii,” alisema.
Alifananisha hatua hiyo na mtu unayetaka kufika mbinguni halafu hutaki kufa, hivyo kuwataka wenzake wakubali mabadiliko na maumivu yake.
“Mimi ninamtia moyo Rais Kikwete asimamie vizuri suala la katiba, ila ajue wabunge wengi wa CCM tunamharibia, awe makini na sisi, kwani mara nyingi tunatumia wingi wetu vibaya.
“Imekuwa aibu sasa mara ya pili rais anarejesha muswada kufanyiwa marekebisho, ingefaa wabunge wa CCM tujitafakari, sisi tunamtumikia nani?”alihoji.
Filikunjombe aliongeza kuwa katika hilo Kikwete ameonesha amedhamiria kwa dhati kuusimamia mchakato, hivyo aungwe mkono.
Akizungumzia kauli za kejeli za mawaziri, mbunge huyo machachali alisema hao wana akili mgando tu, yafaa wawaombe radhi Watanzania.
“Na hii ni kwa sababu hapa kwetu utamaduni wa kujiuzulu haupo, lakini vinginevyo hizo si kauli za kusemwa na mawaziri,” alisema.
Alipotafutwa Waziri Wassira, kuelezea msimamo wake baada ya mazungumzo ya rais na viongozi wa vyama, alijibu kwa kifupi akiomba aulizwe Waziri Chikawe, kwa maana kwamba yeye hakuwa na la kusema.
Waziri Chikawe naye alipotafutwa, aliomba apigiwe simu baadaye kwa maelezo kuwa hakuwa katika nafasi ya kuzungumza kwa wakati huo.
Ndugai asahau kanuni
Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, ambaye alisimamia ubabe wote bungeni hadi muswada kupitishwa na kasoro hizo, alipotafutwa alionesha kushangaa, kwa maana kuwa hajui wapinzani wanabishania nini na walikwenda kumuona rais kwa suala lipi.
“Ni issue (suala) gani hasa ambayo inahitaji udharura wa aina hiyo, unaposema wataurejesha muswada katika Bunge lijalo, je, kanuni zinaruhusu?
“Mimi sioni mantiki yoyote, labda wanaozungumza hoja ya uteuzi wa wajumbe 166, kama rais hataki hilo ni suala jingine, ila sisi tuliona rais ndiye chombo kinachofaa kuchuja wajumbe hao,” alisema.
Kwa mujibu wa Ndugai, bila mamlaka ya kuchuja wanaweza kujikuta wana wajumbe wa kutoka kanda, dini au jinsia moja, kwamba mamlaka ya kuchuja inahitajika.
Kuhusu muswada kurejeshwa bungeni, Ndugai alisema hana uhakika kama utarejeshwa, ila anachofurahi yeye ni kusikia kuwa muswada umesainiwa.
CCM wakubali
Chama Cha Mapinduzi kupitia kwa Katibu wake wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alisema Rais Kikwete kwa kusaini inaonesha anafuata sheria, lakini pia wanampongeza kwa kukutana na viongozi wa siasa.
Alisema kuwa yale yatakayorejeshwa bungeni, wabunge wataamua kama wakiona yana hoja wasikilize na wakiona hayana watajua wao kwa vile Bunge ni mhimili huru.
Kuhusu kauli za kejeli za baadhi ya mawaziri, Nape alisema hajui na hajawahi kusikia.
Naye Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM), Sadifa Khamisi, alisema Bunge ni chombo huru, hivyo litaangalia kama kuna masuala ya kubadili.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Alexanda Makulilo, kwa upande wake alisema rais ametumia busara kuwasikiliza wapinzani, kwa kuwa aliona wana hoja.
Alisema marekebisho yafanyike, wabunge sasa wakafanye majadiliano vizuri, waone umuhimu wa hoja na waweke masilahi ya vyama pembeni na kutanguliza manufaa ya nchi.
Viongozi wa dini wasifu
Baadhi ya viongzoi wa dini wamemsifu Rais Kikwete kwa hatua ya kukutana na viongozi wa vyama, kwamba kitendo hicho ni pigo kwa mawaziri ambao wameifanya Ikulu kuwa hatimiliki yao.
Akizungumza na Tanzania Daima jana, Mwenyekiti wa kamati ya viongozi wa dini wa taaluma, maadili na haki za binadamu kwa jamii, Mchungaji William Mwamalanga, alisema Kikwete ana nia njema lakini watendaji wake wamekuwa wakimpotosha.
Mwamalanga alisema kuwa hatua hiyo ya kuwa na majadiliano ya pamoja imeonesha ujinga uliokuwa ukifanywa na baadhi ya watendaji ambao wamekuwa wakitoa kauli za kukejeli wapinzani.
“Huwezi kuwa na hatimiliki ya Ikulu, hili ni lazima mawaziri Lukuvi, Chikawe na Wassira wakatambua. Maana hatua ya Rais Kikwete kukutana na viongozi hao imewadhalilisha wao mawaziri,” alisema.
Kiongozi huyo alisema kuwa watendaji hao ndio waliokuwa wakipotosha katika suala hilo na kumlazimisha asaini muswada huo haraka bila kuangalia kasoro.
Alisema kuwa ni muhimu sasa Rais Kikwete akasimamia utekelezaji wa makubaliano hayo ili malengo yaliyowekwa yakaweza kufikiwa.
Mwamalanga alisema kuwa iwapo Rais Kikwete atayaacha makubaliano hayo na kuwaachia watendaji hao kuna uwezekano wa kutokea kwa mtafaruku mkubwa ndani ya nchi katika suala hilo

Tingatinga likibomoa majengo makete mjini‏


 Tingatinga likibomoa huku kulia wakionekana wamiliki wa jengo hilo wakiokota masalia ya vitu wanavyoona vitawafaa kwa badaye
 Masalia ya zoezi la bomoa bomoa yakipakiwa kwenye lori tayari kwenda kumwagwa mbali
 Tingatinga likibomoa kuta za nyumba ambazo zipo kwenye hifadhi ya barabara Makete mjini
Baada ya kumaliza kazi hapa linaondoka kuelekea eneo jingine(picha zote na EDDY BLOG)

TASWIRA YA MAONESHO YA UZINDUZI WA MKOA MPYA WA NJOMBE HAPO OKTOBA 18 MWAKA HUU.








Na Sunday Bavuga   Njombe
Wananchi Mkoani Njombe Wametakiwa Kujitokeza Kwa Wingi Kwenye Maonyesho ya Uzinduzi wa Mkoa wa Njombe Yanayoendelea Katika Uwanja wa Sabasaba Mjini Njombe.
Wakiongea Kwa Nyakati Tofauti Baadhi ya Washiriki wa Maonyesho Hayo Wamesema Bado Mwamko wa Wananchi Kufika Kwenye Maonyesho Hayo ni Mdogo .
Aidha Washiriki Hao Wamewataka Wananchi wa Mkoa wa Njombe na Mikoa ya Jirani Kufika Kwenye Maonyesho Hayo Ili Kujipatia Bidhaa Mbalimbali Zinazotengenezwa na Watanzania Wakiwemo 
Wajasiriamali
.
Maonyesho Hayo Yameanza Oktoba 11 Mwaka Huu na Kilele Chake Itakuwa Oktoba 18 Mwaka 2013 Siku Ambayo Itakuwa ya Uzinduzi Rasmi wa Mkoa wa Njombe Ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete Anatarajiwa Kuwa Mgeni Rasmi.
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa