Sara Dumba kuzikwa kesho

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Sara Dumba enzi za uhai wake
MKUU wa Wilaya ya Njombe, Sara Dumba aliyefariki ghafla juzi jioni, anatarajiwa kufanyiwa ibada leo mjini Njombe na kuagwa rasmi na wananchi wa wilaya hiyo na Mkoa wa Njombe na baadaye jioni kusafirishwa kuja jijini Dar es Salaam ambako ndiko atakapozikwa.
Kwa mujibu wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Njombe, Jackson Saikadau, ratiba ya awali inaonesha kuwa Dumba anatarajiwa kuzikwa kesho nyumbani kwake eneo la Mbutu Mwembe Mdogo Kigamboni na msiba wake utafanyika Kigamboni nyumbani kwa baba yake mzazi eneo la Ferry Midizini.
Saikadau alisema ratiba hiyo inaonesha kuwa mwili wa marehemu ambao baada ya mauti ulihifadhiwa katika Hospitali ya Ilembula, utawasili mjini Njombe saa nne asubuhi kwa ajili ya ibada na baadaye kuagwa na wananchi.
“Tunatarajia kuanza safari majira saa 10 jioni kutoka Njombe kwenda Dar es Salaam na maiti itawasili jijini humo alfajiri siku ya Alhamisi (kesho) kwa ajili ya taratibu za msiba na mazishi,” alisema Saikadau. Alisema Dumba alifariki ghafla juzi baada ya kusumbuliwa na tatizo la shinikizo la damu.
Alisema kabla ya mauti, alilalamika kusumbuliwa na kichwa na hivyo kukimbizwa katika Hospitali ya Kibena, lakini pamoja na jitihada za madaktari za kuokoa maisha yake, alifariki dunia majira ya saa moja na nusu usiku.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Makete, Daudi Yassin alisema mkoa umepata pigo kwa kuondokewa na Dumba ambaye katika uhai wake ndiye aliyekuwa Mwenyekiti wa Wakuu wa Wilaya wa mkoa huo wa Njombe.
“Kwa kweli huu msiba umetushtua sana, kwani Jumamosi iliyopita tulikuwa na Dumba katika sherehe za kumpokea Mkuu wetu wa Mkoa, Rehema Nchimbi baada ya kuapishwa, kwa kweli mchango wake utakumbukwa sana,” alisema Yassin.
Kitaaluma Dumba ni Mwandishi wa Habari aliyekuwa mtangazaji wa iliyokuwa Radio Tanzania ambao kwa sasa inajulikana kama Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).
Aidha, alishika nyadhifa mbalimbali za ukuu wa wilaya katika maeneo tofauti zikiwemo wilaya za Kilindi na Njombe alikofikwa na mauti.
Katika hatua nyingine, Rais John Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Dk Rehema Nchimbi kutokana na kifo cha ghafla cha Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Sara Dumba.

Chanzo Gazeti la Habari leo

Vyama vya ushirika Hufa kutokana na madeni makubwa

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

WANAWAWAKE KUMILIKI ARDHI BADO NI NDOTO MAKETE MKOANI NJOMBE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Hii  ni Ofisi ya afisa Mtendaji Kata ya Iwawa, Kituo cha wakulima

Na Blogs za Mikoa Tanzania
Mila potofu zinazokandamiza wanawake zimeripotiwa kuendelea kushamiri katika baadhi ya mambo baada ya kutembelea katika maeneo tofauti tofauti ya wilaya ya Makete mkoani Njombe na kuzungumza na wakazi wa wilaya hiyo

Katika kijiji cha Iwawa wilaya ya Makete mkoani Njombe mwananchi aliyejitambulisha kwa jina la Jane Sanga amesema wanawake wengi wilayani hapo hawamiliki ardhi kutokana na mila potofu kuwa wamiliki wa ardhi ni wanaume pekee
"Kwa hapa Makete wanawake unaowaona wanamiliki ardhi kwa kiasi kikubwa unakuta ni mjane anaimiliki baada ya kufiwa na mumewe au unakuta mwanamke huyo ana uwezo wa kifedha na ameamua kukunua kipande chake cha ardhi na anakimiliki mwenyewe, hapo hakuna anayemuingilia, na hata wale wajane bado utakuta wanasumbuliwa na ndugu wa marehemu mumewe, kwa hiyo bado hali ni ngumu" amesema Jane
Hiki ni kipande kidogo sana ambacho analima Bi. Jane(Hayupo Pichani)

Mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Grace Mbilinyi ambaye amekutwa na mwandishi wetu akiandaa shamba kwa ajili ya kilimo cha mazao ya chakula katika msimu ujao, amesema anamiliki shamba aliloachiwa na marehemu mumewe, licha ya kuendelea kusumbuliwa na ndugu wa marehemu wakidai kuwa mwanamke hataweza kuendeleza ardhi aliyoachiwa na mumewe

"Kwa kweli ni shida lakini Tutafanyaje sasa, mimi ni mama  wa nyumbani ambaye sana sana najishughulisha na ujasiriamali na kilimo kama hivi, kwa sasa ninamiliki hili shamba nililoachiwa na mume wangu kwa ajili ya kilimo, lakini vijimaneno vya ndugu vipo lakini bado sikati tamaa maana uwezo wa kumiliki ninao, na nitaiendeleza kwa kilimo" amesema Bi Grace

James Sigala ni mkazi wa Makete ambaye amekiri kuwepo kwa mila hizo zinazokandamiza wanawake hasa katika umiliki wa ardhi na kusema ingawa elimu inaendelea kutolewa na wanaharakati lakini bado kuna haja ya kuendelea kuitoa ili jamii ibadilike na kuamini kuwa hata wanawake wanaweza kimilikishwa ardhi kama wanaume
Afisa mtendaji kata ya Iwawa Bw. Festo Msigwa akiongea na mwandishi wa Blogs za Mikoa

Blog za Mikoa kupitia Njombe yetu  haikuishia hapo imebisha hodi katika ofisi za kata ya Iwawa iliyoko katika mji mdogo wa Iwawa (Makete Mjini) na kukutana na afisa Mtendaji Bw. Festo Msigwa ambaye amekiri kuwa bado umilikishwaji au umiliki wa ardhi kwa wanawake ni mdogo kutokana na mila potofu 

Amesema katika kata yake zipo kesi za ardhi zinazoletwa katika ofisi yake zikiwemo za wanawake wajane kupokonywa umiliki wa ardhi kutoka kwa ndugu wa mume wake kwa madai kuwa yeye kama mwanamke hawezi kumiliki wala kuiendeleza jambo ambalo limepingwa na kulaaniwa vikali na mtendaji huyo

"Wanawake wanaweza kwanza katika shughuli za shambani wao ndio wachakarikaji kuliko sisi wanaume, fikiria kwa mfano hawa wajane wanaokuja kwenye kesi za ardhi katika baraza la ardhi hapa, unakuta wakati wa uhai wa waume zao wao ndio walikuwa walimaji wazuri na watunzaji wakubwa wa mashamba, sasa kama aliweza toka mwanzoni iweje sasa washindwe" amesema Msigwa

Machi 8 mwaka huu ni kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambapo kwa wilaya ya Makete maadhimisho yatafanyika katika kata ya Iwawa katika mji mdogo wa Iwawa
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa