Home » » TAKUKURU YABURUZA MAHAKAMANI VIONGOZI WA KIJIJI NJOMBE

TAKUKURU YABURUZA MAHAKAMANI VIONGOZI WA KIJIJI NJOMBE

Festus Pangani, Njombe Yetu
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU Wilayani Njombe jana imewafikisha mahakamani viongozi watatu wa Mtaa wa Wikichi Kata ya Ramadhani Akiwemo Afisa Mtendaji wa Kijiji Hicho Bw Zabron Mgeyekwa.
Akisoma Hati ya Mashtaka Mahakamani Hapo, Mwendesha Mashtaka wa TAKUKURU Wilayani Njombe Richard Marekani Amewataja Watuhumiwa Wengine Kwenye Kesi Hiyo Kuwa ni Pamoja na Willy Ngaro Aliekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Shule ya Msingi Wikichi na Emmanuel Mwalongo Aliekuwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Wikichi
Akifafanua Zaidi Mahakamani Hapo Mwendesha Mashtaka Huyo Ameiambia Mahakama Kuwa Mnamo Mwaka 2007 Kwa Pamoja Wakiwa ni viongozi wa kijiji waliwatoza wananchi wa kijiji hicho Michango ya Zaidi ya shilingi laki mbili Huku stakabadhi ya malipo Ikionesha Kuwa Michango Iliyochangwa ni Shilingi Elfu 38 Tu.
Kesi Hiyo iliahirishwa Hadi Agost 23 Baada ya Watuhumiwa Kukana kuhusika na Makosa Hayo na Hivyo Kurudishaw Mahabusu Baaada ya Kukosa Wadhamini.

Akizungumza Nje ya Mahakama Hiyo Mwendesha Mashtaka wa TAKUKURU Wilaya ya Njombe Richard Marekani Amesema Watuhumiwa hao Kwa Pamoja Wanatuhumiwa Kwenda Kinyume na Sheria ya Kupambana na Rushwa Namba 11 ya Mwaka 2007.
Katika Hatua Nyingine Taasisi ya Kuzuia n Kupambana na Rushwa TAKUKURU Wilayani Njombe imewataka Wananchi Kuendelea Kushirikiana na Taasisi Hiyo Katika KUwafichua na KUwataja Watu Wanojihusisha na vitendo Vya Rushwa Kama Njia ya Kusaidia Kupunguiza Tatizo la Rushwa Mkoani Hapa
Blogzamikoa

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa