Home » » WANANCHI NJOMBE WAHAMASISHWA KUWEKEZA KATIKA SOKO LA HISA

WANANCHI NJOMBE WAHAMASISHWA KUWEKEZA KATIKA SOKO LA HISA

Festus Pangani, Njombe yetu
BENKI ya wananchi Njombe (NJOCOBA) Mkoani Njombe, imehamasisha wananchi kununua hisa na kufanikiwa kuuza jumla ya hisa 55,000 zenye thamani ya sh. milioni 55, zilizofikisha jumla ya hisa 442,000 zenye thamani ya sh. milioni 442 katika kipindi cha mwaka 20111.

Akifafanua juu ya mtaji wa benki hiyo, Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi Bi. Twilumba Ulaya amesema, mapato katika benki hiyo kwa kipindi cha mwaka mwaka 2010/11 ilikuwa sh.bilioni 1.8 kwa akaunti zote.

Katika kipindi hicho mapato ya benki yalikuwa sh. milioni 554, ambapo faida ilikuwa sh.milioni 10, ingawa hasara ilikuwa sh. milioni 289 iliyotokana na gharama kubwa uendeshaji ambazo benki kuu iliamuru zihesabike kama manunuzi ya awali wakati benki hiyo inafunguliwa.

Hadi kufikia Desemba mwaka jana  benki hiyo imetoa mikopo ilikuwa imetoa mikopo yenye thamani ya sh. bilioni 3.6 urejeshaji wake umekuwa mbaya ambapo hadi wakati huo mikopo yenye thamani ya sh. milioni 267 sawa na silimia 18, haijarejeshwa. 

Blogzamikoa

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa