Home » » MBUNGE AWATAKA WANANCHI KUSHIRIKIANA

MBUNGE AWATAKA WANANCHI KUSHIRIKIANA

Festus Pangani, Njombe
Wito umetolewa kwa wananchi wa Mkoa wa Njombe kuungana katika kupambana na umasikini kwa kuanzisha miradi mbalmbali yenye manufaa kwao na taifa kwa ujumla.
Wito huo umetolewa na Mbunge wa Viti Maalumu vijana Mkoa wa Dar es Salaam Neema Mgaya wakati wa semina iliyotolewa kwa umoja wa wanawake UWAT mkoani humo iliyoandaliwa na Taasisi ya Povert Reduction in Tanzania PRT.
Mbunge huyo amesma kuwa kuanzishwa kwa taasisi hiyo mkoani Njombe itahamasisha maendeleo ikiwa vikundi vitaungana pamoja na kuunda nguvu ya pamoja kwa kukopeshana fedha za kufanya miradi mbalimbali.
Akizungumza katika semina hiyo Mkurugenzi wa Utawala na Fedha wa taasisi hiyo Ally Manjesi amesema, kuanzishwa kwa taasisi hiyo ni mwanzo wa harakati za kujikomboa kwa wananjombe.
Taasisi ya Povert Reduction in Tanzania PRT imeanzishwa mwezi julai mwaka huu na inakusudia kufanya kazi ndani ya mikoa ya Tanzania bara.
Blogzamikoa

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa