Mchezo wa Shuga wabadilisha tabia za vijana

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mratibu wa mradi wa Shuga akijibu maswali yaliyokua yanaulizwa na kikundi cha wasikilizaji cha Iwawa- Makete mkoani Njombe

Wakionyesha furaha zao baada ya kuelewa mada ya siku ukihusianisha na maisha yao ya kila siku

Mwezeshaji wa kikundi cha wasikilizaji wa Kihesa, Manispaa ya Iringa mjini akitimiza jukumu lake la kuelimisha wenzake na kuwawezesha kushiriki katika majadiliano baada ya kusikiliza kipindi

Vijana wa Iringa wakionyesha nyuso zenye furaha baada ya kuongeza uelewa kupitia majadiliano baada ya kipindi cha saba cha mfululizo wa vipindi vya Shuga


 Kikundi cha wasikilizaji kutoka kijiji cha Kabanga, Kyela wakifurahia uelewa walioupata juu ya kukabiliana na changamoto zinazowakumba katika maisha yao


Kikundi cha wasikilizaji Jitambue 1 kutoka wilaya ya Kyela mkoani Mbeya wakijadiliana sehemu ya saba ya mfululizo wa vipindi vya mchezo wa redio wa Shuga.

Wakina mama wakifuatilia mjadala kuhusu kujitambua na namna ya kujikinga na Virusi vya UKIMWI pamoja 


 Mwana kikundi wa AMKA- Njombe vijijini akiwashirikisha wanakikundi wenzie uzoefu wake katika kukabiliana na changamoto za kutakwa kimapenzi na wanaume waliomzidi umri

Mwanachama ambaye amekua baba katika umri wa miaka 19 akionyesha shukrani zake kwa vipindi vya Shuga kwa kumuwezesha kujitambua, kwenda kupima afya yake na kujiwekea malengo ya kujilinda yeye, mama pamoja na mtoto dhidi ya maambukizi ya VVU


Tunajitambua, Tunajipenda na Tunajilinda na VVU. Tumepima - Kikundi cha AMKA kutoka Njombe




UGONJWA  wa UKIMWI umekuwa janga kubwa sana duniani huku wadau mbalimbali wakiendelea kutoa elimu na kuhamasisha katika kuanzisha programu mbalimbali za kubadilisha tabia chanya kwa jamii.


Akizungumza mwishoni mwa wiki, Mratibu wa mchezo wa redio wa Shuga alisema  tayari wameanzisha programu mbalimbali za vipindi vinavyolenga kuelimisha jamii hususani  vijana juu ya  maambukizi ya Virusi vya ukosefu wa kinga mwilini (UKIMWI), usawa wa jinsia, kufanya maamuzi sahihi, matumizi sahihi ya kinga na kuepukana na msongo rika.

Alisema mfululizo huu wa mchezo wa redio wa Shuga unawalenga zaidi vijana hususan wasichana, kwa kuangalia mtazamo wao, matarajio  pamoja na changamoto wanazopitia kwa  njia sahihi za kukabiliana na changamoto ili kutimiza malengo yao. 

"Mchezo wa redio wa Shuga ulianzishwa mnamo mwaka 2014 kwa ushirikiano kati ya MTV, HIV and AIDS Free Generation, Shirika la TACAIDS pamoja na UNICEF. Baada ya mafanikio makubwa msimu wa kwanza, TACAIDS na UNICEF pamoja na wadau wengine waliamua kupanua wigo wa program hii kwa kuandaa vipindi zaidi ili kuimarisha tabia chanya zilizojengwa katika msimu wa kwanza wa vipindi vya Shuga," alisema Laizer 

Alisema mfululizo wa vipindi vya redio vya Shuga awamu ya pili vilianza kupitia redio mbalimbali nchini kuanzia wiki ya pili ya mwezi wa nne 2016 kwa lengo la kuendeleza elimu ya masula ya UKIMWI.

"Katika kuboresha utoaji elimu kuhusiana na maudhui ya vipindi, kampuni ya True Vision Production imefanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa awamu ya pili ya  mfululizo wa vipindi vya redio vya Shuga katika kuhakikisha jamii inakuwa na uelewa juu ya masuala hayo." alisema Laizer. "Kwa sasa, vituo mbalimbali vya redio vinarusha sehemu ya nane ya mfululizo wa vipindi vya Shuga." Aliongezea Laizer. 


Alisema Matokeo ya mradi huu yameanza kuonekana na vijana ambao ni walengwa wakuu wametoa ushuhuda wao kuhusiana na kipindi hicho cha Shuga na kusema kuwa klipindi kimewaletea mabadiliko makubwa.


‘Vijana tunajitambua, tumehamasika kwenda kupima afya zetu, tunajua njia sahihi za kujilinda na magonjwa ya zinaa na pia tunajiwekea mipango endelevu," alisema Abbas Boniphace, mmoja wa wasikilizaji wa kipindi cha Shuga kutoka Njombe

"Ningepata nafasi ya kusikia Shuga mapema nisingepata ujauzito katika umri mdogo. Sikua na uelewa wakati huo, sasa najitambua, nimepima na najilinda, siwezi kudanganyika" alisema Herieth kutoka Njombe.

"Wazazi huogopa kutuambia ukweli juu ya maswala yahusuyo VVU na UKIMWI ila Shuga inaelezea kwa uwazi zaidi." Alisema Shamila Juma, mwana kikundi cha wasikilizaji wa vipindi vya Shuga

UJUE KWA UNDANI MKOA WA NJOMBE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Njombe Region was established on 1st March 2012 by the Government Gazette No.9 under GN No.72. The region is located in Southern Highlands Zone which comprises of Ruvuma, Iringa, Mbeya, Njombe and part of Morogoro Regions. It borders Iringa Region in the North, Morogoro Region in the East and Ruvuma region in the South. It also borders Republic of Malawi via Lake Nyasa and part of Mbeya Region in the north-west and West. It lies between latitude 08o 40’ and 10o 32’ south of the equator and between longitude 33o 47’ and 35o 45’ east of Greenwich. 


The region is linked with neighbouring regions of Iringa, Mbeya, and Ruvuma by a tarmac road. These roads also link with Mozambique, Zambia and Malawi countries. Most of the roads within the region are in good condition and passable throughout the year. It is divided into four districts namely Njombe, Wanging’ombe, Makete and Ludewa. Also there are six Local Government Authorities namely Njombe and Makambako Town Councils, Njombe, Makete, Wanging’ombe and Ludewa District Councils. There are a total of 18 Divisions, 96 Wards, 384 Villages and 35 Mitaa 

The Regional climate is influenced by a number of factors which have led to the formation of three climatic zones namely, the Highlands Zone, the Midlands Zone and the Lowlands zones. The Highlands Zone lies at an altitude of 1,600 – 3,000 meters above sea level. This area includes Imalinyi in Wanging’ombe district, Lupembe in Njombe district, Mlangali, Liganga and part of Mawengi Division in Ludewa and Makete districts. Temperature is normally below 15o C with rainfall ranging from 1,000 to 1,600 mm per annum, falling in a single season from November through May, The dry and cold season occurs after the rain season, and it lasts from June to September.

The Midlands Zone lies between 700 – 1,700 meters above sea level. This area includes Ludewa and Njombe Town and Northern parts (Lupembe and Makambako) with rainfall ranges between 1,100 and 1,300mm and temperature are mild to cold falling to below 100C during June-July.

The lowland zone lies between 600 – 1,400 metres above sea level. This area includes Mdandu and Wanging’ombe Divisions in Wanging’ombe District, Masasi and Mwambao Divisions in Ludewa District and Mfumbi Ward in Makete District. Temperature is between 150C and 200C with rainfall ranging from 600 to 1000mm, with occasional mild droughts in 4 out of 5 years.

The variation in climatic conditions in terms of temperature and rainfall patterns offers investors opportunities to diversify their agricultural (e.g. horticulture) and livestock products (e.g. milk and wool) to take advantage of low seasonal supplies in other parts of Tanzania, East and Southern Africa and the world market in general.

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa