Home » » WAWILI MBARONI KWA KUKATAA KUHESABIWA MAKAMBAKO

WAWILI MBARONI KWA KUKATAA KUHESABIWA MAKAMBAKO

Festus Pangani, Njombe Yetu
Jeshi la Polisi Mkoani Njombe linawashikilia watu wawili Athuman Saidi Kivanga Mkazi wa Mtaa wa Kawawa Mji wa  Makambako na Yasini Shaibu wa Kijiji cha Kipagamo Kwa Tuhuma za Kukataa Kuhesabiwa.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani  Njombe ACP Fulgency  Ngonyani Amesema Watu Hao Wamekatwa Agosti 27 Mwaka Huu Majira ya Saa Tano Asubuhi Ambapo Watuhumiwa Hao Walikataa Kuhesabiwa Kwa Madai Kuwa Imani Zao Haziruhusu Kufanya Hivyo.
Kamanda Ngonyani Amesema Kitendo cha Kukataa Kuhesabiwa ni Kosa la Jinai na Kinyume cha Sheria na Kwamba Watuhumiwa Wamekamatwa Kwa Mahojiano Ikiwa ni Pamoja na Kuwaelimisha Juu ya Umuhimu wa Sensa na Endapo Watazidi Kukataa Watafikishwa Mahakamani.
Katika Tukio Jingine Kamanda Huyo Amesema Watu Wasiofahamika Wamevunja Nyumba ya Fredy Mtulua Mkazi wa Kijiji Cha Igagala Wilaya ya Wanging'ombe na Kuiba Pikipiki Moja Aina ya Skymark Yenye Namba za Usajili T 664 BNQ Yenye Thamani  Zaidi ya Shilingi Milioni Moja .
ACP Ngonyani Amesema Tukio Hili Limetokea Agosti 27 Mwaka Huu Majira ya Saa Nane Usiku na Hakuna Mtu Yoyote Aliyekamatwa Kuhusika na Tukio Hilo.
Hata Hivyo Jeshi La Polisi Mkoani Njombe Linaendelea na Upelelezi Juu ya Matukio Hayo Ambapo Amewataka Wananchi Kutoa Ushirikiano Kwa Kutoa Taarifa Kwenye Vyombo Vya Dola Ili Kuwabaini Watu Waliojihisisha na Vitendo Vya Uhalifu.
Blogzamikoa

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa