WAZIRI JAFO APONGEZA JITIHADA ZA MBUNGE WA MAKAMBAKO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo(Katikati) alipotembelea Hospital ya Mji wa Makambako.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo akisalimia na Muuguzi wa Hospital ya Mji wa Makambako alipotembelea Hospital hiyo kukagua utoaji wa uduma za Afya
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Njombe Mhe.Lucy Msafiri wakati wa ziara yake katika Hospital ya Mji wa Makambako.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo katika Picha ya pamoja na viongozi wa Wilaya pamoja na watumishi wa Hospital ya Mji wa Makambako.
Huu ndio Muonekano wa Hospital ya Makambako unavyoonekana kwa hivi sasa



Nteghenjwa Hosseah,Makambako.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo amempongeza Mbunge wa Makambako Mhe. Deo Sanga kwa jitihada mbalimbali anazozifanya katika kuboresha Sekta ya Afya katika Jimbo hilo.

Jafo ameyasema hayo wakati alipotembelea Hospital ya Mji wa Makambako na kuona vyumba viwili vya Madaktari ambavyo vimejengwa na Mbunge Mhe. Sanga.

“Kwa dhati kabisa nimpongeze Mhe. Sanga kwa kujitoa kuboresha huduma za Jamiia hii inaonyesha nia yake njema katika kuwaletea wananchi maendeleo kwa sabababu wananchi wakiwa na Afya Njema wataweza kuendelea na shughuli zao kikamilifu za kujitaftia kipato kisha kupata maendeleo” Alisema Jafo

Kwa kutambua Idadi kubwa ya watu wanaopata huduma katika Hospital hiyo ambayo ina miundombinu Duni ikiwa ni pamoja na ukosefu wa Jengo la kisasa la Kuhifadhia Maiti pamoja na Ukosefu wa wodi mbalimbali.Waziri Jafo amesema Serikali itaangalia jinsi ya kuboresha miundombuni hiyo ili wakazi wa Makambako waweze kupata huduma bora za Afya kama Watanzania wanazopata wengine.

“Tutaweka Jitihada katika kutafuta Fedha kutoka kwenye vyanzo vyetu Ili kuongeza miundombinu ya Afya na hospital hii iweze kuwa na hadhi ya kuwa na Hospital ya Mji” Alisema Jafo.Hata hivyo Jafo amechukua kilio cha Hospital hiyo kuendelea kupata mgao wa Kituo cha Afya wakati imeshapandishwa hadhi kuwa Hospital ya Mji ana ameahidi kulishughulikia.

“Makambako ni eneo muhimu sana katika Kanda hii yenye wakazi wengi, shughuli nyingi za kiuchumi na muingiliano wa watu wengi kutoka ndani na nje ya Nchi hivyo inahitaji huduma bora zaidi za Afya kwa kwa kuzingatia umuhimu wa eneo na wananchi wake” alisema Jafo.

Waziri Jafo anaendelea na ziara yake katika Mikoa Mbalimbali lengo ni ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo iki chini ya Ofisi ya Rais Tamisemi.

MBUNGE:WAJASIRIAMALI ANZENI KUSAFIRISHA CHIPS

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mbunge wa Njombe Mjini, amewataka wajasiriamali wadogo mkoani Njombe kuwekeza kwenye viwanda vidogo vidogo na kuanza kusafirisha viazi ambavyo tayari vimecharagwa chips ili kuepuka kulaliwa na wafanyabiashara wanaolazimisha kufunga lumbesa za viazi.

Edward Mwalongo amesema hayo akiwa anaongea na baadhi ya wajasiriamali mkoani humo ambao wameanzisha kiwanda kidogo cha kumenya viazi na kucharanga chips na kudai kuwa wana Njombe wanapaswa kuvitumia viazi kama malighafi yao ambayo inaweza kuwaletea viwanda vingi vidogo vidogo.

"Viazi ni sehemu ya malighafi ambavyo tungeweza kuvitumia kama hivi na huo ndiyo mwanzo tuitumie malighafi ya viazi ili kusudi tuanzishe viwanda vidogo vidogo vingi kadri inavyowezekana, kwa sababu kila kiazi kinachotoka Njombe kikisafirishwa hakipelekwi kwa ajili ya mbegu bali kinakwenda kuliwa na kama kinakwenda kuliwa kinaliwa kama chips au kinakwenda kumenywa lakini sehemu kubwa inajulikana vinakwenda kuliwa kama chips sasa tufike mahala wana Njombe badala ya kulalamika na Lumbesa tuanze kusafirisha chips zilizomenywa kwa kuweka kwenye ubaridi na ziwafikie walaji" alisisitiza

Mbunge huyo wa Njombe Mjini aliwakabidhi mashine ya kukatia viazi wanawake wajasiriamali ambao wameunda kikundi chao na kuanza kufanya kazi hiyo ya kukata chips na kuziuza kwenye mahoteli, migahawa na wapishi wa chips mkoani humo.

MBUNGE MGAYA AWASAIDIA WANAWAKE VYEREHANI 370 NJOMBE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Njombe Neema Mgaya (katikati mstari wa mbele) akiwa na baadhi ya wanawake aliowakabidhi vyerehani 370 vyenye thamani zaidi ya Shilingi Milioni 90 Halmashauri ya Makambako Mkoani Njombe ili wajikwamue kiuchumi.
Mbunge wa Viti Maalum CCM mkoa wa Njombe, Neema Mgaya (mbele) akiwa na baadhi ya wanawake aliowakabidhi vyerehani 370 vyenye thamani zaidi ya Shilingi Milioni 90 Halmashauri ya Makambako Mkoani Njombe ili wajikwamue kiuchumi.
Baadhi ya vyerehani 370 vyenye thamani zaidi ya Shilingi Milioni 90 vilivyolewa na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Njombe, Neema Mgaya vikiwa tayari kukabidhiwa kwa baadhi ya wanawake wa Mkoa wa Njombe ili wajikwamue kiuchumi. 

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Njombe, Neema Mgaya ametoa msaada wa vyerehani 370 vyenye thamani zaidi ya Milioni 90 kwa wanawake mkoani humo ili wajikwamue kiuchumi huku akiunga mkono juhudi za Serikali inayohimiza uchumi wa viwanda. Akizungumza Mjini Makambako wakati wa hafla ya kukabidhi vyerehani hivyo kwa baadhi ya wanawake, Mgaya amesema amefikia uamuzi huo ili kuunga mkono juhudi za Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuifanya Tanzania kuwa taifa la uchumi wa kati kupitia viwanda. Akibainisha zaidi ameeleza juhudi za kumkomboa mwanamke wa mkoa wa Njombe ni jambo linalopiganiwa kwa miaka mingi hivyo vyerehani hivyo vitawafungulia njia kuweza kujikwamua kiuchumi.

“Nimekuwa sina papara katika utendaji wangu, mwaka jana nilitoa msaada wa vitabu vya ziada kwa Shule za Sekondari Halmashauri ya Makambako, ambapo kwa mwaka huu nimeamua kuunga mkono juhudi za serikali upande wa viwanda kwa kuwasadia wanawake hawa vyerehani hivi 370,” alisema Mgaya.

Akifafanua amesema anatambua thamani kubwa walionayo wanawake hivyo kwa kuwawezesha vyerehani hivyo kutainua familia na jamii zinazowazunguka kwani fedha zitakazopatikana zitasaidia huduma za kijamii na mahitaji mengine.

“Mtu ninayemthamini huwa nampa kitu ambacho kitadumu na kumsaidia kwa muda mrefu, mimi nimeamua kutowapa samaki kwani mtamla ataisha, nimewapa nyavu ambayo mtaitumia kuvua samaki, nendeni mkavitunze vyerehani hivi kujiletea maendeleo endelevu,” alisema Mgaya.

Akizungumza baada ya kupokea cherehani yake Diwani wa Viti Maalum Lupembe Neema Limbanga amesema alilolifanya Mbunge huyo wa Viti Maalum halijawahi kutokea katika maisha yake na kwamba vyerehani hivyo vimewafungulia njia kimaisha.

Naye Diwani wa Viti Maalum CCM Njombe, Stella Francis amesema Mgaya amewapa zawadi ambayo licha ya kuwainua kiuchumi itakuwa mkombozi hasa katika ndoa zao, kwani sasa wataweza kuhudumia familia kwa kushirikiana na wanaume zao.

Kutolewa kwa vyerehani hivyo 370 ambavyo ni sawa na viwanda vidogo 92 kwa dhana ya vyerehani vinne sawa na kiwanda kimoja kidogo kunaufanya mkoa wa Njombe kuitikia vilivyo wito wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuhamasisha uchumi wa viwanda. Lengo la Mkoa kupitia wanawake ni kuwa na viwanda vidogo 35 hivyo kwa vyerehani  370 ambavyo Neema amevitoa ni kwamba lengo la kimkoa kupitia wanawake limeshafikiwa.

WAKULIMA 206 WAPATA MAFUNZO YA KILIMO CHA CHAI KUTOKA NOSC

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji mkoa wa Njombe Bwana Lameck Noah(wapili kushoto) akikabidhi cheti bwana Thiemo Msewa(kulia) katika hafla ya kufunga mafunzo kwa wakulima wa chai(farmer field school) mkoani humo yaliyoratibiwa na Kampuni ya kuhudumia wakulima wadogo Njombe(NOSC). Mafunzo hayo yalilenga kuwajengea uwezo wakulima katika kilimo cha chai na mazao mengine. Wapili kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa NOSC, Bwana Filbert Kavia. Watatu kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bi.Ruth Msafiri 
Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji mkoa wa Njombe Bwana Lameck Noah akizungumza jambo wakati wa hafla hafla ya kufunga mafunzo kwa wakulima wa chai(farmer field school) mkoani humo yaliyoratibiwa na Kampuni ya kuhudumia wakulima wadogo Njombe(NOSC). Mafunzo hayo yalilenga kuwajengea uwezo wakulima katika kilimo cha chai na mazao mengine. 
Operation Director wa Wood foundation Tanzania Bwana Mathew Ng’enda(watatu kushoto) akishangilia mara baada ya wakulima kuwasilisha mada mbalimbali juu ya elimu ya kilimo cha chai (farmer field school) waliyoipata kutoka Kampuni ya kuhudumia wakulima wadogo Njombe(NOSC). Kulia ni Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji mkoa wa Njombe Bwana Lameck Noah. na watatu kulia ni Mkurugenzi mkuu wa NOSC Bwana Filbert Kavia. 

KUTOKANA na ushirikishwaji wa wakulima wadogo katika zao la chai kupitia Kampuni ya Kuhudumia Wakulima Wadogo Njombe (NOSC), viongozi wa Mkoa wa Njombe wanajivunia mafanikio yaliyopatikana katika kilimo cha chai kilichosaidia kuinua kipato cha wakulima wadogo na kuongeza fedha za kigeni.

Hayo yamesemwa na Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Njombe, Bwana Lameck Noah kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo Bw. Christopher Ole Sendeka mkoani hapa jana katika mahafali ya mwaka mmoja kuhusiana na mafunzo ya kilimo cha chai kilichohusisha wakulima zaidi ya 206.

“Katika mkoa wetu tulijiwekea utaratibu kuwa kila mkulima alime mazao ya aina mbili ya chakula na biashara, kwa upande wa chai tatizo lilikuwa ni aina ya miche, ilikua inachukua muda mrefu kukua lakini tunaishukuru NOSC imetuletea mice inayokua kwa miezi 12 mkulima anaanza kupata majani mabichi ya chai,” alisema Bw. Noah.

Alibainisha kuwa elimu hiyo ina maana kubwa kwa mkoa wake kwa sababu itawasaidia kulima kisasa na kuwaongezea kipato wananchi wa mkoa huo, lakini pia viwanda vitapata malighafi hiyo muhimu kwa ajili ya soko la ndani na nje.

“Tunafahamu chai inapendwa na mataifa ya magharibi, zao hili lina fedha nyingi za kigeni. Soko la chai lipo na tunawahakikishia wakulima serikali inahangaika kupata mnada wa chai katika ukanda huu badala ya kufanyika Mombasa nchini Kenya.

JUKWAA LA HAKI JINAI LATEMBELEA MAGEREZA NA VITUO VYA POLISI IRINGA,NJOMBE NA RUVUMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

 Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka akiongea na wataalamu wa Jukwaa la haki jinai nchini ambao walioongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof Sifuni Mchome  walipoanza ziara ya kutembelea magereza na vituo vya polisi mkoani humo.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Amina Masenza akiwakaribisha ofisini kwake  wataalamu wa Jukwaa la
haki jinai nchini ambao walioongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof Sifuni Mchome mjini Iringa walipoanza ziara ya kutembelea magereza na vituo vya polisi mkoani humo juzi.

 Wataalamu kutoka taasisi zinazosimamia utoaji haki nhini ikiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof Sifuni Mchome wa pili kulia waliosimama mbele wakiwa na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka wapili kushoto waliosimama mbele Wataalamu hao walikwenda kumsalimia Mkuu wa Mkoa  wa Njombe kabla ya na kutembelea gereza la wilaya ya Njombe na kituo cha Polisi cha wilaya hiyo na kuzungumza na wafungwa na mahabusu walioko kizuizini katika maeneo yao na kutatua changamoto zinazowakabili.
 Timu ya wataalamu kutoka Jukwaa la Haki Jinai nchini ikiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof. SifuniMchome katika picha ya pamoja na askari magereza nje ya gereza la wilaya ya njombe baada ya kutembelea gereza hilo na kuzaungumza na wafungwa na mahabusu walioko katika gereza hilo mjini Njombe jana
ilikujionea changamoto zinazowakabili  wafungwa na mahabusu nchini katika kupata haki zao wakiwa vizuizini au magerezani na kuangalia namna ya kuzitatua.
 Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Amina Masenza (katikati waliosimama mbele) katika picha ya poamoja na wataalamu wa Jukwaa la haki jinai nchini ambao walioongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof Sifuni Mchome baada ya kutoka kumsalimia Mkuu huyo wa mkoa Ofisini kwake mjini Iringa walipoanza ziara ya kutembelea magereza na vituo vya polisi mkoani humo juzi.

Timu ya wataalamu kutoka Jukwaa la Haki Jinai nchini ikiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome inatembelea Magereza katika mikoa ya Iringa, Njombe  na Ruvuma ili kujionea changamoto zinazowakabili  wafungwa na mahabusu nchini katika kupata haki zao wakiwa vizuizini au magerezani na kuangalia namna ya kuzitatua. 
Akizungumza katika siku ya kwanza ya ziara hiyo mjini Iringa, Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof.Mchome amesema utekelezaji wa mradi huo pia unalenga kuziongezea  uwezo taasisi zinazoshughulika na utoaji haki na kusimamia haki za binadamu nchini ili ziweze kutoa huduma stahiki kwa watanzania ya utoaji haki na ulinzi wa haki za binadamu. 
Amesema ni matarajio ya Serikali kuwa ziara hiyo itawezesha taasisi zinazosimamia utoaji haki nchini kuchukua hatua katika kuhakikisha wafungwa na mahabusu wanapata haki zao kwa wakati.

Ujumbe huo wa jukwaa  la haki jinai unamshirikisha Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP) Biswalo Mganga, Naibu Mkurugenzi Upelelezi Makosa ya Jinai nchini (DDCI) Charles Kenyela, Ofisi ya Msajili wa Mahakama ya Tanzania, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Magereza na Jeshi Polisi.

Ujumbe huo umetembelea Gereza la wilaya ya Iringa,  Selo iliyoko katika kituo cha Polisi Iringa mjini, Gereza la Wilaya Njombe na selo iliyoko katika kituo cha Polisi Njombe na kujionea mazingira yaliyopo na kusikiliza kero zinazowakabili wafungwa na mahabusu walioko katika vituo hivyo vya polisi na magereza hayo katika kupata haki zao. 

Wananchi hao waliomba kupata msaada katika maeneo ya kufikishwa mahakamani kwa wakati, uchunguzi wa tuhuma zinazowakabili kufanywa kwa wakati, kupatiwa nakala za hukumu kwa wakati   ili wawahi muda wa kukata rufaa na mashitaka yao kusikilizwa kwa wakati ikiwa ni pamoja na kusikilizwa kwa rufaa zao. 
Ziara hiyo ni utekelezaji wa mradi wa upatikanaji haki na ulinzi wa haki za binadamu nchini unaoendeshwa kwa pamoja kati ya Serikali ya Tanzania na Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa –UNDP.

TAMASHA LA TIGO FIESTA LAACHA GUMZO MKOANI NJOMBE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Wasanii wa kizazi kipya wa kundi la Rostam wakiwa kwenye staili ya aina yake kwenye jukwaa la tamasha la  Tigo Fiesta lililofanyika uwanja wa sabasaba mjini Njombe usiku wa kuamkia jumamosi.

Msanii Ommy Dimpoz akitoa burudani kwenye jukwaa la tamasha la Tigo Fiesta lililofanyika  uwanja wa sabasaba mjini Njombe usiku wa kuamkia jumamosi.

Aslay akiimba kwa hisia mapema wiki iliyopita katika jukwaa la Tigo Fiesta Mkoani Njombe



Wasanii Jux, Nandy, Ben Pol na Maua Sama walipanda pamoja na kuimba  nyimbo zao mbalimbali kwenye tamasha la Tigo Fiesta lililofanyika uwanja wa sabasaba mjini Njombe usiku wa kuamkia jumamosi.

Mr blue akiwapagawisha wakaziwa mkoa wa Njombe mapema wiki iliyopita.

Chege Chigunda akitumbuiza na madansa wake

Darasa akiburudisha wakazi wa Mkoa wa Njombe mapema wiki iliyopita.




Squeezer akiburudisha umati wa wakazi wa Njombe waliojitokeza katika Tamasha la Tigo Fiesta wiki iliyopita

Vanesa Mdee akiwa katika jukwaaa la Tigo Fiesta Mkoani Njombe usiku wa kuamkia jumamosi.

NENO LA UKARIBISHO KUTOKA KWA MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA NJOMBE MJI MH. EDWIN MWANZINGA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Mhe.. Edwin Mwanzinga
Mwenyekiti wa Halmashauri
Kwa niaba ya Watumishi na Wananchi wote wa Halmashauri ya Mji Njombe ninayofuraha kubwa  kukukaribisha katika tovuti hii ambako tunaimani kubwa utapata taarifa za kuaminika na shughuli zinazofanyika katika Halmashauri ya Mji Njombe.Kama taasisi ya Serikali tunaamini katika uwazi,ukweli na uwajibikaji kwenye utendaji wetu wa kila siku.
Aidha kwa kutambua umuhimu wa wateja  tunaowahudumia zipo taarifa na fomu mbalimbali ambazo zinakuwezesha kupata huduma moja kwa moja kwenye tovuti.
Hii inahusisha upatikanaji wa leseni za biashara na leseni za vileo na taarifa mbalimbali.Ni matumaini yangu utatumia tovuti hii kupata taarifa muhimu na kwa malalamiko,mapendekezo basi usisite kuwasiliana nasi na kutumia tovuti yetu kutoa malalamiko yako nasi tutakufikia.
Karibu Halmashauri ya Mji Njombe,Mji wenye fursa za maendeleo kwako na kwa Taifa

KARIBU SANA,

TARSIER: MNYAMA MWILI MDOGO, MACHO MAKUBWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

WATU wengi husema kwamba mnyama huyu ana sura nzuri; hata hivyo wengine husema kwamba ana sura ya ajabu. Ana miguu myembamba, manyoya laini, na macho makubwa yanayong’aa. Pia, ana urefu wa sentimita 12.5 na uzito wa gramu 114. Ni mnyama gani huyo? Anaitwa tarsier! 

Acheni tumchunguze tarsier wa Ufilipino. Kwa sababu ana mwili mdogo sana—macho yake, masikio, mikono, miguu na mkia huonekana mikubwa sana. Hata hivyo, ukimchunguza kwa makini utagundua jinsi alivyoumbwa kwa njia ya pekee sana.

UWEZO WA KUSIKIA: Masikio yake membamba kama karatasi yanaweza kujikunja na kujikunjua, na hata kunasa sauti ndogo kabisa. Uwezo huo wa kusikia humsaidia aepuke wanyama hatari na kujua mawindo yake yalipo. 

Usiku, masikio ya mnyama huyu yanamwezesha kusikia milio ya nyenje, mchwa, mbawakawa, ndege, na vyura. Anaposikia mlio wa windo lake yeye huelekeza kichwa mahali hapo akiwa amekodoa macho yake makubwa.

UWEZO WA KUSHIKA: Mikono ya tarsier ina uwezo wa pekee wa kushika matawi membamba. Ncha za vidole vyake zina miinuko kama ile ya gurudumu la gari inayomsaidia kukamata vizuri. 

Hata anapokuwa amelala, mnyama huyu anahitaji kujishikilia kwa nguvu. Miinuko iliyo kwenye sehemu ya chini ya mkia wake mrefu humsaidia asianguke anapokuwa amelala.

UWEZO WA KUONA: Hakuna mnyama mwingine mwenye mwili mdogo na macho makubwa kama mnyama huyu. Isitoshe, jicho lake moja tu ni kubwa kuliko ubongo wake! 

Macho yake hayazunguki; sikuzote hutazama mbele tu. Je, hilo ni tatizo? Hapana. Kwa sababu mnyama huyo anaweza kugeuza shingo yake pande zote kufikia nyuzi 180.

WEPESI: Miguu mirefu ya tarsier inaweza kumsaidia kuruka kufikia umbali wa mita 6. Umbali huo ni zaidi ya mara 40 ya mwili wake! Mnyama huyu mdogo huwinda usiku akitumia vidole vyake kukamata mawindo yake bila kukosea.

Wanyama hawa hawawezi kuishi muda mrefu wakiwa wamefungiwa, kwa sababu wanapenda sana kula wadudu walio hai na pia hawapendi kuguswa. Licha ya hilo, mnyama huyu wa ajabu huwavutia sana watu wa Ufilipino. Karibu kila sehemu ya mwili wa mnyama huyu wa msituni inastaajabisha kwelikweli!

Kumlinda Tarsier

Mwaka wa 1997, Serikali ya Ufilipino ilitangaza kwamba tarsier wa Ufilipino ni mnyama anayepaswa kulindwa. Kwa hiyo ni kosa kumwinda, kuharibu mazingira yake, au hata kumfuga. Mnyama huyu anapendwa sana na Wafilipino na yeye ni alama ya utalii nchini humo.-(Kwa msaada wa Mtandao).
Chanzo:Nipashe

AFYABANDO KAMPENI KUWAKOMBOA WATANZANIA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mtaalam Mwelekezi wa Afyabando-Nordic Foundation Tanzania, Dkt. Respicius Salvatory akiongea na waandishi wa habari Dar es Salaam leo Septemba 3 2017, wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya kujishindia kadi ya bima ya Afya ijulikanayo kama ‘AfyaBando’. Kulia ni Afisa Mwandamizi Mipango na Utawala wa Taasisi ya Nordic, Maria Nimrod na Afisa Tehama wa Taasisi hiyo, Dickson Leonard.

Afisa Mwandamizi Mipango na Utawala wa Taasisi ya Nordic, Maria Nimrod akifafanua jambo kwa waandishi wa habari Dar es Salaam leo wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya kujishindia kadi ya bima ya Afya ijulikanayo kama ‘AfyaBando’. Pamoja naye ni Mtaalam Mwelekezi wa Afyabando-Nordic Foundation Tanzania, Dkt. Respicius Salvatory (wa pili kulia) , Afisa Tehama wa Taasis hiyo, Dicson Leonard Afisa Afya na Teddy Uledi.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

MAKALA MICHEZO: BUSWITA NA OBI KOSA MOJA ADHABU TOFAUTI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.



Na Honorius Mpangala

Ilikuwa ni mwaka 2006 klabu ya Manchester United ilipofanya ujanja kumsainisha John Michael Nchekwube Obinna. Obi kama anavyojulikana na wengi akiwa klabu ya FK Lyn ya Norway alijikuta akiingia tamaa ya kuvaa jezi ya United na kuingia mkataba wa awali bila wakala wake na klabu yake kujua.

Akili aliyoitumia Obi ni ya wachezaji wetu wa kiafrika ambao wana teswa na ile methali "tamaa mbele mauti nyuma".Akiwa mzaliwa wa mji wa Jos katikati ya Nigeria alianza safari yake ya soka katika klabu ya hapo nyumbani kwao ya Plateau United.

Akiwa Norway Obi alipotea ghafla katika klabu yake na kusemekana kuwa ametekwa. Kumbe iligundulika alikuwa na Watu wa Manchester United ndipo alifanya 'uswahili' wa kusaini kandarasi ya kuitumikia United. Baadae picha zikasambaa kwenye mitandao akiwa na jezi ya United.
Kwa mapungufu yaliyofanywa na United iliwafanya Chelsea,kupita njia halali ya kumsajili. Uhalali na uwazi walioutumia Chelsea ukaonekana kuwa Manchester walimlazimisha Obi na kutokana na ukubwa wa klabu yao alijikuta anashindwa kukataa kuichezea klabu yao.
Baada ya sakata kufikishwa mbele ya Uefa maamuzi yanatolewa kuwa Manchester United walimsajili Obi kwa njia zisizo sahihi. Hawakumtumia wakala wake walimteka kijana wa watu lakini katika mazingira ambayo hata klabu yake inasemekana walijua ila hawakutaka kuwa wawazi. Maamuzi yalimnufaisha Chelsea na hatimaye Obi mwenyewe kwa kinywa chake akasema nataka kucheza Chelsea na sio Manchester United. Akakazia kuwa huko nilisaini kwa kushinikizwa.

HAKIMU MAKETE: ACHENI KUWALAUMU POLISI WANAPOTOA DHAMANA KWA WATUHUMIWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na Edwin Moshi

Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Makete Mjini ameitaka jamii kuacha kutupa lawama kwa polisi ama Mahakama pale Mtuhumiwa anapoachiwa kwa dhamana

Ameyasema hayo hivi karibuni katia kikao Maalum cha timu ya ulinzi na usalama wa Mtoto kilichoketi katika Ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Makete kujadili mambo mbalimbali Kuhusu Watoto

"Kama kuna mahali unapoona huridhiki na kupewa dhamana mtuhumiwa, nenda polisi ukaulize, na kama ni mahakamani nenda mahakamani ukaulize na sio kuwalaumu polisi au mahakama mitaani" amesema hakimu huyo

Zaidi Tazama video hii hapa chini:-

WATANZANIA TUUNGE MKONO JUHUDI ZA RAIS MAGUFULI KWA VITENDO.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
Na Agness Moshi - MAELEZO.
 
Tukielekea miaka miwili tangu kuapishwa kwa Rais John Pombe Magufuli kuwa Rais wa Awamu Ya Tano wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania ni wajibu wa kila Mtanzania mwenye kiu ya maendeleo na mzalendo kwa nchi yake kuunga mkono juhudi za Rais ili kuifikia Tanzania ya uchumi wa kati ifikapo mwaka  2025.
 
Nakumbuka hotuba yake ya kwanza baada ya kula kiapo cha kulitumikia Taifa hili  aliyoitoa katika shughuli za kuapishwa uwanja wa Uhuru jijini Dar Es Salaam, Novemba 5, mwaka  2015 ambayo ilibeba maneno yenye busara, hekima na yenye hamasa ya  kuleta maendeleo ya nchi yetu.
 
“Nchi yetu ni kubwa kuliko vyama vyetu vya siasa, mapenzi yetu na matakwa yetu.Uchaguzi Mkuu sasa umekwisha sote tushikamane kama watu wa Taifa moja kuijenga nchi yetu kwa kuweka itikadi na vyama vyetu pembeni”,alisema Rais Magufuli.
 
Ni wazi maendeleo ya nchi hayana dini, kabila, itikadi au chama bali yana undugu na uzalendo, ushirikiano, umoja, kufanya kazi kwa bidii na amani baina ya wananchi na serikali kwa ujumla.
 
Hivyo basi, tunawajibu wa kushikamana kama watoto wa baba mmoja na kufanya kazi kwa bidii na kuunga mkono juhudi  za Rais  Magufuli kwa vitendo ili tuweze kuifikisha Nchi kwenye uchumi wa kati utakaotuwezesha kupambana na maadui wakubwa watatu ambao ni Maradhi, Ujinga na Umaskini badala ya kukaa vijiweni kujadili mambo yasiyo na tija kwa  maendeleo yetu.
 
Aidha, hivi karibuni tumeshuhudia Taasisi, Mashirika,Viongozi mbalimbali wa dini na serikali  na watu mbalimbali wakituma salamu za pongezi kwa Rais Magufuli kwa juhudi na utendaji kazi wake. Lakini je?,tumewahi kujiuliza pongezi hizi na za maneno tu au wanashiriki kwa vitendo?
 
Sina maana kuwa, kumpongeza Rais ni vibaya au uovu,ni jambo jema lakini ingekua vyema zaidi kama pongezi zingeambatana na vitendo  kwani  “maneno bila vitendo si kitu” ndio maana Serikali  Awamu Ya Tano inaongozwa na  kaulimbiu  ya “HAPA KAZI TU” kwa lengo la kuhamasisha Watanzania kufanyakazi kwa  bidiii badala ya kusubiri serikali kuwafanyia kila kitu.Kauli mbiu hii imekua ikitumika pia nchi mbalimbali duniani ili kuhamasishana katika kufanyakazi na kujiletea maendeleo.
 
Maneno ya Rais Magufuli alipohutubia Bunge la Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania kwa mara ya Kwanza yanaishi na kutekelezwa kwa vitendo katika Serikali ya Awamu ya Tano hadi  kwa wananchi wenye kupenda maendeleo .
 
“Kila mmoja wetu afanye kazi, awe shambani, ofisini, kiwandani, sokoni, kwenye bustani na kadhalika badala ya kupoteza muda vijiweni”, alisema Rais Magufuli.
Ni wazi kuwa , Rais Magufuli amekuwa kiongozi  anayeisimamia na kutekeleza kauli mbiu ya Serikali yake kikamilifu tangu aingie  madarakani kwa  kuwajibika ipasavyo katika kuhakikisha utekelezaji wa  miradi mbalimbali ambayo imekua na manufaa makubwa kwa wananchi na Serikali kwa ujumla.
 
Hivi karibuni,  tumeshudia Mradi  wa ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda mpaka kwenye bandari ya Tanga kwasababu  ni  moja ya mradi mkubwa ambao nchi imetekeleza na utakaobadilisha maisha ya watanzania takribani elfu 30 kwa wakati mmoja. Pia, kuinufaisha Serikali kupitia kodi na utengenezaji wa ajira kwa wananchi wake.
 
Ipo miradi midogo ambayo imetekelezwa na tumeona , ikiwa ni pamoja na ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami, mfano barabara ya Msata-Bagamoyo na  Kagoma-Biharamuro-Lusahunga na  mabadiliko kwenye sekta ya afya ambayo yamekua msaada mkubwa katika  kubadilisha maisha ya watanzania na kuifanikisha safari ya nchi kuelekea uchumi wa kati na ujenzi wa Tanzania ya viwanda.
 
Kama Serikali iliahidi na imetekeleza, yatupasa kuhakikisha tunafanya kazi kwa biidi kwenye miradi hiyo na kuhakisha tunailinda ili isiharibike kwa namna yoyote badala ya kutoa pongezi za maneno matupu.
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa