Home » » WANANCHI LUDENDE WALIA UKOSEFU WAHUDUMU WA AFYA.

WANANCHI LUDENDE WALIA UKOSEFU WAHUDUMU WA AFYA.


Festus Pangani, Njombe Yetu Blog
Wananchi wa Kata ya Ludende wilayani Ludewa katika Mkoa wa Njombe wameulalamikia uongozi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo kwa kushindwa kupeleka wahudumu wa afya katika Zahanati Ludende hali inayosababisha adha kubwa kwa wakazi wa kata hiyo.
Pamoja na Zahanati hiyo kufunguliwa wakati wa maadhimisho ya miaka hamsini ya uhuru wa Tanzania mwaka jana lakini hakuna mfanyakazi hata mmoja na kwamba majengo ya zahanati hiyo ikiwa ni pamoja na nyumba ya mganga mkuu vimetelekezwa.
Akiongea kwa sharti la kutotajwa jina lake, mmoja wa wananchi hao alisema kuwa haoni sababu ya kuwa na majengo mazuri yaliyojengwa kwa kodi ya wananchi bila ya kuwepo wahudumu wa afya huku wananchi wakiendelea kuumia.
Mtendaji wa Kata ya Ludende, Lezile Luoga alikiri kutokuwepo kwa mfanyakazi yeyote katika Zahanati hiyo na mpaka sasa hakuna maelezo ya kina yanayohusu upatikanaji wa wafanyakazi katika Zahanati hiyo.
Luoga alisema wananchi wamekuwa wakijitolea kufanya maendeleo ya ujenzi wa Zahanati hiyo cha kushangaza wamekuwa wakipata huduma za matibabu katika Zahanati za vijiji vya mbali wakati dhahanati yao iko katika ubora unaokubalika.
“Tumewahamasisha wananchi kuchangia ujenzi wa zahanati hii hadi imekamilika lakini cha kushangaza Serikali imeshindwa kuleta wafanyakazi, hii inakatisha tamaa na wananchi wanaweza wasijitolee kufanya kazi za kimaendeleo” alisema Luoga.
Naye Makamu Mkuu wa shule ya Sekondari Ikovo, Menrufu Mgaya alisema ukosefu wa huduma ya afya umeleta usumbufu kwa wanafunzi wa shule yake hasa pale yanapotokea magonjwa ya milipuko yanayowakumba wanafuzi kutokana na ukosefu wa maji safi na salama.
Blogzamikoa

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa