Home » » WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII WATOA ELIMU YA KUPAMBANA NA UKATILI NA UNYANYASAJI KWA WATOTO WILAYANI MAKETE‏

WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII WATOA ELIMU YA KUPAMBANA NA UKATILI NA UNYANYASAJI KWA WATOTO WILAYANI MAKETE‏





 Miongoni mwa vitendo vinavyoshamiri Makete vya watoto kujihusisha na biashara ya kuuza mkaa


 Hapa watoto hao wakiandaa mkaa kwa ajili ya kuuza kwa wateja wao


 Mkaa ukisubiri wateja.

-------


Na Edwin Moshi

Mafunzo ya ulinzi na usalama wa mtoto dhidi ya ukatili na unyanyasaji yaliyoanza jana wilayani Makete mkoani Njombe yanaendelea katika ukumbi wa Sumasesu Tandala



Mafunzo hayo yaliyofunguliwa na Afisa Ustawi wa Jamii wilaya ya Makete Bw. Leonce Panga yameshirikisha wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa dini, dawati la jinsia kutoka kituo cha polisi Makete, maafisa elimu, mwanasheria, magereza, wauguzi, madaktari pamoja na hakimu mfawidhi wa wilaya ya Makete



Katika mafunzo hayo yanayowezeshwa na Bi Asha Mbaruku pamoja na Ramadhani Yahaya kutoka  ustawi wa jamii makao makuu jijini Dar es Salaam wamesema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wadau hao namna ya kuwahudumia watoto wanaokuwa wamefika kwenye ofisi zao kupata msaada endapo anakuwa amepata tatizo akitolea mfano kufukuzwa shule kwa kukosa ada


HABARI KAMILI BOFYA HAPA


0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa