Home » » Walalamikia mchango mdogo

Walalamikia mchango mdogo

Njombe.Uchangiaji mdogo wa halmashauri katika sekta ya afya kutoka kwenye vyanzo vyake vya ndani, umeelezwa kuwa miongoni mwa changamoto zinazovikabili vituo vingi vya kutolea huduma ya afya.
Hayo yalisemwa juzi na Mratibu wa Ukimwi katika Halmashauri ya Mji wa Makambako, Dk. Margreth Msasi, alipokuwa akizungumza katika uzinduzi wa Kampeni ya Tokomeza Maambukizi ya Virusi vya Ukimwi kutoka kwa mama kwenda mtoto.
Dk Msasi alisema hali hiyo inachagiza utekelezaji wa mpango wa kuzuia maambuki ya virusi vya Ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.
Alisema changangamoto nyingine katika utekelezaji wa mpango huo ni ukosefu wa dawa katika Bohari Kuu ya Dawa.

Chanzo;Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa