Home » » NI SIKU TATU TUU ZIMEBAKIA KUPATIKANA KWA MAMA SHUJAA WA CHAKULA , MPENDEKEZE SASA

NI SIKU TATU TUU ZIMEBAKIA KUPATIKANA KWA MAMA SHUJAA WA CHAKULA , MPENDEKEZE SASA


Tshs. Milioni 5 Kushindaniwa

Kama unamfahamu mkulima yeyote mwanamke, mtanzania, mwenye umri wa miaka 18 na zaidi, anayelima mazao ya chakula, huu ni wakati wako sasa wa kumpa zawadi ya kufungia mwaka.

Kampeni ya Grow inayoendeshwa na shirika la kimataifa la Oxfam kupitia balozi wake Shamim Mwasha (Blogger 8020fashions) inatoa zawadi ya vifaa vya kilimo vyenye thamani ya Tshs. Milioni 5 pamoja na nafasi ya ushiriki katika shindano la Mama Shujaa wa Chakula 2013 litakalofanyika sambamba na Maisha Plus.

Mpendekeze ashinde sasa kwa kubofya hapa na kujaza nafasi zote  surveymonkey.com/s/growtanzania

Zimebaki siku tatu tu kabla ya shindano kufungwa. Usikubali nafasi hii ikupite. 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa