Home » » CCM WILYA YA NJOMBE YATAKA KUENDELEZWA KWA MIRADI KATA YA MATOLA.

CCM WILYA YA NJOMBE YATAKA KUENDELEZWA KWA MIRADI KATA YA MATOLA.

7 2aac9
 Chama cha Mapinduzi Wilayani Njombe Kimewataka Wananchi wa Kata ya Matola Kuiendeleza Miradi ya Maendeleo Inayotekelezwa Katika Kata Hiyo Kwa Lengo la Kusogeza na Kuboresha Huduma za Kijamii.

Agizo Hilo Limetolewa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Njombe Adam Msigwa Wakati wa Ziara ya Siku Moja Iliyolenga Kutembelea na Kukagua Miradi ya Maendeleo Inayotekelezwa  Katika Kata Hiyo , Ikiwa ni Utekelezaji wa Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu ya Mwaka 2010/2015.

Aidha Mwenyekiti Huyo Aliyeambatana na Viongozi Wengi wa CCM Wilaya   Kwenye Ziara Hiyo Wametembelea na Kukagua Ujenzi wa Vyumba Vya Madarasa, Mabweni , Nyumba za Walimu, Zahanati, Pamoja na Vyoo Vya

Miradi Ambayo Inagharimu Zaidi ya Shilingi Milioni 297  Hadi Kukamilika Kwake.

Akiongea na Wananchi wa Kata ya Matola  Katibu Mwenezi wa CCM  Wilaya ya Njombe Hitra Msola Amewataka Wananchi wa Kata Hiyo Kuwapuuza Watu Wanao Eneza Udini na Ukabila Kwani Husababisha Migogoro Katika Jamii.

Katika Hatua Nyingine Bwana Msigwa Amempongeza Diwani wa  Kata Hiyo Edwini Mwanzinga Pamoja na Wananchi  Wake Kwa Ushirikiano Waliyouonesha Katika Kusimamia Miradi ya Maendeleo na Kuhakikisha Wanasogeza Huduma za Kijamii.
 
Na  Steven  Ngole Njombe

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa