Home » » SHIRIKA LA UMEME TANZANIA MKOA WA NJOMBE LA CHELEWESHA HUDUMA YA KUUNGANISHA UMEME KWA WATEJA

SHIRIKA LA UMEME TANZANIA MKOA WA NJOMBE LA CHELEWESHA HUDUMA YA KUUNGANISHA UMEME KWA WATEJA

 
Meneja wa TANESCO Wilaya ya Njombe Mhandisi Emanuel  Kachewa Amesema Tatizo Hilo Limetokana na Upungufu wa Vifaa Unaolikabili Shirika Hilo

 Hii ni Orodha ya Majina ya Wateja Waliolipia Huduma Hiyo Lakini Bado Hawajapata Kwa Zaidi ya Miezi Saba Sasa.

Zaidi ya Wateja Mia Sita wa Shirika la Umeme Tanzania TANESCO Wilayani Njombe Wameulalamikia Uongozi wa Shirika Hilo Kwa Kushindwa Kuwaunganishia Huduma ya Umeme Kwa Zaidi ya Miezi Sita Licha ya Kukamilisha Taratibu Zote Ikiwemo Malipo ya Huduma Hiyo.

Aidha Wateja Hao Wamelalamikia Kitendo Cha Shirika Hilo Kukiuka Mkataba wa Huduma Kwa Mteja Ambao Kwa Mujibu wa Wateja Hao Walitakiwa Kuunganishiwa Huduma Hiyo Ndani ya
Siku Thelathini Baada ya Kukamilisha Malipo na Kujaza Mkataba.

Wakizungumza na mwandishi wa mtandao huu Baadhi ya Wateja Hao Wamesema Licha ya Kufika Mara Kadhaa Katika Ofisi za Shirika Hilo Kwaajili ya Kufuatilia,Bado Kumekuwa Hakuna Majibu ya Uhakika Jambo Linalosababisha Kushindwa Kupata Huduma Hiyo Hadi Sasa.

Akizungumzia Hali Hiyo Meneja wa TANESCO Wilaya ya Njombe Mhandisi Emanuel  Kachewa Amesema Tatizo Hilo Limetokana na Upungufu wa Vifaa Unaolikabili Shirika Hilo Kwasasa na Kusema Hali Hiyo Imeendelea Kujitokeza Katika Mikoa Mbalimbali Nchini.

Kutokana na Hali Hiyo Bw Kachewa Amewataka Wateja Hao Kuendelea Wavumilivu Katika Kipindi Hiki Ambapo Shirika Hilo Linaendelea Kulitafutia Ufumbuzi Tatizo Hilo na Kuongeza Kuwa Tayari Shirika Hilo

Limezungumza na Wateja Hao na Kuwafahamisha Tatizo Lililopo Kwasasa.
Na  Prosper  Mfugale Njombe 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa