Home » » TSHs.BIL 13.647 ZAANZA KUTUMIKA KATIKA UJENZI WA BARABARA NJOMBE

TSHs.BIL 13.647 ZAANZA KUTUMIKA KATIKA UJENZI WA BARABARA NJOMBE



Meneja wa barabara Mkoa wa Njombe Mhandisi Yusuph Mazana.
Jumla ya Shilingi Bilioni 13.647  Ambazo ni Bajeti ya Barabara Mkoa wa Njombe Kwa Mwaka wa Fedha wa 2013/2014 Zimetajwa Kuanza Kutumika Katika Kuboresha Miundombinu ya Barabara Katika Maeneo Mbalimbali Mkoani Hapa.

Pamoja na Fedha Hizo Kushindwa Kufika Zote Kwa Wakati Lakini Hadi Sasa Fedha za Kuwalipa Wakandarasi Wanaomaliza Kazi Zao Zinaendelea Kutolewa Kutokana na Sekta ya Miundombinu ya Barabara Kupewa Kipaumbele Kikubwa Hapa Nchini.

Meneja wa Tanroad Mkoa wa Njombe Mhandisi Yusuph Mazana Amesema Kuwa Fedha Hizo ni Zile za Barabara Zenye Urefu wa Kilomita 1123.42 Katika Maeneo Yote ya Barabara za Mkoa Ambazo Baadhi ya Zabuni Bado Hazijakamilika.

Mhandisi Mazana Amesema Kati ya Fedha Hizo Shilingi Bilioni 3.150 Zinatoka Kwenye Mfuko wa Matengezo wa Barabara na Kiasi cha Shilingi Bilioni 10.497 Zinatoka Kwenye Mfuko wa Barabara Kuu.

Katika Hatua Nyingine Ameeleza Kuwa Jumla ya Kilomita 719.44  za Barabara ni za Mkoa na Kilomita 403.98 ni Barabara Kuu Ambazo Zinaendelea Kulimwa Katika Kipindi Chote cha Mwaka wa Fedha.

Hata Hivyo Amewataka Wakandarasi Hao Kuhakikisha Wanakamilisha Kazi Zao Kwa Kiwango Kilicho Pangwa na Kwa  Mujibu wa Mikataba Yao Ili Kuendana na Kasi ya Maendeleo Katika Mkoa wa Njombe.




0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa