Home » » WAGANGA WA JADI NJOMBE CHANZO CHA MAUAJI YA VIKONGWE

WAGANGA WA JADI NJOMBE CHANZO CHA MAUAJI YA VIKONGWE

MAUAJI ya vikongwe yameendelea kushamiri katika mkoa wa Njombe kutokana na imani za kishirikina zinazochochewa na waganga wa jadi ambao hupiga ramri chonganishi na kusababisha jamii kutokuwa na amani na ndugu zao..

Imeelezwa katika mwaka 2013 mauaji yanayoshabihiana na Imani za kishirikiana yameripotiwa kwa watu zaidi ya 17 kuuawa kikatiri katika wilaya za Ludewa, makete,Njombe na Wangong’ombe.


Serikali kwa kushirikiana na jeshi la polisi limekuwa likitoa likitoa elimu kwa wananchi kutokimbilia kwa waganga wa tiba asilia, kupiga Ramri hizo  jambo hilo limeonekana kuwa tatizo sugu katika mkoa huo.



Akizungumaza katika kikao cha mwaka cha waganga wa jadi Dkt. Maria Lupenza amesema, kuwa  zaidi ya asilimia 60 ya wagonjwa hutumia tiba asilia kabla ya kufika katika vituo vya tiba za  hospitali na Zahanati jambo ambalo linaonesha ni kwa zaidi ya asilimia 50 ya watanzania bado wanaamini zaidi tiba za asili.

Salumu Mkalla ni Inspekta wa jeshi la polisi katika kikao hicho ameeleza kuwa mauaji ambayo yametokea katika kip[indi cha mwaka mengi kati ya hayo yanashabihiana na imani za kishirikina kutokana na mazingirz ya kifo hata hivyo ameonya waganga hao kukomesha mara moja huduma ya ramri.


Menyekiti wa chawatiata mkoani humo Salumu Lugenge amesema waganga wanaotoa huduma ya kupiga ramri ni wa kutoka nje ya mkoa na hufanya kazi hiyo kwa kujiotangaza kupitia vyombo vya habari kisha hutoweka mara yanapotokea mauaji ambayo ni matokeo ya kazi yao.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa