Home » » IDARA YA UHAMIAJI MKOA WA NJOMBE YAKABIDHI MSAADA KWA WATOTO YATIMA

IDARA YA UHAMIAJI MKOA WA NJOMBE YAKABIDHI MSAADA KWA WATOTO YATIMA

 Bi.Rose Mhagama Akitoa Taarifa ya Gharama za Msaada walioutoa Kwa Watoto Yatima Leo
Watumishi wa Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Njombe Wakiongozwa na Afisa Uhamiaji Mkoa Bi.Rose Mhagama Leo Wamekabidhi Misaada Mbalimbali Kwa Watoto Wanaoishi Kwenye Mazingira Magumu na Yatima Vyenye Thamani Ya Zaidi ya Shilingi Laki Nne.

Akizungumza Wakati wa Kukabidhi Misaada Hiyo Kwa Mwakilishi wa Watoto Yatima Afisa Uhamiaji Mkoa wa Njombe Bi.Rose Mhagama Amesema Kuwa Vitu Hivyo Wameamua Kuvitoa Kama Watumishi Kwa Kutambua Adha Wanazozipata Watoto Yatima Katika Mazingira Tofauti ya Mkoa wa Njombe.

Aidha Amesema Kuwa Miongoni Mwa Vitu Walivyovitoa ni Pamoja na Mchele Kilo Mia Moja,Chumvi,Mafuta Katoni za Sabuni,Dawa za Meno na Miswaki,Mafuta ya Kupikia Pamoja na Soda.

Akipokea Vitu Hivyo Kwa niaba ya Watoto Hao Bwana Sambala Amepongeza Jitihada Kubwa Zinazofanywa na Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Njombe na Kwamba Kitendo Hicho Kinawafanya Watoto Yatima Kufarijika na Kuto kata tamaa ya Kuishi.


Pia Bwana Sambala Amewaomba Wadau Wengine Kuendelea Kujitolea Kuwasaidia Watoto Hao Ambao Wamekuwa Wakipata Shida Katika Katika Maisha Yao.
Chanzo;Na Gabriel Kilamlya blog 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa