Home » » HOT NEWS: ASKARI MAGEREZA WILAYANI MAKETE AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA RUSHWA

HOT NEWS: ASKARI MAGEREZA WILAYANI MAKETE AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA RUSHWA


Juma Msam Swedi mtumishi wa wizara ya mambo ya ndani kitengo cha askari magereza wilayani Makete mkoa wa Njombe amefikishwa katika mahakama ya wilaya ya Makete kwa kosa la kushawishi na kupokea rushwa iliyokuwa na lengo la kumuachia huru mfungwa anayetumikia kifungo gerezani wilayani hapo.

Akisoma hati ya mashtaka mbele ya hakimu mkazi wa wilaya John Kapokolo mwendesha mashtaka wa TAKUKURU mkoani Njombe Bw. Colman Njau amesema kuwa mtuhumiwa anatuhumiwa kwa makosa mawili ambayo aliyafanya mwezi Julai mwaka huu eneo la Ivalalila wilayani hapo ambapo kosa la kwanza ni kushawishi kupewa rushwa ya laki mbili na elfu hamsini kutoka kwa Felix Kivengi Sanga ili kuweza  kumuachia huru Godfrey Mahenge ambaye bado anaendelea kutumikia kifungo kwa sasa.

Kosa la pili kupokea rushwa kiasi cha laki mmoja kutoka Felix  Mahenge ili kumwachia huru mfungwa huyo kinyume cha sheria TAKUKURU sura ya 15 kwenye mabano mmoja A ya mwaka 2007.

Hata hivyo mshitakiwa Juma Swedi alipoulizwa mahakamani hapo alikana kuhusika na tukio hilo na mheshimiwa hakimu Kapokolo ameiharisha kesi hiyo hadi Desemba 13 mwaka huu na mshitakiwa yupo nje kwa dhamana na upelelezi wa tukio hilo bado unaendelea.
 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa