Home » » KIJIJI CHA IKONDO KINAKABILIWA KERO MBALIMBALI.

KIJIJI CHA IKONDO KINAKABILIWA KERO MBALIMBALI.

WANANCHI wa kijiji cha Ikondo mkoani Njombe wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo baadhi ya askari wa jeshi la  polisi kuwadai fedha kama gharama ya kuwafikia kijijini hapo mara  wanapo ripoti kuwepo kwa matukio tofauti kama vifo na mengineyo.

Hayo yamebainishwa na wananchi katika mkutano ulioitishwa na serikali ya kijiji baada ya kutembelewa na kamati ya ushauri ya wilaya, ambayo imefika katika kata hiyo kufanya mkutano na wananchi ili kubaini mapungufu ya kiutendaji na kuyatafutia ufumbuzi.

Ezkieli Mhenga ni mmoja kati ya wananchi ambao wamefunguka kwa kulitupia lawama jeshi la polisi kuwa hutozwa fedha zaidi ya laki tano hadi milioni tano iwapo watatoa taarifa za kuwepo kwa matukio kama ya mtu kujinyonga fedha ambazo askari hudai kuwa ni kwaaajili ya mafuta ya gari.

Akizungumza kwa niaba ya jeshi la Polisi Mrakibu msaidizi wa jeshi la polisi Issa Asali amewashauri wananchi hao kuwa jeshi hilo linapaswa kutoa huduma bure na iwapo watakutana na askari anayedai fedha kama malipo ya kazi taarifa zitolewe kwa viongozi ili kumshughulikia kisheria askari atakaye bainika kupokea fedha hizo.
  
Katika hatua nyingine wameelekeza malalamiko yao katika sekta ya afya  wanawake wajawazito na watoto chini ya miaka mitano kutozwa fedha , Conradi  Ugonile  ni mganga mkuu wa Wilaya  amesema, huduma za watoto na wajawazito ni bure, wakati mkuu wa Wilaya Sarah Dumba amesema kero za wananchi zinashughulikiwa, ikiwemo ukosefu wa dawa katika zahanati na bajeti ya mwaka 2013/14 fedha kwaajili ya kuboresha miundo mbinu imetengwa kinasubiriwa ni utekelezaji

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa