Home » » MKUU WA MKOA AWAKOROMEA WANAOHARIBU VYANZO VYA MAJI

MKUU WA MKOA AWAKOROMEA WANAOHARIBU VYANZO VYA MAJI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Mkuu wa  mkoa wa Njombe  Kapteni Mstaafu Asery Msangi amewaka wananchimkoani    hapa kuitunza na kuiendeleza miradi ya maji inayotekelezwakatika maeneo mbalimbali kwa ufadhili  wa watu wa nje pamoja na
kuvitunza nyanzo vya maji.

Keptein Mstaafu  Msangi  ametoa kauli hiyo  katika wilaya
ya Makete  ambapo amezindua  tenki la maji lenye ujazo wa lita 20,000  litakalo pinguza hitaji la watumia maji ambapo jumla ya lita 1400 zinahitajika kwa matumizi ya siku moja ambapo tatizo la maji wilayani humo ni kubwa.

Wakati huo huo Mkuu wa Wilaya ya NjombeBi. Sara Dumba amewapongeza wananchi wa vijiji ambavyo  vimenufaika katika kutekeleza miradi wa maji huku akiwataka kutunza vyanzo vya maji kwa njia ya kupanda miti rafiki ili visikauke.

Katika taarifa ya utekelezwaji wa mrida wa maji mtiririko wa kijiji
cha Limage iliyosomwa kwa mgeni rasmi ilieleza kuwa kijiji hicho kina jumla ya vituo 15 vya maji ambavyo vinatoa huduma za maji kwa watu 2,119 ,mradi ambao umeanza  kutekelezwa  mwezi januari 2013 na ulitarajiwa kukamilika mwezi disemba 2014.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa