Home » » HALMASHAURI YA MJI NJOMBE YANG’ARA KWA HATI SAFI RIPOTI YA CAG, IDARA ZAASWA KUTOKIONA KITENGO CHA UKAGUZI WA NDANI KAMA MWIBA WA PORI.

HALMASHAURI YA MJI NJOMBE YANG’ARA KWA HATI SAFI RIPOTI YA CAG, IDARA ZAASWA KUTOKIONA KITENGO CHA UKAGUZI WA NDANI KAMA MWIBA WA PORI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.








Mweka Hazina wa Halmashauri ya Mji Njombe Dorcas Mkello akiwasilisha hoja za ukaguzi mbele ya Mkutano Maalumu wa Baraza Kuu la Madiwani.




Wakuu wa Idara na Vitengo Halmashauri ya Mji Njombe wakisikiliza kwa Makini mapendekezo ya Baraza la Madiwani.




Katibu Tawala Mkoa wa Njombe Jackson Saitabahu akitoa mapendekezo yake mara baada ya kupitia hoja za ukaguzi.




Madiwani wakipitia makabrasha yenye hoja za Ukaguzi.

Na Hyasinta Kissima, Njombe

Halmashauri ya Mji Njombe imerudisha heshima yake kwa kupata Hati safi katika ripoti ya mthibiti na mkaguzi wa serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2015/2016) ambapo kwa mwaka wa fedha 2014/2015 Halmashauri hiyo ilipata hati inayoridhisha na yenye maswala ya msisitizo.

Akitoa mapendekezo yake wakati wa Mkutano Maalumu wa Baraza la Madiwani la kujadili hoja za Mthibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Katibu Tawala Mkoa wa Njombe  Jackson Saitabahu ameipongeza Halmashauri kwa kupata hati safi na kwa kukusanya mapato kwa asilimia 100.1 na amezitaka idara na vitengo vya Halmashauri kutoona Ofisi ya Ukaguzi wa ndani kama mwiba wa pori na mahali pasipoingilika kwani Kitengo hicho kipo kwa ajili ya kutoa ushauri lakini pia kuiandaa Halmashauri kwa Ukaguzi Mkuu hivyo wasisite kuomba ushauri pale inapobidi.

“Hati safi haiji kwa bahati mbaya, napenda niwapongeze kwa jitihada kubwa mlizoonyesha lakini pia niwasihi sana msikwepe Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani, Kitengo hiki kinatakiwa kiwezeshwe vizuri na Halmashauri ijenge mahusiano mazuri na Kitengo cha Ukaguzi kwani wakaguzi wa ndani ndio wanatuandaa kwa ajili ya ukaguzi wa nje.Tunapoimarisha mahusiano mazuri miongoni mwetu hatutakua na hoja za ukaguzi.Tusiwe mabingwa wa kujibu hoja zaidi ya kuwa wataalamu wa kuzuia hoja zisitokee.”Alisema Katibu Tawala.

Sambamba na hilo Halmashauri pia imeendelea kuimarika kwa kufikia asilimia 35% za kuweza kujitegemea jambo ambalo limeendelea kuifanya Halmashauri ya Mji Njombe kufanya vizuri katika shughuli mbalimbali za maendeleo.

Kwa mwaka 2017/2018 Halmashauri imejipanga kuhakikisha kuwa hoja zote zinafungwa, kukusanya mapato zaidi ya mwaka uliopita na kuhakikisha kuwa Halmashauri haitoruhusu kufanya biashara na Wakandarasi na wazabuni wasio na mashine za kielektroniki na kuhakikisha kuwa nyaraka na kumbukumbu zote za manunuzi zinatunzwa ipasavyo.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa