Home » » TUKIO KATIKA PICHA: BASI LA KAMPUNI YA JAPANESE LATUMBUKIA MTONI MKOANI NJOMBE

TUKIO KATIKA PICHA: BASI LA KAMPUNI YA JAPANESE LATUMBUKIA MTONI MKOANI NJOMBE


 Basi la Japanese lenye namba za usajili T 261 CMK aina ya YUTONG likiwa limetumbukia mtoni na kusababisha abiria kadhaa waliokuwa wakisafiri na basi hilo kutoka Ikonda wilayani Makete kwenda Makambako mkoani Njombe kujeruhiwa. Hadi tunaondoka eneo la tukio hakuna abiria aliyepoteza maisha na majeruhi wote waliwahishwa hospitali kwa matibabu zaidi. Ajali hiyo imetokea jana majira ya saa nane mchana.
 Majeruhi wa ajali hiyo akizungumza na mwandishi wetu muda mchache kabla ya kuwahishwa hospitali kwa matibabu zaidi.
Mmoja wa wafanyakazi wa basi hilo ambaye naye amejeruhiwa kidogo katika ajali hiyo akiwa katika hali ya huzuni. Taarifa na picha zaidi za tukio hilo zitakujia hivi punde endelea kusoma Eddy Blog
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa