Home » » MAOFISA WA AFYA NJOMBE WATAKIWA KWENDA KUFANYA UKAGUZI MITAANI

MAOFISA WA AFYA NJOMBE WATAKIWA KWENDA KUFANYA UKAGUZI MITAANI

Diwani wa Kata Ya Mjimwema Jimmy Ngumbuke
Uongozi wa Kata ya Mjimwema Mjini Njombe Umewataka Wananchi na Wafanyabiashara Mbalimbali Kuyaweka Mazingira Yao Katika Hali ya Usafi Hasa Katika Kipindi Hiki cha Mvua Ili Kuepuka  Magonjwa ya Mlipuko.

Rai Hiyo Imetolewa na Diwani wa Kata Hiyo Jimmy Ngumbuke Kufuatia Baadhi ya Wananchi na Wafanyabiashara wa Maeneo ya Kata ya Mjimwema Kutupa Uchafu Ovyo Hali Inayotishia Afya za Wakazi wa Maeneo Hayo.

Diwani Mgumbuke Ameuomba Uongozi wa Halmashauri ya Mji wa Njombe Kuwaagiza Wataalam wa Afya na Mazingira Kuyafanyia Ukaguzi Mara Kwa Mara Maeneo ya Biashara Zikiwemo Hoteli , Migahawa , Vilabu Vya Pombe za
Kienyeji Pamoja na Makazi ya Watu.

Kwa Upande Wao Baadhi ya Wakazi wa Mitaa ya Mpechi na Joshoni Wameuomba Uongozi wa Halmashauri ya Mji wa Njombe Kuwajengea Ghuba la Kutupia Taka , na Kuongeza Kuwa Kwasasa Wamekuwa Wakihifadhi Takataka Kwenye Ndoo na Mifuko na Kisha Kuziweka Barabarani  Jambo Linalohatarishaa Afya Zao Kwani Wakati Mwingine Takataka Hizo Hukaa Zaidi ya Siku Mbili Bila Kuondolewa.

Alfani Ngulwa ni Mwenyekiti wa Mtaa wa Joshoni Ambaye Amekiri Kuwepo Kwa Tatizo Hilo Katika Mitaa Hiyo na Kusema Kuwa Hali Hiyo Inatokana na Kutokuwepo Kwa Ghuba la Kutupia  Takataka Hizo.
Chanzo; gabriely kilamlya blog

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa