
Mfuko
wa Pensheni wa PSPF unapenda kuutaarifu Umma kuwa umezindua Mpango Mpya wa
uuzaji nyumba zake zilizojengwa kwa ajili ya makazi katika mikoa ya Dar es
Salaam- Ilala (Buyuni), Morogoro (Lukobe), Tabora (Usule), Mtwara (Mang’amba), Shinyanga
(Ibadakuli) na Iringa (Mawelewele).
Bei
za nyumba ni kati ya sh. 52,000,000.00 hadi sh. 71,000,000.00 (bila VAT). Bei
hizi ni kulingana na ukubwa wa nyumba na mkoa nyumba ilipo. Ukubwa wa nyumba ni kuanzia vyumba viwili
hadi vinne.
Chini
ya utaratibu huu mpya unaoanza kutumika kuanzia Februari 2014; Muombaji
atapaswa kuainisha kwenye fomu ya maombi aina ya nyumba anayohitaji na Mkoa
ilipo. Malipo...