Home » » MWENYEKITI MPYA WA CCM LUDEWA AAHIDI MAKUBWA KWAVIJANA

MWENYEKITI MPYA WA CCM LUDEWA AAHIDI MAKUBWA KWAVIJANA

Festus Pangani, Njombe Yetu.

Mwenyekiti wa vijana kupitia Chama Cha Mapinduzi wilayani Ludewa Bi.Elizabeth Augustino Haule ameahidi kufanya mambo makubwa kwa vijana baada ya kumchagua kuwa mwenyekiti kwa kipindi cha miaka mine.

 Akizungumza na waandishi wa habari jana Bi. Elizabeth alisema kutokana na yeye kuwa mjasiliamali atatumia fulsa hiyo kwa kushirikiana na wadau wengine wilayani humo kutoa elimu ya kujitambua kwani vijana walio wengi bado hawajitambui.

 Alisema kijana anapaswa kijiajiri na si kusubiri kuajiriwa kwa maisha bora kwa kila mtanzania hayaji kwa kutofanya kazi na kusubiri mtu au kampuni ianzishe ndipo uajiliwe.

Elizabeth alibainisha kuwa mafanikio yake mpaka alipofikia kuwa mwenyekiti ni juhudi binafsi na si mtu alikuwa nyuma yake kwani katika mikakati yake ilikuwa kuwa diwani wa viti maalumu lakini bado lengo hilo halijafikiwa na hajakata tamaa kwa hilo.

Aidha amewataka vijana wa Chama Cha Mapinduzi kutokukubali kurubuniwa na wanasiasa kwa kuwa mgongo wao bali kuzingatia kanuni na sheria za chama hicho katika kuwapata viongozi bora na kuendeleza juhudi za kukijenga chama.

Bi.Eliza alisema vijana kwa sasa wanahitaji elimu ya ujasilia mali na mitaji na si vinginevyo hivyo kama itaanzishwa Bank ya vijana itakuwa ukombozi mkubwa kwani vijana wengi wataweza kupata mitaji na kufanya biashara zao.

Aliwaasa vijana wa wilaya ya Ludewa kutobweteka badala yake kujituma katika kazi mbalimbali kwani kupitia migodi ya Mchuchuma na Liganga vijana wa Ludewa wataweza kujikwamua kiuchumi na kuendesha maisha yao bila hofu.

Bi.Elizabeth alisema vijana wengi nchini wamekuwa ni watu wa kulalamika badala ya kufanya kazi hiyo si busala kwani maisha bora kwa kila mtanzania hayaji kwa malalamiko bali kwa kujitambua katika ufanyaji kazi za kujiongezea kipato.

Blogzamikoa

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa