Home » » WASHANGAZWA NA USHINDI WA HALMASHAURI YA MJI NJOMBE USAFI WA MAZINGIRA

WASHANGAZWA NA USHINDI WA HALMASHAURI YA MJI NJOMBE USAFI WA MAZINGIRA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Na James Festo, Njombe.

KATIKA kuelekea siku ya maadhisho ya mazingira  ambayo hufanyika june tano ya kila mwaka  huku Halmashauri ya mji wa Njombe ikiwa inaendelea kushika nafasi za juu kwa usafi   wananchi wake wameendelea kuitupia lawama za kushindwa kuzoa takataka  kwenye vizimba hali ambayo inaweza kusababisha  magonjwa ya mlipuko.

Hali hiyo inakuja kufuatia kusuasua kwa uzoaji taka  katika vizimba vya takataka vikiwemo vilivyopo karibu na maeneo yanayotumika katika uuzaji wa vyakula  kitu ambacho kinaweza kusabisha madhara makubwa kwa wauzaji pamoja na wateja wao

Mwandishi wa habari hii alitembelea na kujionea  vituo mbalimbali Ndani ya halmashauri ya Mji wa Njombe  hali mbaya ya takataka zilizofurika  nje ya vizimba  licha ya wananchi kuendelea na biashara  likiwemo eneo nyuma ya kituo cha mabasi mjini njombe.

Wakizungumza na majira baadhi ya wafanyabiashara hao walisema kuwa tangu kusimama  kwa mawakala waliokuwa wakifanya kazi hiyo ya kuzoa takataka kwenye vizimba na Halmashuri kuvaa jukumu hilo  mwenendo umekuwa wa kusuasua na kueleza kushangazwa  kuona wakilipa ushuru kila uchao wakati taka hazizolewi kwa wakati.

 "   sasa hivi michango imesitishwa  ndio maana ya kwenye vizimba taka ni nyingi.... labda kila mwananchi awe anachangia  kila kaya ...tunataka tuchangie..... tukisema tufanye hivi hatufiki ...... wakala ameshindwa kufanya kazi kwa sababu  kipato anachopata halmashauri  ni kidogo "   walisema wafanyabiashara hao.

Aidha Wafanyabiashara  hao waliiomba halmashuri kutumia  fedha zinazokusanywa katika ushuru wa soko kutumika katika kufanya usafi wa soko hilo na kuwasisitiza watumishi wa sekta hiyo kuacha uzembe wa kukaa ofisini.

Andove Mgani ni mwenyekiti wa  soko la  wafanyabishara lililopo nyuma ya kituo cha mabasi cha Njombe alisema kuwa tangu Halmashuri ya Mji ianze kusimamia yenyewe  zoezi ya utoaji wa taka hizo imekuwa ikizidiwa na kusababisha  taka kukaa zaidi ya wiki  kitu ambacho ni hatari kwa wananchi  mjini hapa.

"  ninachojua zamani taka taka na yule wakala alikuwa makini na kazi yake lakini baada ya kusimamiwa na halmashauri  vizimba vya hapa mjini vyote vinakaa na takataka muda wote  kama wafanyabiashara tungekuwa na uwezo wa kuamua  tungemuaomba arudi afanye kazi ya kuzoa takataka"   alisema Bw Ndonya.

Kwa upande wake kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Njombe Bw. Venance Msungu alikiri kuwepo kwa tatizo hilo la uzoaji wa takataka  alisimama kutokana kiasi cha fedha aliyokuwa akilipwa huku mji wa Njombe ukiendeea kuongezeka kwa uchafu.

Alisema kuwa katika kipindi cha miezi miwili baada ya wakala huyo Halmashauri hiyo imekuwa ikiendelea na zoezi hilo  huku wakisubiri mwezi julai mwaka huu wa kutangazwa kwa mzabuni ambaye ataanza kufanya kazi hiyo ambaye atakuwa na vifaa vya kutosha tofauti na Halmashauri  ambayo imekuwa ikitumia magari mawili pekee.

"  hata waandishi wa habari inayostahili watu wanaongea kwamba uchafu bado tatizo jambo linaonyesha kukosa uelewa wa kulinganisha na sehemu zingine  hapa nchini....zabuni zitafunguliwa mwezi huu  wa sita  na inapoanza mwezi julai  tutakuwa na mzabini mwenye vifaa vya kutosha vya kutolea uchafu"   alisema bw Msungu.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa