Home » » Katiba mpya: Wakulima wadai kupuuzwa maoni yako

Katiba mpya: Wakulima wadai kupuuzwa maoni yako

Njombe

RASIMU ya katiba mpya imeingia doa baada ya wakulima kudai kuwa tume ya katiba ya Jaji wa Joseph Walioba imeyapuuza maoni yao.

Hoja hiyo imeibuliwa  katika mkutano  mkuu wa mwaka  wa muungano wa  vikundi vya wakulima  wadogo wadogo  nchini  (MVIWATA)  ambao umefanyika katika  mkoa wa Njombe.

Mkutano huo umehusisha   wanachama  na viongozi wa bodi Taifa wa MVIWATA kutoka  Kanda  sita  zinazojumisha mikoa yote ya Tanzania  bara , ambao ulilenga kuzungumzia maendeleo ya Mtandao kwa ujumla.

Mwenyekiti MVIWATA  Habibu Simbamkuti amesema, kuna mambo ambayo ni ya msingi yamepuuzwa katika Rasimu ya katiba mpya amabayo walianisha na kuwayawasilisha katika Tume.

Upande wao wakulima   wamesema,licha ya kuwepo vikwazo lukuki pia ushirikishwaji ni kitendawili kisichoteguka, kile kilichodaiwa kuwa mikataba ya uwekezaji katika sekta ya ardhi haihusishi maoni ya mkulima moja kwa moja na kusababisha migogoro kati yao.


Mjadala wa rasimu ya katiba mpya umehitimishwa mwishoni mwa wiki hii, ambapo maoni na mapendekezo ya kitaasisi yanawasilishwa kwenye tume ya Jaji  mstaafu  Joseph  Walioba  kabla ya kupeleka kwenye Bunge la katiba Novemba mwaka huu.
mwisho

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa