Home » » WANAOJISAIDIA OVYO MAKETE WAICHEFUA SERIKALI

WANAOJISAIDIA OVYO MAKETE WAICHEFUA SERIKALI


Na Edwin Moshi, Makete

Serikali wilayani Makete mkoani Njombe imewataka wananchi kutoa ushirikiano wa pamoja kuwakamata ama kutoa taarifa kwa ngazi husika pindi wanapowaona watu wakijisaidia ovyo maeneo yasiyo rasmi.

Hayo yamesemwa na afisa afya wilaya ya Makete Bw Boniphace Sanga wakati akizungumza na mtandao huu na kuongeza kuwa kumekuwa na ongezako la magonjwa hasa ya kuhara ambayo yanatokana na watu wanaojisaidia ovyo na kuchafua mazingira.

Bw sanga amesema jukumu la usafi ni la kila mmoja na si la bwana ama bibi afya pekee na kwa kuwa wananchi ndio wanaoshinda maeneo mbalimbali wanawaona wale wanaojisaidia hovyo na kuomba watoe taarifa kwenye ofisi yake ili wachukuliwe hatua za kisheria.

Amesema inashangaza kuona hadi sasa wapo watu ambao hawana vyoo na wanaongoza kwa kuchafua mazingira kutokana na kujisaidia ovyo, na kutoa wito kuwa msimu huu ni wa kiangazi hivyo wanatakiwa kujenga vyoo kabla mvua haijanyesha.

"Kwa kweli natoa wito nyumba bila choo haijakamilika, acheni kun***a(akimaaisha kujisaidia) maeneo ambayo si kwa ajili hiyo, unakuta mtu kavaa vizuri lakini ni namba moja kujisaidia maporini, huu si ustaarabu na watu wa namna hii ndio wanaoleta magonjwa kwenye wilaya yetu.

Katika hatua nyingine Bw. sanga amewaomba wananchi kuendelea kujijengea utaratibu wa kutupa taka maeneo yanayoruhusiwa( kwenye vizimba vya taka) na kuwaasa kuacha tabia ya kutupa chupa za soda na maji mitaani kwani hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa watakaokamatwa.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa