Home » » KAMPUNI YA TANWAT YATOZWA FAINI YA MILIONI HAMSINI KWA UHARIBIFU WA MAZINGIRA

KAMPUNI YA TANWAT YATOZWA FAINI YA MILIONI HAMSINI KWA UHARIBIFU WA MAZINGIRA

Na Lulu Mussa
Njombe

Wadau wa Mazingira wametakiwa kufuata Sera, Kanuni na Tararibu katika kuendesha shughuli zao.  Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. January Makamba ameyasema hayo leo Mkoani Njombe alipokuwa katika mwendelezo wa ziara ya kutembelea Mikoa mbalimbali hapa nchini kwa lengo la kujionea hali ya mazingira na kutoa maelekezo stahiki.
Waziri Makamba ametoza faini Kampuni ya TANMAT kwa kuikuka Sheria ya Mazingira inayokataza upandaji wa miti ndani mita sitini kutoka katika chanzo cha maji. "Kampuni hii imevunja sheria hivyo hamna budi kuchukuliwa hatua stahiki ili iwe mfano na kwa wengine" alisisitiza Waziri Makamba.
Kampuni hiyo imeagizwa kulipa faini hiyo ndani siku saba na endapo watakiuka hatua kali zaidi za kisheria zitachukuliwa dhidi yao. Waziri Makamba pia ameiagiza Kampuni hiyo kuondoa miti hiyo ambayo si rafiki kwa mazingira mapema iwezekanavyo na kuagiza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kuwapa 'Restoration Order"  kurudisha mazingira katika hali yake ya kawaida.
Katika hatua nyingine, Meneja wa Kampuni hiyo inayojishughulisha na upandaji wa miti Bw. Joseph Shirima amekiri kupokea barua zizoelekeza kusitisha uharibifu huo wa Mazingira katika chanzo cha Mto Mbukwa ambacho kinasambaza maji kwa wakazi wengi wa Wilaya ya Wanging'ombe.
Aidha, Waziri Makamba ameupongeza Uongozi wa Mkoa wa Njombe kupitia Mkuu wa Mkoa huo Dkt. Rehema Nchimbi kwa kuwa mstari wa mbele kuhamasisha wanachi kuacha kulima bustani za mbogamboga pembezoni mwa mito.
Dkt. Nchimbi alimfahamisha kuwa kwa sasa kuna kikundi kijulikanacho kwa jina la "Jerusalemu" kinachotoa mafunzo kwa wananchi juu ya matumizi bora ya ardhi na kuhamasisha uhifadhi wa mazingira ambapo lengo ni kuanzisha vituo kama hivyo vya mafunzo kwa Halmashauri zote za Mkoa huo.
Waziri Makamba alitembelea na kuona "vinyungu" ambavyo awali vilikua vikilimwa kando ya mito na kwasasa vimehamishiwa majumbani, katika kuunga mkono jitihada hizo njema Waziri Makamba amechangia mifuko Hamsini ya Saruji kwa ajili ya ujenzi wa darasa litakalotumika kutoa mafunzo zaidi ya kilimo.
Waziri Makamba Waziri Makamba anaendelea na ziara yake ya kikazi ya kukagua hali ya mazingira nchini, hii leo amewasili katika Mkoa wa Mbeya.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa