Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji), Dk. Mary Nagu.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na
Uwezeshaji), Dk. Mary Nagu, amesema kazi ya kuwawezesha wananchi
kiuchumi si ya serikali pekee hivyo wadau malimbali na taasisi za fedha
zinapaswa kutumia sehemu ya faida yake kuwasaidia wananchi kujikwamua
kiuchumi.
Aliyasema hayo ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana wakati wa
kikao cha kazi baina yake na Wajumbe wa Baraza la Uwezeshaji la Baraza
la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), akiwamo Katibu Mtendaji
wa Baraza hilo, Beng’i Issa na Mwenyekiti wa Bodi, Omari Issa.
Baadhi...
AIBU NYUMBA ZA WAKUBWA KUTUNZA MIHADARATI
Tanzania imekuwa katika vita ngumu ya kupambana na matatizo
mbalimbali yanayoisumbua, yakiwamo ya kiuchumi, kijamii na hata kisiasa.
Katika baadhi ya nyakati, matatizo hayo yamegeuka kuwa kikwazo kwenye azma ya kuwapa maendeleo na ustawi wananchi.
Pamoja na matatizo hayo, siku za karibuni na
pengine miaka michache iliyopita, biashara za dawa za kulevya imegeuka
adui anayeichachafya nchi.
Kwa kiasi kikubwa, biashara hii ambayo inaonekana
dhahiri kuwa inahusisha wengi, wakiwamo watu wazima na hata watoto na
wengine vijana wasomi wazuri, imegeuka vita ambayo kama nchi ijihesabu
kuwa imeshindwa kuidhibiti.
Hatuchelei kusema nchi yetu imeshindwa vita...
SIMU ZINAVYOSHAWISHI MAPENZI KWA WANAFUNZI
Tangu teknolojia ya mawasiliano ya simu za mkononi ilipoingia
nchini, mambo mengi katika jamii, ukiwamo mfumo mzima wa maendeleo na
namna ya kuishi, yamebadilika.
Teknolojia hiyo imeondoa usumbufu uliokuwapo
awali, mtu alikuwa analazimika kukaa muda mrefu kusubiri kuunganishiwa
simu posta na baadaye katika Kampuni ya Mawasiliano ya Simu Tanzania
(TTCL). Hata baada ya kupata mawasiliano bado usikivu ulikuwa hafifu
licha ya kupiga kelele sana.
Si hivyo tu, watu walikuwa wanalazimika kufika
mjini au miji maarufu kwa ajili ya kusaka mawasiliano ya simu. Pia,
wengi walikosa.
Kutokana na gharama kubwa ya simu wakati ule,
haikuwa rahisi kwa wanafunzi kuzifikia. Wale waliomudu kupiga...
FAMILIA YA MSWEMWA YATUMIA MILIONI 100 KUSAIDIA JAMII YA WANANJOMBE
Mkurugenzi wa
Hotel ya Miriam Njombe Bw Ditram Msemwa wa sita kushoto akimpongeza
Bw Ngamanga kwa uzinduzi wa kitabu chake
Mkurugenzi wa Hotel ya Miriam Njombe Bw Ditram Msemwa akizungumza katika hafla ya kufunga mwaka
Baadhi ya vijana wanaonufaika na fursa hiyo
Baadhi ya wanafamilia na wadau mbali mbali
washiriki wakifuatilia hafla hiyo
Mkurugenzi wa taasisi ya Mafanikio foundation for personal development na mratibu wa raslimali watu Bw Michael uhahula akitoa maelezo ...