Home » » TANESCO NA MWEKEZAJI KUTOKA MAREKANI KUZALISHA UMEME MEGAWATI 400

TANESCO NA MWEKEZAJI KUTOKA MAREKANI KUZALISHA UMEME MEGAWATI 400

Na Festus Pangani, Njombe Yetu
Serikali ya Tanzania kupitia shirika la umeme tanesco kwa kushirikiana na mwekezaji kutoka nchini marekani, inajiandaa kutekeleza mradi wa umeme wa maji katika mto ruhuji.
Akizungmza wakati wa baraza la madiwani Mpimaji ardhi   mwandamizi wa Tanesco makao makuu Hamis Boby amesema mradi huo unatarajiwa kukamilika hadi kufikia mwaka 2019 na kuzalisha umeme wa megawati takribani mia tatu hadi mia nne.
Boby amesema mradi huo utahusisha ujenzi wa mgodi kufua  umeme wa megawati 350 hadi 400, bwawa la kuhifadhi maji, bwawa la kuzalisha umeme, njia ya umeme, barabara, njia ya kusafirisha maji chini ya ardhi, ofisI na makazi.
Hata hivyo amesema hatua hiyo itazingatia haki za wananchi katika eneo husika kwa kulipwa fidia ya ardhi, kupata huduma za kijamii, elimu ya mahusiano, pamoja na huduma nyingine zitakazopendekezwa kwenye makubaliano yao na wadau.
Kwa upande wao madiwani wa halmashauri ya mji wa Njombe na wilaya ya Njombe wameupongeza mpango huo wa serikali na kuwataka wawekezaji hao kutoa fidia kwa wananchi watakaohamishwa ili kupisha utekelezaji wa mradi huo bila ubaguzi wala upendeleo.
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ludewa Venancy Kabelege amewataka madiwani kushirikiana na serikali katika kuwahamasisha wananchi ili kufanikisha zoezi hilo la mradi.
Blogzamikoa

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa