Home » » MAFUTA YA PETROLI YAADIMIKA MKOANI NJOMBE

MAFUTA YA PETROLI YAADIMIKA MKOANI NJOMBE

Festus Pangani, Njombe Yetu
Kwa siku ya tatu sasa mji wa Njombe umekumbwa na adha ya kukosekana kwa nishati ya mafuta ya petroli kwenye vituo vya mafuta hali inayopelekea kukwama kwa usafiri na kushuka kwa uchumi miongoni mwa jamii.
Hali hiyo imetokea kuanzia septemba 30 mwezi uliopita hadi sasa ambapo hadi hii leo ni kituo kimoja tu cha mafuta cha Ndime PetrolSstation kinauza mafuta hayo.
Wakizungumza na Njombe Yetu kwa nyakati tofauti baadhi ya madereva wa magari na pikipiki mjini Njombe wamesema kuwa adha hiyo imepelekea baadhi ya magari na pikipiki kuzima njiani yakiwa na abiria kitu ambacho kimeleta usumbufu kwa abiria.
Kwa upande wao mameneja wa baadhi ya vituo vya mafuta mjini hapa Prosper Mtewelewa wa kituo cha Ndime Petrol Station na Kaimu Meneja wa kituo cha mafuta cha Total wamesema tatizo hilo limetokea sehema ya kusambazia mafuta kutokana na siku za jumamosi na jumapili kutokuwepo kikazi.
Hata hivyo pamoja na kutokuwepo kwa mafuta mjini Njombe hakuna ongezeko lolote la bei ya mafuta mkoani hapa.
Blogzamikoa

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa