Home » » WANANCHI LUDEWA WAMZOMEA MGOMBEA UBUNGE AOKOLEWA KUPIGWA KISA UONGO KUMTUKANA FILIKUNJOMBE‏

WANANCHI LUDEWA WAMZOMEA MGOMBEA UBUNGE AOKOLEWA KUPIGWA KISA UONGO KUMTUKANA FILIKUNJOMBE‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

kada wa CCM anayeomba  kuteuliwa  kugombea ubunge jimbo la Ludewa kepten mstaafu Jacob Mpangala ambae leo amezomewa mkutanoni na kuokolewa  kichapwa baada ya kujinadi kwa kutumia lugha za matusi na uongo dhidi ya mbunge Deo  Filikunjombe 
mbunge Filikunjombe akiwapungia mkoano  wananchi wa mndindi baada ya  kujinadi
wananchi wa kata ya Ibumi  wakiwa  wametuliwa wakimsikiliza kwa makini mbunge Filikunjobe wakati akiomba  kura  zao
Filikunjombe  akisisitiza jambo wakati akiomba kura kwa wananchi wa Ibumi leo ,wananchi hao walivuruga mkutano  huo baada ya mtia nia mmoja kupanda jukwaani na kutoa taarifa  za uongo na matusi ya nguoni dhidi ya mbunge wao
Filikunjombe akiwashukuru wananchi wa Ibumi kwa imani yao kwake
mratibu wa  zoezi la kuwanadi wagombea kwa wana ccm John kiowi akitangaza kuvunja mkutano  huo baada ya kuibuka vurugu .

Na matukiodaima BLOG

 KATIKA kile  kinachoonyeshwa  kuwa wananchi  wa Ludewa kumkubali mbunge wa  jimbo  hilo Deo Filikunjombe kuendelea kuongoza  jimbo  hilo kwa awamu  nyingine leo  wana CCM na  wananchi  wa kata  ya Ibumi wamemzomea mmoja kati ya watia nia ubunge wa jimbo hilo na  kutaka kumchapa wakati wa mkutano wa  watiania hao kujinadi kwa  wananchi baada ya mtiania  huyo kepten mstaafu Jacob Mpangala kutumia maneno ya uongo na  lugha chafu dhidi ya mbunge huyo  wakati akiomba kura .

Tukio   hilo  limetokea majira ya saa 11 jioni katika   viwanja vya ofisi ya  CCM kata ya  ibumi wakati mgombea  huyo ambae alikuwa wa  mwisho kujieleza na kuomba  kura kujikuta akishishwa  jukwaani kwa kuzomewa huku baadhi ya wananchi wakimsogelea  kwa lengo la kutaka  kumpiga kwa madai ni muongo na anatumika kumchafua mbunge  wao na mmoja kati ya vigogo  wa CCM ambae alikuwa akitaka ubunge wa  jimbo  hilo.


Kabla ya  mtia nia  huyo  kukutwa na tukio  hilo la  kuzomewa na kutaka kupigwa tayari mbunge  Filikunjombe alikuwa ameanza  kujieleza na kuwaeleza  wananchi hao kazi ambazo amepata  kuzifanya na kazi ambazo anataraji kuzifanya kwa awamu ya  pili iwapo watamchagua tena katika  kinyang'anyiro  hicho 


Akijinadi kwa wananchi hao huku akishangiliwa na kwa kuitwa jembe letu ,Filikunjombe alisema  kuwa amejitahidi kufanya kazi kubwa  kulingana na uwezo wake na  atakuwa muongo mbele za Mungu na  wananchi hao iwapo atajisifu kuwa amemaliza kero  zote za  wananchi wa Ludewa ila anajivunia kuwepo kwa maendeleo makubwa ukilinganisha na wabunge  waliopita na yale yaliyofanywa na wabunge  wenzake.

'' Ndugu  zangu  natambua  nimefanya mengi  kulingana na uwezo wangu na kulingana na wabunge  wenzangu  waliotangulia ila sipendi kuwadanganya  kuwa matatizo ya  wana Ludewa nimeyamaliza  yote ......kupanga ni kuchagua na mimi nilichagua kuanza na mambo makubwa mawili likiwemo na kuanza kwa miradi mikubwa ya mchuchuma na liganga ambayo  wakati wowote kabla ya Rais Dr Jakaya Kikwete hajamaliza  muda  wake atafika  kuweka  jiwe la msingi la uanzwaji na ujenzi wa viwanda   hivyo .....lakini  pia juu ya miundo mbinu tayari ujenzi wa barabara ya lami umeanza  na mengine mengi ambayo hajakuwemo katika ahadi  zangu  ili  nilifanya kulingana na uhitaji wa  wananchi wangu'


Filikunjombe ambae  muda  wote  wakati akijinadi  wananchi  walishindwa  kujizuia  kushangilia mbali ya kuzuiwa kufanya  hivyo alisema  kuwa matumaini yake ni kuona kasi ya maendeleo katika  jimbo  hilo  inazidi kupaa zaidi ya hapo na  kuwa ushirikiano ambao wananchi  wameonyesha kwake kwa  kipindi  kilichopita  ndio ambao  anategemea  wataonyesha  kwake kwa kumchagua kwa kura  nyingi  zaidi siku ya Augost 1 mwaka huu wakati wa  kura  za maoni .

Hata  hivyo  aliwataka  wana ccm  na  wananchi wa Ludewa  kujiepusha na kauli  za uongo ambazo  zinatolewa  hivi  sasa na baadhi ya wagombea ambao wanatumika  kumchafua na badala  yake  kubaki na msimamo  wao wa  kushirikiana nae kuendelea  kuleta maendeleo  zaidi .

katika hali  isiyo ya kawaida wananchi hao  waliomba kurusiwa  kumshingalia ama  kumpa  zawadi  mbunge huyo kama pongezi zao kwa kazi kubwa aliyoifanya  japo mratibu wa  zoezi  hilo la kuwatembeza  watia nia hao alizuia kuwa  taratibu haziruhusu .

Hali ya mkutano huo  ilionekana ni shwari hadi mtia nia wa pili injinia zephania chaula alipopanda jukwaani na kujinadi na kuulizwa maswali yake matatu   na  kujibu kisha  kuomba  kura  zake  ila upepe  ulibadilika  ghafla  alipopanda  mpangala ambae alionyesha  kuwa na jazba  zaidi na badala ya  kuwaeleza wananchi atafanya nini  alianza kubeza maendeleo yaliyofanywa na mbunge   huyo pamoja na kutumia  lugha za matusi ya nguoni kumshambulia mbunge kbala ya  wananchi kupandwa na hasira na  kuanza kumzomea na wengine  waklitawanyika katika mkutano  huo huku baadhi yao wakipangwa na jazba na kumshusha mgombea  huyo jukwaani kwa kutishia  kumpiga.

Wananchi hao  walifikia hatua  hiyo  baada ya mtia  nia huyo ambae ni mara  yake ya kwanza  kufika katika  kata  hiyo kudai  kuwa kazi za maendeleo  zilizofanywa na mbunge katika kata  hiyo na zile za ujenzi wa lami amezifanya yeye huku akitukana matusi ya nguoni mbele ya watoto na  wananchi hao hali  iliyopandisha hasira na kumshusha jukwaani  kabla ya mratibu wa zoezi hilo kulingilia kati na kumpokonya kipasa  sauti na kumtaka akae katika kiti na kuzuia kuulizwa maswali na kuvunjwa mkutano  huo kwa usalama wa mgombea  huyo ambae alionyesha  kuwakwaza  wananchi kabla ya  wao kuhamaki na kutaka kumchapa.

Wakizungumza kwa jazba  wananchi  hao akiwemo mzee Joachim Luoga walisema  kuwa  wamesikitishw sana na hatua ya mtia  nia huyo  kutumia  vibaya  jukwaa na kutukana matusi ya nguoni  badala ya  kueleza sera  zake kwa wana Ludewa na kuwa wao kama  wazee  walimtaka aombe radhi ila amnegoma na kuwa wanakiomba  chama cha mapinduzi kumwondoa mtia nia huyo katika mchakato  huo kwani anavuruga sifa ya  chama.


Mratibu wa zoezi hilo la  kuwazungusha watia nia hao John Kiowi akizungumza na  wananchi hao mbali ya  kuwaombra  radhi kwa kauli za matusi za mtia nia  huyo  bado alisema  watia nia  wote  walionywa  kuepuka  lugha  chafu badala ya  kunadi  sera  zao na kuwa kilichomkutano Mpangala ni matokeo ya kutoheshimu taratibu na  hivyo wamelazimika  kuvunja mkutano  huo ili  kuokoa usalama  wake.

Hali ya  upepo  wa kisiasa katika jimbo la Ludewa bado ni ngumu zaidi kwa  watia nia  hao wawili kutokana na wananchi kuonyesha imani yao na mbunge Filikunjombe na kila mkutano ambao akianza  kuomba  kura mbunge Filikunjombe wananchi wote  hutawanyika   huku wakiimba nyimbo za jembe letu kama ishara ya kumuunga mkoano na  kumpongeza mbunge  huyo kwa kazi aliyoifanya .



0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa