Home » » Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mh. Dk. Rehema Nchimbi afungua kikao kazi cha biashara ya kilimo

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mh. Dk. Rehema Nchimbi afungua kikao kazi cha biashara ya kilimo

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

1
Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mh. Dk. Rehema Nchimbi akifungua kikao kazi cha biashara ya kilimo kwa kongani ya Ihemi iliyoandaliwa na SAGCOT (Southern Agricultural Growth Corridor of Tanzania) kwa ushirikiano na UONGOZI Institute (Taasisi ya Uongozi Afrika kwa Maendeleo Endelevu) mapema leo Iringa mjini. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Kilimo wa TCCIA Bi. Magadalena Mkocha, Mwenyikiti wa Bodi ya Agricultural Council of Tanzania Dk. Sinare Y. Sinare, DC wa Iringa Mh. Angeline Mabula, DC wa Mufindi Mh. Mboni Mhita na Katibu Mkuu Kiongozi mstaafu Philemon Luhanjo.
2
  Katibu Mkuu Kiongozi mstaafu Philemon Luhanjo ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa bodi ya UONGOZI Institute akitoa salaam kwa niaba ya taasisi hiyo wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha biashara ya kilimo kwa kongani ya Ihemi inayoendelea Iringa mjini. UONGOZI Institute imeshiriki katika kuwezesha kikao kazi hicho.
3
Mkurugenzi Mtendaji wa SAGCOT Bw. Geoffrey Kirenga akitoa utangulizi wa mada ya biashara ya kilimo kwa nyanda za juu kusini. Mkutano huu wa siku mbili unakutanisha  viongozi wa serikalini, sekta binafsi, mashirika ya kimataifa pamoja na wakulima kwa ajili ya kujadili kuhusu kuboresha biashara ya kilimo nchini kwa nyanda za juu kusini.
4
Picha ya pamoja ya wageni waalikwa na washiriki wa kikao kazi cha biashara ya kilimo inayoendelea Iringa mjini. Mada zinazojadiliwa ni pamoja na wajibu wa viongozi katika kuleta mageuzi katika kilimo.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa