Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

CHEKI POMBE AINA YA ULANZI ILIVYO "DILI" NJOMBE


Ulanzi ukiandaliwa
Miti inayotengeneza pombe aina ya ulanzi ikiwa imestawi mashambani wilayani Makete
Mingine tayari imeshavunwa
Hii ndiyo michache iliyobakia baada ya kuvuna ulanzi
Hapa ulanzi ukipelekwa majini tayari kabisa kuwafikia watumiaji.Ulanzi ni moja ya bidhaa inayotegemewa sana na wananchi wengi wa mikoa ya nyanda za juu kusini ikiwemo Njombe kwa ajili ya kuwapatia kipato

CHANZO EDDY MO BLAZE BLOG

UKARABATI WA BARABARA YA MAKETE - NJOMBE SEHEMU ILIYOHARIBIWA NA MVUA WAANZA


Katapila likiwa eneo lililoharibiwa na maji ya mvua kwenye kipande cha lami barabara kuu ya Makete-Njombe katika kijiji cha Usungilo wilayani Makete tayari kabisa kurekebisha eneo hilo
 Ukarabati ukiendelea, mapipa yakiashiria hapo ndipo sehemu iliyoathiriwa na mvua 
 Huu udongo unaouona haukuwepo baada ya mvua kuusomba hali iliyosababisha eneo hili kumegeka na kumomonyoa lami, na huu ni udongo mpya uliojazwa wakati ukarabati ukiendelea
Kina mama wakiangalia eneo hilo linalofanyiwa ukarabati 
Hapa panapoonekana ndipo palipobomolewa na mvua, hivyo kwa hivi sasa pamejazwa kifusi kabla ya kufanyika utaratibu wa kurejesha lami kama palivyokuwa awali 
Wajameni hiki kibao kitasomeka kweli hasa kwa madereva ambao hawajui kama ujenzi unaendelea jirani? maana hii rangi waliyotumia kuandikia duuuuuu!
(Picha zote na Edwin Moshi)

Mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro Makete asisitiza amani




 Mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro

Na Edwin Moshi
Serikali wilayani Makete imewataka wananchi wa wilaya hiyo kuwa makini na kutoa taarifa kwa viongozi pale wanapokiona kitua ambacho hawakifahamu ama wanapomuaona mtu ama watu wageni ambao hawawafahamu katika maeneo yao

Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Makete Mh. Josephine Matiro wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake ikiwa ni siku kadhaa zimepita tangu kulipuka kitu kinachosadikika kuwa ni bomu katika kanisa moja jijini Arusha

Matiro amesema kufuatia tukio hilo lililotokea Arusha hakuna budi wananchi kuwa makini kwa kuwa kumekuwa na muingiliano wa watu ambao wanafika kwenye wilaya yake na wengi wao wakiwa wageni lakini hawatoi taarifa na pia hakuna mtu mwingine ambaye anatoa taarifa kuwa kuna watu wageni ambao hawafaamiki na wameingia kwenye eneo hilo

Amesema si lazima watu ama mtu huyo afike kwako lakini endapo ataonekana hata kwa jirani ni lazima utoe taarifa ili ahojiwe na kujulikana ametoka wapi.

“zamani kulikuwa na utaratibu mzuri ambao hivi sasa tutaurejesha, watu walikuwa hawakubali kumpokea mtu yeyote mgeni bila taarifa zake kujulikana wazi ikiwemo kwa viongozi, lakini hivi sasa hicho kitu hakipo” alisema Matiro

Katika hatua nyingine mkuu huyo amewataka wale wote wenye kanda ama CD zenye uchochezi wa kidini kuzisalimisha kwenye vyombo vya usalama kwa kuwa ni kosa kisheria na atakayekamatwa nazo atachukuliwa hatua za kisheria

Amesema cd hizo zinachochea uvunjifu wa amani na zitaweza kupelekea vita ya kidini ambyo ni vita hatari kuliko zote, hivyo kuwataka wenye nazo kuzipeleka wenyewe kwenye vyombo vya usalama na kusisitika kila mtu kulilinda amani iliyopo wilayani mwake isivunjike

Mwanafunzi ajinyonga Njombe

WATU watatu wamekufa mkoani Njombe katika matukio tofauti likiwemo la ajali iliyosababisha mwanafunzi kupoteza maisha  na wengine wawili kujinyonga.

Kamanda wa polisi mkoani Njombe kamishna msaidizi wa polisi Fulgence Nginyani amesema katika tukio la kwanza, la april 19 saa 11 jioni katika maeneo ya uwanja wa polisi makambako, mwanafunzi aliyetambuliwa kwa jina la jina la Helen Mwitula (9) mwanafunzi wa shule ya msingi Mwembetogwa  darasa la tatu alikufa baada ya kugongwa na gari.

Kamanda Ngonyani amesema,ajali hiyo ilisababishwa na gari lenye namba T. 809 BHC double Cabin pick-up mali ya kampuni ya Jah- People investment  Ltd. ya mjini makambako lililokuwa likiendeshwa na dereva Seily Mtafya (28) ambapo katika ajali hiyo hiyo,mwanafunzi mwingine Joyce mwakipesile (9) amelazwa katika hospitali ya kkkt ilembula baada ya kuvunjika miguu yote miwili.

Katika tukio jingine april 19 Oktar Mahenge (12) mwanafunzi wa darasa la na tano katika shule ya Lupalilo wilayani Makete alijinyonga hadi kufa kwa kutumia koti la suti nje ya nyumba yao.

Wakati huo huo, Ezekiel Haule (28) mkazi wa kijiji cha Kiwe kata ya Mawengi wilayani Ludewa alikutwa akiwa amekufa baada ya kujinyinga na kamba ya manila porini nje ya nyumba yake chanzo kinachunguza.

Afariki kwa kupigwa na kuvunjwa viungo vya mwili

MTU mmoja mwanaume amekufa wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Wilaya ya Kibena mkoani Njombe, baada ya kukutwa akiwa amepigwa na watu wasio julikana mjini Makambako.

Kamanda wa polisi,kamishna wa polisi mkoani humo, Fulgence Ngonyani, amemtaja mtu huyo kuwa ni Peles Sanga (33) mkazi wa mji mwema makambako ambaye Aprili 10 saa 10 alfajiri alipokutwa katika pipeline akiwa amevunjwa miguu yote miwili, na mkono wa kulia kisha kutelekezwa eneo la tukio.

Kamanda Ngonyani amesema, mtu huyo aliokotwa na wasamalia kisha kufikishwa katika kituo cha afya ambapo alihojiwa na kueleza bayana kuwa alitoka matembezini na kuvamiwa na watu watatu ambao walivalia makoti meusi marefu,ambao baada ya kumjeruhi walitokomea kusiko julikana.

Marehemu alifikishwa kibena na kuanza matibabu ambapo hata hivyo alikufa saa 6 mchana april 11, baada ya  kuvuja damu nyingi katika majeraha, na jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi kuhusiana na tukio hilo.

HASSAN MAAJAR TRUST YAKABIDHI MADAWATI 680 KWA RC WA NJOMBE.



 Mkuu wa mkoa wa NjombeKaptain Mstaafu Asseri Msangi katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi.

 Mkuu wa mkoa wa Njombe Kaptain Mstaafu Asseri Msangi (aliyekaa wa pili kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi Hassan Majaar Trust Bi. Zena Maajar Tenga (waliosimama wa pili kushoto) na Mwakilishi kutoka Kampuni ya Tigo pamoja na baadhi ya Walimu na Wanafunzi wakiwa katika picha ya ukumbusho.

Wanafunzi wakionyesha furaha baada ya kuboreshewa mazingira ya kusoma na Taasisi ya Hassan Maajar Trust ambayo lengo lake ni kutatua tatizo la Madawati nchini na kuhakikisha kauli mbiu yao ya “Dawati kwa kila mwanafunzi” inatimia.
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa