Home » » Afariki kwa kupigwa na kuvunjwa viungo vya mwili

Afariki kwa kupigwa na kuvunjwa viungo vya mwili

MTU mmoja mwanaume amekufa wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Wilaya ya Kibena mkoani Njombe, baada ya kukutwa akiwa amepigwa na watu wasio julikana mjini Makambako.

Kamanda wa polisi,kamishna wa polisi mkoani humo, Fulgence Ngonyani, amemtaja mtu huyo kuwa ni Peles Sanga (33) mkazi wa mji mwema makambako ambaye Aprili 10 saa 10 alfajiri alipokutwa katika pipeline akiwa amevunjwa miguu yote miwili, na mkono wa kulia kisha kutelekezwa eneo la tukio.

Kamanda Ngonyani amesema, mtu huyo aliokotwa na wasamalia kisha kufikishwa katika kituo cha afya ambapo alihojiwa na kueleza bayana kuwa alitoka matembezini na kuvamiwa na watu watatu ambao walivalia makoti meusi marefu,ambao baada ya kumjeruhi walitokomea kusiko julikana.

Marehemu alifikishwa kibena na kuanza matibabu ambapo hata hivyo alikufa saa 6 mchana april 11, baada ya  kuvuja damu nyingi katika majeraha, na jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi kuhusiana na tukio hilo.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa