Home » » Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda apokea mitambo ya kisasa ya kutengenezea barabara na miundombinu mingine kwa ajili ya Halmashauri ya Mji wa Njombe

Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda apokea mitambo ya kisasa ya kutengenezea barabara na miundombinu mingine kwa ajili ya Halmashauri ya Mji wa Njombe

Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akipokea mfano wa Ufunguo kutoka kwa Mkurugenzi wa kamapuni ya GF Trucks & Equipment Ltd ya jijini Dar es Dar es Salam Bw. Imran Karmali baada ya makabidhiano ya Mitambo ya Kisasa ya kutengeneza Barabara na miundombinu kwa ajili ya Halmashauri ya Mji wa Njombe. Mitambo hiyo imenunuliwa kwa gharama ya Tsh. Million 700 kwa makubaliano maalum ya mkopo nafuu usiokuwa na riba. Kulia ni Mwenyekiti wa Kampuni ya GF Trucks & Equipment Ltd Mehboob Karmali na aliye kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Njombe George Mkindo.
Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akijaribu mojawapo ya mitambo hiyo mara baada ya kukabidhiwa rasmi kwa ajili ya Halmashauri ya Mji wa Njombe. Pembeni yake ni Mkurugenzi wa kamapuni ya uuzaji mitambo hiyo ya Jijini Dar es Salaam ya GF Trucks & Equipment Ltd Bw. Imran Karmali.
Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akifurahia mojawapo ya mitambo ya kisasa ya kutengenezea barabara na miundombinu mingine iliyonunuliwa na Halmashauri ya Mji wa Njombe kutoka Kampuni ya GF Trucks & Equipment Ltd. Pembeni yake ni Mkurugenzi wa kampuni hiyo Imran Karmali, Mwenyekiti wa Kampuni hiyo Bw. Mehboob Karmali na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Njombe George Mkindo.
Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akimkabidhi mfano wa Ufunguo wa Mitambo hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Mji wa Njombe George Mkindo mara baada ya kuipokea kutoka kampuni ya GF Trucks & Equipment Ltd ambayo ndio walioiuzia Halmashauri hiyo mitambo hiyo.
Spika wa Bunge akitoa shukrani zake kwa uongozi wa Kampuni ya GF Trucks & Equipment Ltd kwa kuiwezesha Halmashauri ya Mji wa Njombe kupata Mitambo ya kisasa ya kutengenezea barabara na miundombinu mingine iliyonunuliwa na Halmashauri ya Mji huo.
Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akimsikiliza kwa makini Afisa Mauzo Mwandamizi wa kampuni ya GF Trucks & Equipment Ltd Mhandisi Juma Hamsini alipokuwa akielezea ubora wa mitambo ya kampuni hiyo kabla ya kumkabidhi rasmi Mhe. Spika kwa ajili ya Halmashauri ya Mji wa Njombe. Mitambo hiyo imenunuliwa kwa gharama ya zaidi ya Milion 700 za Kitanzania kwa makubaliano ya mkopo usiokuwa na riba kutoka Mfuko wa Halmashauri ya Mji wa Njombe. Kulia kwa Mhe. Spika ni Mwenyekiti wa Kampuni ya GF Trucks & Equipment Ltd Mehboob Karmali na walioko kushoto ni watendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo wakiongozwa na George Mkindo (mwenye koti)Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Njombe George Mkindo akitoa pongezi zake kwa kampuni ya uuzaji wa mitambo ya ujenzi ya GF Trucks & Equipment Ltd baada ya kukubali kuizia Halmashauri yake Mitambo ya kutengenezea barabara na miundombinu mingine katika Halmashauri ya Mji wa Njombe kwa Mkopo usio kuwa na Riba wa kiasi cha Million 700 za Kitanzania.
Mhe. Makinda akifanya mahojiano na waandishi wa habari mara baada ya kupokea mitambo hiyo.
Picha na Owen Mwandumbya wa Bunge.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa