Home » » Mtihani wa Kidato cha Sita unaendelea vizuri

Mtihani wa Kidato cha Sita unaendelea vizuri

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 



Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako

BARAZA la Mitihani Tanzania (NECTA) limesema Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita na ule wa Ualimu, umeanza vizuri katika maeneo yote nchini. Akizungumza jana ikiwa ni siku ya pili tangu kuanza kwa mtihani wa taifa, Ofisa Habari wa Necta, John Nchimbi alisema mtihani huo umeanza kwa wakati uliopangwa na umefanyika katika hali ya utulivu na na amani.
“Taarifa za kanda zote zinaonesha kuwa mtihani umeanza vizuri maeneo yote, kwa wakati na umefanyika katika mazingira ya utulivu kama taratibu za mtihani zinavyotaka,” alisema Nchimbi. Mtihani wa Kidato cha Sita ulianza Jumatatu na utafanyika hadi Mei 19, mwaka huu wakati ule wa Ualimu utafikia tamati Mei 13, mwaka huu.
Jumla ya watahiniwa 74,920 wanafanya mtihani wa kuhitimu Kidato cha Sita katika shule mbalimbali nchini huku watahiniwa 11,597 wakifanya mtahini wa ualimu. Kati ya watahiniwa hao waliosajiliwa, watahiniwa 65,610 ni watahiniwa wa shule huku watahiniwa wa kujitegemea wakiwa 9,310.
Kati ya watahiniwa wa shule 65, 610, wasichana ni 24,549 na wavulana ni 41,061 huku watahiniwa wa kujitegemea wasichana wakiwa ni 3,176 na wavulana ni 6,134. Kwa upande wa mtihani wa ualimu, watahiniwa 11,597 wanafanya mtihani wa Ualimu.
Kati ya hao watahiniwa 10,942 wanafanya mtihani wa Ualimu daraja A na watahiniwa 654 wanafanya mtihani wa Diploma ya sekondari na mmoja anafanya mtihani wa Ualimu wa Diploma ya Ufundi.
Chanzo Gazeti la Habari leo
 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa