DK MAGUFULI ATOA MPYA TENA AFANYA MAZOEZI YA NGUVU JUKWAANI MAKAMBAKO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli akifanya mazoezi jukwaani akijiandaa kujinadi kwa wananchi katika Mji wa  Makambako, mkoani Njombe leo,  jambo ambalo lilizua vifijo, nderemo na vigelegele kutoka kwa wananchi waliofurika kwenye mkutano huo wa kampeni.PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG


 Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli akijinadi kwa wananchi  kwa kuwaomba ifikapo Oktoba 25, mwaka huu wakati wa Uchaguzi Mkuu, waende wote kumpigia kura za ndiyo ili ashinde kwa kishindo urais.
 Wakazi wa Mwanjelwa, jijini Mbeya, wakimsikiliza Dk Magufuli akijinadi kwao baada ya msafara wake kuzuiwa eneo hilo ukitokea Uwanja wa Ndege wa Songwe ukienda Mbarali kuendelea na kampeni.
 Dk Magufuli akiomba kupigiwa kura na wananchi wa Nswisi wilayani Mbarali huku akirekodiwa na Shaban Kwaka wa TBC.

 Mama mkazi wa Igurusi wilayani Mbarali Mbeya, akifurahi baada ya kumuona Dk Magufuli.PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Dk Magufuli akizungumza na wananchi wa Igurusi waliouzuia msafara wake

 Wananchi wakimshangilia Dk Magufuli alipokuwa akihutubia na kuomba kura kwao katika Mji wa Chimala, Mbarali mkoani Mbeya leo.
 Mfuasi wa CCM, akishangilia huku akiwa na picha ya Dk Magufuli  wakati wa mkutano wa kampeni Rujewa wilayani Mbarali, Mbeya leo.
 Waziri Mkuu mstaafu,  Samuel Malecela akitangaza wasifu wa Dk Magufuli na kwamba niye anayefaa kuchaguliwa kuwa rais tofauti na mgombea wa Ukawa, Edward Lowassa.
 Sehemu ya wananchi wakiwa katika mkutano wa kampeni Rujewa leo
 Wananchi wakimshangilia Dk Magufuli wakati wa mkutano huo na kukubali kumpigia kura za ndiyo
 Dk Magufuli akimnadi mgombea ubunge Jimbo la Mbarali,
 Ni furaha iliyoje kwa wananchi wa Mbarali baada ya kufurahishwa na ahadi mbalimbali za maendeleo alizokuwa akizitoa kwaoPICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Dk Magufuli akimpokea mmoja wa wanachama wa chama cha ACT -Wazalendo aliyeamua kujiunga na CCM wilayani Mbarali
 Dk Magufuli akimnadi Mgombea ubunge jimbo la Wanging'ombe, Gerson Lwenge katika Mji wa Ilembula, mkoani Njombe. Lwenge alikuwa Naibu waziri wa ujenzi wilazara iliyokuwa akiiongoza yeye
 Wananchi wa Ilembula wakimsikiliza Dk Magufuli akijinadi
 Moja ya mabango yalyokuwepo katika mkutano wa kampeni za CCM, mjini Makambako,
 Mgombea ubunge Jimbo la Makambako, Jah People akijinadi kwa wananchi katika mkutano wa kampeni mjini Makambako ambapo pia alimuombea kura Dk Magufuli
 Huree Dk Magufuli
 Jah People akiibusu picha ya Dk Magufuli ikiwa ni ishara ya kumkubali kuwa rais
 Mjumbe wa Kamati ya Kampeni za CCM, Abdallah Bulembo akitangaza wasifu wa Dk Magufuli na kwamba anafaa kuchaguliwa kwa kura nyingi kuwa Rais wa Tanzania mjini Makambako, mkoani Njombe.
 Wananchi wakifurahia hotuba ya Dk Magufuli
 Dk Magufuli akiwa na baadhi ya waliovihama vyao vya upinzani na kuamua kujiunga na CCM wakati wa mkutano mjini Makambako

Dk Magufuli akihutubia katika mkutano wa kampeni mjini Mafinga, wilayani Mufindi

LOWASA ALIVYOPOKELEWA NJOMBE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akiwasili kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Matarawe, Songea Mjini, Mkoani Ruvuma leo Septemba 1, 2015, ambako kumefanyika Mkutano wa Kampeni zake anazoendelea nazo kwa nchi nzima. Mh. Lowassa amepata mapokezi makubwa sana mkoani hapo, akitokea Mkoa wa Njombe.

MTOTO HAPPY LIMWAMWA (9-10) AKIMBIA KIPIGO ALIPOKUWA AKIFANYA KAZI ZA NDANI NJOMBE‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
  Happy  Limwamwa (9-10) Pichani
   Happy  Limwamwa 9-10 (kushoto) akizungumza kwa uchungu  kwa Msaidizi wa Kisheria Geophrey Kaduma, (wapili kulia)  manyanyaso aliyokuwa akiyapata toka kwa mama aliyekuwa amemtowa kwao Wilaya ya  Mbinga Mkoa wa Ruvuma, kwa malengo ya kufanya kazi za ndani, ndipo alipokutana na kichapo toka kwa mama huyo na mume wake na kumfanya akimbiye na kuishi mitaani na kuokotwa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bryceson Mgaya wa Mtaa wa Kambarage Kata ya Njombe Mjini  Wilaya  ya Njombe Mkoa wa Njombe, Pamoja na Mwenyekiti huyo kutowa taarifa katika kituo cha Polisi na kumtembeza katika mitaa tofauti alipokuwa akifanya kazi  zaidi ya wiki 3  bado juhudi yoyote haijazaa matunda kwa  mtoto huyo kurudishwa kwao, kwa yoyote anaye weza kumfaham mtoto huyo awasiliane na Mwenyekiti huyo wa Mtaa, 0766336403, Mwenyekiti wa Kituo cha Sheria Geophrey Kaduma, 0759601915-o655601915. wapili kushoto ni Katibu wa Kituo cha Msaidizi wa Kisheria Magy Mtalla na wakwanza kulia ni mke wa mwenyekiti wa Mtaa wa Kambarage Matha Maiseli (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)
 Katibu wa Kituo cha Msaidizi wa Kisheria Magy Mtalla, akizungumza na mtoto huyo Happy  Limwamwa 9-10
Happy  Limwamwa 9-10 akiwa katika picha

Na Khamisi Mussa
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa