MAGUFULI AZIDI KUCHANJA MBUGA,AWATAKA WANANCHI WAWEKE IMANI KUBWA KWAKE NA KUMPA KURA NYINGI ZA USHINDI‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi (CCM),Dkt John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi wa Njombe mjini katika mkutano wa hadhara wa kampeni uliofanyika jioni ya leo katika uwanja wa saba saba.Magufuli amesema akichaguliwa kuwa rais wa awamu ya tano ataendeleza juhudi zake za kujenga barabara kwa kiwango cha lami,amesema dhamira yake aliokuwa nayo ya Uwaziri wa Ujenzi katika kujenga barabara za lami katika maeneo yote hapa nchini.

Amesema tangu kupewa kuwa waziri wa ujenzi ameweza kujenga barabara  zaidi kilomita 7000 nchi nzima,ambapo ilipelekea kuongeza kuongeza pato la mfuko wa barabara kutoka bilioni 73,3 hadi kufikia bilini 866 kwa mwaka huu hivyo ameahidi akiwa rais atajenga zaidi barabara za lami.

Dkt MAGUFULI ambae anaendelea na mikutano ya kampeni za Urais mikoa ya nyanda za juu kusini , amelalamikia udanganyifu wa baadhi ya mitandao ya kijamii  na baadhi ya vyombo vya habari kuripoti  kuwa amelazwa wodi ya wagonjwa mahututi katika hospitali ya mkoa wa mbeya wakati sio kweli.

Aidha pia Magufuli  amewaomba wananchi waweke imani kubwa kwake kwa  kumpa kura nyingi  zitakazomwezesha kuwa raisi wa awamu ya tano,na kIsha alipe fadhira hizo kwa kutatua kero zinazowakabili hasa wananchi wenye kipato cha chini.

PICHA NA MICHUZI JR-NJOMBE
 Mgombea Urais wa CCM Dkt Joh Pombe Magufuli akipeana mkono na Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara,Ndugu Phillip Mangula mara baada ya kumkaribisha mgombea huyo jukwaani kuwahutubia wananchi wa njombe na kuzinadi sera za chama chake na kuomba ridhaa ya kuiongoza Tanzania katika kipindi cha awamu ya tano
 Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara,Ndugu Phillip Mangula akiwashukuru wananchi wa Njombe waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni,uliofanyika jioni ya leo katika uwanja wa sabasaba mjini humo,ambapo pia Ndugu Mangula alimkaribisha mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli kuwahutubia wananchi wa njombe na kuzinadi sera za chama chake na kuomba ridhaa ya kuiongoza Tanzania katika kipindi cha awamu ya tano
 Wananchi wa Njombe wakimsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dkt John Magufuli kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika jioni ya leo kwenye uwanja wa sabasaba mjini Njombe.
 Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM na Mgombea Ubunge wa jimbo la Kyela,Mh Harrison Mwakyembe akiwahutubia wananchi wa Njombe jioni ya leo kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni
 Waanchi wakishangilia jambo kwenyemkutano wa kampeni wa CCM.

 Mgombea Urais wa CCM,Dkt John Pombe Magufuli akimnadi mgombea Ubunge wa jimbo la Wanging'ombe Mh. Gerson Lwenge kwa wananchi wa Makoga ndani ya wilaya hiyo ya Wanging'ombe
 Mgombea Urais wa CCM,Dkt John Pombe Magufuli akimkabidhi Ilani ya CCM mgombea Ubunge wa jimbo la Wanging'ombe Mh. Gerson Lwenge kwa wananchi wa Makoga ndani ya wilaya hiyo ya Wanging'ombe kwa ajili ya kuwaambia wananchi ni namna gani wataiongoza Tanzania katika awamu ya tano. 
  Mgombea Urais wa CCM,Dkt John Pombe Magufuli akimnadi mgombea Ubunge wa jimbo la Makete Dkt Norman Msigala kwa wananchi wa Makoga ndani ya wilaya hiyo ya Wanging'ombe
 MKutano wa Kampeni ukiendelea. 
 Wananchi wakisikiliza sera za mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli,hayupo pichani alipowahutubia jioni ya leo mjini Njombe. 
 Wananchi wakiwa katika mkutano wa hadhara wa kampeni
 Wananchi wakiwa na mabango yao ya kumsifu na kumkaribisha mgombea Urais wa CCM Ndugu John Pombe Magufuli,mara baada ya kufunga barabara alipokuwa akipita katika kijiji cha Mgagala akielekea mkoani Njombe kwenye mkutano wa kampeni
 Wananchi na Mabango yako
 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi wa Makoga katika wilaya ya Wanging'ombe mapema leo mchana.
 Wananchi  wa kijiji cha Ikonda wakimsikiliza Dkt Magufuli 
 Bango .



DK AZIDI KUWACHANGANYA WAPINZANI KAMPENI ZA URAIS NJOMBE‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk John Magufuli akihutubia katika mkutano wa hadhara wa kampeni kwenye Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe
Makamu Mwenyekiti wa CCM, Tanzania Bara, Philip Mangula akihutubia kwa kumnadi Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk John Magufuli  katika mkutano wa hadhara wa kampeni kwenye Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe

 Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk John Magufuli akimtambulisha Naibu Waziri wa Ujenzi, ambaye anagombea ubunge Jimbo la Njombe Kaskazini, Gerson Lwenge katika mkutano wa hadhara wa kampeni wilayani Wanging'ombe, mkoani Njombe
 Msanii wa muziki wa kizazi kipya  Shilole akitumbuiza leo kwenye mkutano wa kumnadi Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM kwenye Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe.
Dk Magufuli akitoa shukrani kwa viongozi wa CCM Mkoa wa Mbeya baada ya kumaliza ziara mkoani humo  na kuanza kampeni katika Mkoa wa Njombe
  Dk.Magufuli akijinadi kwa wananchi na kutoa ahadi  katika nKijiji cha Igoma, Mbeya Vijijini aliposimama kwa muda akielekea Makete mkoani Njombe kuendelea na kampeni.  Akichaguliwa ameahidi kujenga barabara  ya lami ya Njombe hadi Mbeya kuptia Makete na kijijini hapo. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Wananchi wakishangilia baada ya kuelezwa na Dk Magufuli kuhusu ijenzi wa barabara ya lami itakayopita kijijini hapo
 Wananchi wakimshangilia Dk Magufuli kijijini hapo
 Dk Magufuli akijinadi katika Kijiji cha Ilungu Mbeya Vijijini mpakani na Mkoa wa Njombe
 Wananchi wakishangilia huku wakiwa na vipeperushi vyenye picha za Dk Magufuli
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), ambaye pia alikuwa Mbunge wa Jimbo la Makete,  Binilith Mahenge akimpigia debe Dk Magufuli pamoja na Mgombea ubunge wa Jimbo la Makete, Norman Sigalla.
 Dk. Magufuli akijinadi kwa wananchi katika mkutano uliofanyika Iwawa wilayani Makete
 Dk Magufuli akimtambulisha mgombea ubunge jimbo la Makete, Dk Norman Sigalla katika mkutano wa kampeni uliofanyika Iwawa Makete
 Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Wenye Ulemavu nchini, Amon Mpanju akimpigia debe Dk Magufuli eneo la Iwawa wilayani Makete
 Wananchi wakimsikiliza kwa makini Dk Magufuli mjini Makete
 Dk Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafuasi wa vyama vya upinzania waliovihama vyama vyao na kujiunga na CCM katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika  Iwawa, Makete leo.PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG

 Mmoja wa wafuasi wa Chadema akiwa amesamama karibu na pikipiki yenye bendera ya chama hicho huku akimsikiliza kwa makini Dk Magufuli akijinadi katika Kijiji cha Kenja, wilayani Makete leo.
 Mfuasi wa Chadema (kulia) akishangilia baada ya kumsikia Dk Magufuli akitangaza kwamba akichaguliwa kuwa urais watoto watakuwa nasoma bure kuanzia darasa  la kwanza hadi kidato cha nne. Kutano huo ulifanyika katika Kijiji cha Kenja wilayani Makete baada ya msafara kuzuiwa wananchi katika eneo hilo wakiwa na hamu ya kusikiliza sera zake.
 Baadhi ya wananchi katika Kijiji cha Kenja wakimsikiliza Dk Magufuli huku wakiwa na mabango yenye picha za mgombea huyo wa urais wa CCM
 Dk Magufuli akisisitiza jambo katika mkutano uliofanyika katika Kijiji cha Kenja wilayani Makete
 Mjumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya CCM,  William Lukuvi akizungumza na Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Philip Mangula katika mkutano wa kampeni wilayani Wangi ng'ombe, Mkoa wa Njombe leo
 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Pindi Chana akihutubia katika kutano wa kampeni wa kumnadi Dk Magufuli wilayani Wanging'ombe mkoani Njombe leo

 Makamu Mwenyekiti wa CCM, Tanzania Bara, Philip Mangula akisalimiana na Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk John Magufuli katika mkutano wa hadhara wa kampeni wilayani Wanging'ombe, mkoani Njombe
 Wananchi wa Kijiji cha Igagala wakiwa na mabango yenye ujumbe mbalimbali walipokuwa wakimlaki Dk Magufuli, wilayani Wanging'ombe, Njombe
 Dk Magufuli akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Igagala, wilayani Wanging'ombe
 Wananchi wakiwa katika mkutano wa kampeni wa CCM mjini Njombe
Msanii Cgegge akitumbuiza katika mkutano wa kampeni za CCM kwenye Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe leo

WANACHAMA WA CHADEMA ZAIDI YA 500 LUDEWA WAHAMIA ACT WAZALENDO ,WACHUKIZWA NA LOWASA KUPOKELEWA CHADEMA NA KUKATWA KWA MSHINDI WA KURA ZA MAONI‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Add caption
Wanachama  wa Chadema wilaya ya  Ludewa  mkoa wa  Njombe  wakiandamana  kupinga  maamuzi ya  chama  hicho  kukata  jina la mshindi  wa  kura  za maoni na  kumteua  aliyeshindwa ,mbali ya  kuandamana  pia  wanachama  hao  zaidi ya  500  walikihama  chama  hicho na  kujiunga na  ACT  Wazalendo
Wanachama  wa  Chadema  waliohamia ACT wazalendo  wakiwa na  mabango ya  kukituhumu  chama   hicho  kwa  kukiuka  Demokrasia


kadi na nyalaka  za Chadema  zikichomwa moto
Wanachadema  wakiwa  nje ya  ofisi ya  ACT  Wazalendo  ambako  walifika  kuomba  kujiunga huko
kadi  za  chadema  zikiteketezwa  kwa  moto


wana chadema  wakiwa na mabango
Hasira  za  kukatwa  kwa  mshindi  wa kura  za maoni Ludewa


wanachadema  wakijiandaa kwa maaandamano ya amani  kujiengua na  Chadema  na  kujiunga  ACT  wazalendo
Bango  likimtaka  aliyeteuliwa na chama  kwenda  kugombea  jimbo la Hai kwa Mbowe


Add caption
Mwanzo  wa maandamano ya  kujiengua na  Chadema
Add caption
wana Chadema katika maandamano  ya  kupinga  uonevu ndani ya  chama
Tuhuma  dhidi ya  Chadema Taifa


Wanachadema  katika maandamano ya  kupinga mshindi  kutemwa


Wanachadema  waliojiengua na  kujiunga na ACT  wazalendo  wakiwa nje ya ofisi ya  Chadema  wilaya ya  Ludewa
barua  ya  tuhuma  za  mteuliwa  kutoa  ahadi ya  rushwa hii hapa

barua  ikionyeshwa  kwa  wanahabari na  wanachadema
Ni  full jaziba  kwa  wana Chadema  Ludewa
Wanachadema  wakiwa  nje ya  ofisi   ya chama  wilaya  walikokwenda  kurudisha  kadi kabla ya  kuhamia ACT wazalendo
Aliyekuwa mwenyekiti wa BAWACHA  wilaya ya  Ludewa akionyesha  kadi ya  ACT  wazalendo
Aliyeenguliwa Bw  Haule  akiwapongeza wana Chadema kwa kuhamia pamoja  ACT  wazalendo
Wanachadema  wakirudisha  kadi  za chamna  hicho na kujiunga na ACT  wazalendo
Baadhi ya  nguo  na kadi  zikiandaliwa  kuchomwa  moto
katibu wa ACT  wazalendo  Ludewa Alfred Ulaya  akionyesha kadi  za  Chadema 
Wanachadema  wakijipata  kuhamia  ACT wazalendo
Kadi  zikiwa  zimekusanywa kwa kuchomwa  moto
mwana  Chadema  akichoma  moto kadi  za  Chadema Ludewa  kupinga  uonevu  ndani ya  chama  hicho
Add caption
Hivi  ndivyo kadi  zinavyoteketezwa  kwa  moto  baada ya  wana Chadema  kujiengua na  chama  hicho na kujiunga na ACT  wazalendo 














Mabango  ya  kuagana na Chadema  kwa  wana Ludewa






Bango  likionyesha  Chadema kura  za Chadema  Urais X ,Ubunge X na udiwani X huku  likimaliza kwa  kusema  msituchagulie




Mwanachama wa Chadema  akiongea  kwa jazba  juu ya hali ya mambo ndani ya  Chadema kabla ya  kujiunga na ACT  wazalendo
Ofisi ya  Chadema  wilaya  ikiwa  imefungwa  wakati  wanachadema  walipofika  kurudisha  kadi zao


Kadi  ya  ACT  baada ya  kuhama  Chadema
Makada  wapya  wa ACT  kutoka  Chadema 


Aliyekuwa mshindi wa kura za maoni  akionyesha  barua  nyenye  siri nzito  za  mteuliwa  kununua nafasi hiyo
Bw Haule  akijiandaa  kuchoma moto vifaa vyake vya Chadema kabla ya  kujiunga na ACT wazalendo
........................................................................................................   


*Wafanya Maandamano Makubwa. Wachoma Moto Kadi
* Ofisi  ya Chadema Wilaya  Nusuru  Ichomwe Moto;  Viongozi  wakimbia; Watelekeza ofisi
 Na MatukiodaimaBlog,Ludewa
WANACHAMA zaidi  ya 500 wa  Chama  Cha  Demokrasia  na Maendeleo ( Chadema)  Wilayani Ludewa  Mkoani  Njombe wamekihama  chama  hicho  na kujiunga na  chama  cha  ACT Wazalendo   wakipinga  hatua ya  uongozi  wa  juu  wa  chama  hicho kukata  jina  la  mshindi  wa  kwanza wa  kura  za maoni Bw. Ocol Haule  na kumteua aliyekuwa mshindi  wa  pili katika mchakato huo Bw Bartholomeo Mkinga .

Wanachama  hao ambao  kutoka  kata  mbali mbali  za  wilaya  ya  Ludewa wamefanya maandamano hayo ya amani leo  kuelekea   ofisi ya  Chadema  wilaya  huku wakitishia    kuichoma moto  ofisi  hiyo  baada ya  viongozi  wake  kuifunga,  kuitelekeza  na kukimbia kunusuru maisha yao. 

Wakizungumzia  hatua   hiyo ya kupinga  maamuzi ya  chama ngazi ya  taifa wanachama hao Bi Hongera  Gama,  Taukile Mapunda  na aliyekuwa  Mwenyekiti  wa Baraza la  Wanawake  (BAWACHA) wilaya ya Ludewa Bi. Sophia Mtega  walisema  kuwa wanachama  walikuwa na  imani  kubwa na mshindi  wa kura  za maoni  kwani alifanya kazi kubwa ya kukijenga chama na sio  huyo  waliomuacha katika  kura  za maoni .

“Kinachoendelea sasa hivi ndani ya CHADEMA ni ufisadi mtupu,” alisema Bi. Gama akiongeza kuwa yeye binafsi alitoka  CCM na  kujiunga na Chadema  kutokana na  mapungufu  yaliyokuwepo   ndani ya  CCM  ila  kinachoendelea  kwa  sasa  ndani  ya  Chadema  anajuta kuingia Chadema  na  hivyo  ameamua  kuhama chama  hicho  kumfuata mtu  wao  waliyemchagua popote atakakokwenda .

“ Mwenendo  wa  chadema  kwa  sasa ni  wa  ovyo  zaidi  kuliko  chama  chochote  cha siasa hapa nchini tulikuwa  tukishuhudia  CCM  watu  wakikatwa ila  leo  ndani  ya Chadema  imekuwa  ni kawaida  kuona  wale  waliochaguliwa na  wanachama kukatwa na   watu  wachache akiwemo  mwenyekiti  wa Taifa  wa  chama  hicho Freeman Mbowe …..tumechoka tunahitaji kwenda  kupata Demokrasia ya  kweli ACT wazalendo sio  ndani ya  chadema”

Huku Bw Mapunda akidai  kuwa siasa  za  ukabila  zinaendelea  kukitesa  Chadema  na  kuwa  suala   hilo  la ukabila  na  kuwakumbatia  mafisadi  ndilo  ambalo  linaendelea  kukitafuna chama hicho pia  siasa za  ukanda na  kukumbatia  ufisadi  imekuwa ni kawaida  Chadema.

Hivyo alisema  katika kuhakikisha  wana  Chadema  wilaya ya  Ludewa na   kote  nchini  wanapinga siasa  za  ukanda na zile za kuwachukua  watu  wenye  tuhuma  za  ufisadi kugombea  ndani ya  chama  hicho  ni lazima  wanachadema  kuungana  kupinga hali  hiyo  kwa  kuhama  ndani  ya  chama  hicho na  kujiunga na ACT  wazalendo.

Aliyekuwa  mwenyekiti wa BAWACHA  wilaya ya  Ludewa Bi Mtenga  alisema  kuwa  uonevu  na  rushwa  vimechangia  wanachama na  wananchi kukosa  imani kabisa na  chama  hicho na  sasa badala ya  kuwa chama cha  wanyonge  kimekuwa ni chama  cha  wenye  pesa na mafisadi jambo ambalo  wao kama  wananchi wa chini hawapo  tayari  tena  kukaa ndani ya  Chadema.

Akimkaribisha  mgombea ubunge   huyo  aliyekatwa ndani  ya  Chadema  Bw Haule na  wanachama  zaidi ya 500 wa  chadema , katibu  wa  ACT wazalendo  wilaya ya  Ludewa Bw Alfred Ulaya  alisema  kuwa  pia  alipata  kuwa  kiongozi  ndani ya  Chadema  wilaya  ya  Ludewa  ila alihama  pamoja na  viongozi  wengine  kutokana na siasa  za chuki ndani ya chama  hicho na hatua ya  kukumbatia  ufisadi.

Hivyo  alisema  wanachama  hao  hawajachelewa  kujiengua na chadema na kujiunga na chama cha  ACT  wazalendo kwani ni chama chenye  misingi  bora na chama pekee  chenye malengo sahihi ya kulikomboa  Taifa  na Chadema na  pamoja na umoja  wao  wa vyama  vinavyo unda katiba ya  wananchi (UKAWA) ni CCM B  hivyo  lazima watanzania  wapenda mabadiliko lazima  kuchagua ACT wazalendo.

Katibu  huyo  alisema  kwa  wanachama  wote  ambao  wamejiengua na Chadema na kujiunga na ACT wazalendo wakiwemo makatibu na  wenyeviti wa kata   zaidi ya 10  waliojiunga na ACT wazalendo na viongozi  wengine  watakuwemo ndani ya  chama  hicho na vyeo  vyao kama  walivyotoka  Chadema.

Kwa upande  wake mgombea  huyo aliyeenguliwa  kugombea  ubunge  mbali ya  kushinda kura za maoni Bw Haule  alisema  kuwa kimsingi aliyeteuliwa  kugombea nafasi hiyo alikuwa amewaandikia barua baadhi ya  viongozi ngazi ya  wilaya  ya  kuwaahidi kuwapa  pesa ,kufungua  duka la  vifaa  mbali mbali pamoja na kuwahonga  pikipiki barua  ambayo aliinasa na  kuwaonyesha  wanachama  hao.

Pia  alisema kimsingi baada ya  kuenguliwa  kugombea nafasi hiyo  alitaka  kukaa kimya kama  aliyekuwa katibu mkuu wa Chadema Dr  Slaa ila  akaona  kukaa kimya  bado  si jibu na  hivyo kuamua  kujiunga na ACT wazalendo na  kuweka  uozo  huo  wazi.

Bw  Haule  alisema  kuwa kwa  sasa atahakikisha anazunguka jimbo nzima  kufikisha  kilio  chake kwa  wana Chadema  na  kupinga kwa nguvu  zote wagombea wa udiwani na ubunge wa Chadema kupewa kura na  kuwa kwa  sasa uhai  wa Chadema katika  wilaya  hiyo umekufa  rasmi .
 
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Njombe Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa